< Proverbios 29 >
1 El hombre que al ser reprendido es indómito, Será quebrantado de repente, Y no habrá para él medicina.
Mtu anayeendelea kuwa na shingo ngumu baada ya maonyo mengi, ataangamia ghafula, wala hapati dawa.
2 Cuando aumentan los justos, el pueblo se regocija. Cuando gobierna el impío, el pueblo gime.
Wenye haki wanapostawi, watu hufurahi; waovu watawalapo, watu hulia kwa huzuni.
3 El que ama la sabiduría, alegra a su padre, Pero el que se junta con prostitutas, destruye su riqueza.
Mtu apendaye hekima huleta furaha kwa baba yake, bali aambatanaye na makahaba hutapanya mali yake.
4 Un rey justo estabiliza el país, Pero el que lo carga de impuestos lo destruye.
Kwa haki mfalme huipa nchi uthabiti, bali mfalme aliye na tamaa ya rushwa huiangamiza.
5 El hombre que lisonjea a su prójimo Tiende una red a sus pasos.
Yeyote amsifuye jirani yake isivyostahili, anautandaza wavu kuitega miguu yake.
6 En la transgresión del hombre perverso hay trampa, Pero el justo cantará y se alegrará.
Mtu mbaya hutegwa na dhambi yake mwenyewe bali mwenye haki huweza kuimba na kufurahi.
7 Preocupa al justo la causa de los pobres, Y el perverso no entiende esa preocupación.
Mwenye haki hujali haki kwa ajili ya maskini, bali mwovu hajishughulishi na hilo.
8 Los burladores agitan la ciudad, Pero los sabios aplacan la ira.
Wenye mzaha huuchochea mji, bali watu wenye hekima hugeuzia mbali hasira.
9 Si un sabio contiende con un necio, Aunque se enoje éste o se ría, no tendrá reposo.
Kama mwenye hekima akienda mahakamani na mpumbavu, mpumbavu hukasirika na kudhihaki, wala hakuna amani.
10 Los hombres sanguinarios aborrecen al íntegro, Pero los rectos se preocupan por su vida.
Watu wamwagao damu humchukia mtu mwadilifu na hutafuta kumuua mtu mnyofu.
11 El necio da rienda suelta a su ira, Pero el sabio la reprime.
Mpumbavu huonyesha hasira yake yote, bali mwenye hekima hujizuia.
12 Si el gobernante atiende a palabras mentirosas, Todos sus ministros serán perversos.
Kama mtawala akisikiliza uongo, maafisa wake wote huwa waovu.
13 El pobre y el opresor tienen esto en común: A ambos Yavé les iluminó los ojos.
Mtu maskini na mtu anayeonea wanafanana kwa jambo hili: Bwana hutia nuru macho yao wote wawili.
14 Si el rey juzga a los pobres con verdad, Su trono será establecido para siempre.
Kama mfalme akiwaamua maskini kwa haki, kiti chake cha enzi kitakuwa thabiti siku zote.
15 La vara y la reprensión dan sabiduría, Pero el muchacho consentido avergonzará a su madre.
Fimbo ya maonyo hutia hekima, bali mtoto aliyeachiwa bila maonyo humwaibisha mama yake.
16 Cuando los perversos se multiplican, aumenta la transgresión, Pero los justos presenciarán la caída de ellos.
Wakati waovu wanapostawi, pia dhambi vivyo hivyo, lakini wenye haki wataliona anguko lao.
17 Corrige a tu hijo y te dará descanso, Y dará satisfacciones a tu alma.
Mrudi mwanao, naye atakupa amani, atakufurahisha nafsi yako.
18 Donde no hay visión profética, el pueblo se desenfrena. Pero, ¡inmensamente feliz es el que guarda la Ley!
Mahali pasipo na ufunuo, watu kujizuia, bali ana heri mtu yule aishikaye sheria.
19 El esclavo no se corrige solo con palabras, Porque entiende, pero no hace caso.
Mtumishi hawezi kuonywa kwa maneno matupu, ajapoelewa, hataitikia.
20 ¿Has visto a un hombre precipitado en sus palabras? Más esperanza hay del necio que de él.
Je, unamwona mtu azungumzaye kwa haraka? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko yeye.
21 El que mima a un esclavo desde la niñez, Al final lo tendrá como un hijo.
Kama mtu akimdekeza mtumishi wake tangu ujanani, atamletea sikitiko mwishoni.
22 El hombre iracundo levanta contiendas, Y el furioso comete muchas transgresiones.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi, naye mtu mwenye hasira ya haraka hutenda dhambi nyingi.
23 La soberbia del hombre lo abate, Pero el de espíritu humilde recibirá honra.
Kiburi cha mtu humshusha, bali mtu mwenye roho ya unyenyekevu hupata heshima.
24 El cómplice del ladrón aborrece su propia vida, Oye la maldición, pero no lo denuncia.
Anayekubaliana na mwizi ni adui wa nafsi yake mwenyewe; huapishwa lakini hathubutu kushuhudia.
25 El temor al hombre coloca una trampa, Pero el que confía en Yavé estará seguro.
Kuwaogopa watu huwa ni mtego, bali yeyote amtumainiaye Bwana atakuwa salama.
26 Muchos buscan el favor del gobernante, Pero la sentencia para el hombre viene de Yavé.
Wengi hutafuta kusikilizwa na mtawala, bali mtu hupata haki kutoka kwa Bwana.
27 El hombre inicuo es aborrecido por los justos, Y el de camino recto es aborrecido por los perversos.
Mwenye haki huwachukia sana wasio waaminifu; waovu huwachukia sana wenye haki.