< Proverbios 31 >

1 Palabras del rey Lemuel, La profecía que le enseñó su madre:
Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
2 ¿Qué te diré, hijo mío? ¡Oh, hijo de mi vientre! ¿Qué te diré, hijo de mis votos?
“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
3 No des tu fuerza a las mujeres, Ni tus caminos al que destruye a los reyes.
Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
4 No es de reyes, oh Lemuel, Ni es de los reyes beber vino, Ni de los gobernantes el licor.
“Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
5 No sea que al beber, olviden lo que se decretó, Y perviertan el derecho de todos los afligidos.
wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
6 Den el licor fuerte al desfallecido, Y el vino a los de ánimo amargado,
Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
7 Para que beban y olviden su necesidad, Y ya no se acuerden de su miseria.
Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
8 Abre tu boca a favor del mudo, Defiende la causa de todos los abandonados.
“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
9 Abre tu boca, juzga con justicia Y defiende al pobre y al necesitado.
Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
10 Mujer virtuosa, ¿quién la hallará? Porque su estima sobrepasa largamente a la de las piedras preciosas.
Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
11 El corazón de su esposo está confiado en ella, Y no carecerá de ganancias.
Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
12 Ella le dará bien y no mal Todos los días de su vida.
Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
13 Busca la lana y el lino, Y diligentemente trabaja con sus manos.
Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
14 Es como la nave del mercader, Que trae su pan desde lejos.
Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
15 Se levanta cuando aún es noche, Da alimento a su familia, Y la porción asignada a sus criadas.
Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
16 Evalúa un campo y lo compra, Y del fruto de sus manos planta una viña.
Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Ciñe con firmeza su cintura, Y esfuerza sus brazos.
Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
18 Ve que sus negocios van bien. Su lámpara no se apaga de noche.
Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
19 Aplica sus manos a la rueca, Y sus dedos manejan el huso.
Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
20 Extiende su mano al pobre, Sí, alarga sus manos al necesitado.
Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
21 No tiene temor por su familia a causa de la nieve, Porque toda su familia lleva ropas dobles de color escarlata.
Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
22 Teje tapices para sí. De lino fino y púrpura es su vestido.
Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
23 Su esposo es conocido en la puerta Cuando se sienta con los ancianos de la tierra.
Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
24 [Ella] hace ropa de lino y la vende, Y provee cinturones al mercader.
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
25 Está vestida de fuerza y dignidad, Y sonríe ante el mañana.
Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
26 Abre su boca con sabiduría, Y la ley de la clemencia está en su lengua.
Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
27 Vigila la marcha de su casa, Y no come su pan de ociosidad.
Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
28 Sus hijos crecen, y la consideran inmensamente feliz, Su esposo también la alaba y dice:
Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
29 Muchas mujeres hicieron el bien, Pero tú las superaste a todas.
“Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 Engañosa es la gracia y vana la hermosura, La mujer que teme a Yavé será alabada.
Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
31 ¡Denle del fruto de sus manos, Y que sus mismas obras la alaben en la puerta!
Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.

< Proverbios 31 >