< Proverbios 20 >
1 El vino es burlador y alborotador el licor, Y cualquiera que en ello se desvía no es sabio.
Divai ni dhihaka na kinywaji kikali ni mgomvi; anayepotea kwa kunywa hana busara.
2 Como rugido de león es la ira del rey, El que provoca su ira expone su propia vida.
Kumwogopa mfalme ni kama kumwogopa simba kijana aungurumaye, yeyote anayemkasirisha hutoa fidia ya maish yake.
3 Honra del hombre es evitar la contienda, Pero todo insensato se envolverá en ella.
Ni heshima kwa mtu yeyote kujiepusha na mafarakano, bali kila mpumbavu hurukia kwenye mabishano.
4 En otoño no ara el holgazán, Rebuscará en la cosecha y nada hallará.
Mtu mvivu halimi majira ya kipupwe; hutafuta mazao wakati wa mavuno lakini hapati kitu.
5 Como agua profunda es el propósito en el corazón del hombre, Pero el hombre entendido logrará extraerlo.
Makusudi ndani ya moyo wa mtu ni kama maji yenye kina, bali mtu mwenye ufahamu huyateka.
6 Muchos hombres proclaman su propia bondad, Pero un hombre fiel, ¿quién lo hallará?
Mara nyingi mtu husema yeye ni mwaminifu, lakini ni nani awezaye kumpata yule mwaminifu?
7 El justo camina en su integridad, Después de él, sus hijos son muy dichosos.
Mtu atendaye haki hutembea katika uaminifu wake na wana wake wanaofuata baada yake wanafuraha.
8 Un rey sentado en el tribunal, Con su mirada disipa toda maldad.
Mfalme anayeketi kwenye kiti cha hukumu akifanya kazi za kuhukumu hupembua kwa macho yake mabaya yote yaliyoko mbele yake.
9 ¿Quién podrá decir: Tengo mi conciencia limpia, Estoy purificado de mi pecado?
Nani anayeweza kusema, “Nimeuweka safi moyo wangu; nipo huru na dhambi zangu”?
10 Pesa falsa y medida falsa, Ambas son repugnancia a Yavé.
Mizani tofauti na vipimo visivyosawa - Yehova huvichukia vyote.
11 Aun el muchacho es conocido por sus hechos, Si su conducta es limpia y recta.
Hata kijana hujulikana kwa matendo yake, kwa mwenendo wake kama ni safi na uadilifu.
12 El oído que oye y el ojo que ve, Ambas cosas las hizo Yavé.
Masikio yanayosikia na macho yanayoona- Yehova aliyafanya yote.
13 No ames el sueño No sea que te empobrezcas. Abre tus ojos y te saciarás de pan.
Usipende usingizi au utakuwa masikini; fumbua macho yako na utakuwa na vyakula tele.
14 Es malo, es malo, dice el comprador, Pero cuando se va, se jacta.
“Mbaya! Mbaya!” anasema mnunuzi, lakini akiondoka anajisifu.
15 Existe el oro y multitud de piedras preciosas, Pero los labios sabios son algo más precioso.
Ipo dhahabu na mawe ya thamani, lakini midomo yenye maarifa ni kito cha thamani.
16 Tómale la ropa al que salió fiador de un extraño, Y tómale prenda cuando da garantía a los forasteros.
Chukua vazi kama mmiliki wake ataweka fedha kama dhamana kwa deni la mgeni, na lichukue kama anaweka dhamana kwa uzinifu.
17 Sabroso es al hombre el pan mal adquirido, Pero después su boca estará llena de fragmentos de piedra.
Mkate uliopatikana kwa ulaghai unaladha tamu, lakini baadaye kinywa chake kitajaa kokoto.
18 Confirma los planes por medio del consejo, Y con sabias estrategias haz la guerra.
Mipango huimarishwa kwa ushauri na kwa mwongozo wa busara utapigana vita.
19 El que revela secretos levanta calumnia, Por tanto, no te metas con un chismoso.
Mmbea hufunua siri na kwa hiyo hupaswi kushirikiana na watu ambao huongea sana.
20 Al que insulte a su padre o a su madre, Se le apagará su lámpara en medio de la oscuridad.
Kama mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itapulizwa katikati ya giza.
21 Herencia adquirida con robo al comienzo, Al fin no será bendita.
Urithi uliopatikana mwanzoni kwa haraka utakuwa na mema kidogo mwishoni.
22 No digas: Yo me vengaré. Espera a Yavé, y Él te salvará.
Usiseme “Mimi nitakulipiza kwa kosa hili” Msubiri Yehova na yeye atakuokoa.
23 Las pesas desiguales son repugnancia a Yavé, Y una balanza con trampa no es buena.
Yehova huchukia mizani isiyo sawa na vipimo vya udanganyifu si vizuri.
24 De Yavé son los pasos del hombre, ¿Cómo, pues, podrá el hombre entender su camino?
Hatua za mtu huongozwa na Yehova; namna gani basi ataifahamu njia yake?
25 Trampa es al hombre el voto apresurado, Y después de hacerlo, reflexionar.
Ni mtego kwa mtu kusema kwa pupa, “Kitu hiki ni kitakatifu” na kuanza kufikiri juu yake kwamba kina maana gani baada ya kufanya kiapo.
26 El rey sabio dispersa a los perversos, Y hace pasar sobre ellos la rueda de trillar.
Mfalme mwenye busara huwapepeta waovu na huligeuza juu yao gurudumu la kupuria.
27 Lámpara de Yavé es el espíritu del hombre, Que escudriña lo más recóndito del ser.
Roho ya mtu ni taa ya Yehova, hutafiti sehemu zake zote za ndani kabisa.
28 Misericordia y verdad preservan al rey, Y la clemencia sustenta su trono.
Agano la uaminifu na udhamini humhifadhi mfalme; kiti chake cha enzi hufanywa thabiti kwa upendo.
29 La gloria de los jóvenes es su fortaleza, Y el esplendor de los ancianos, sus canas.
Utukufu wa watu vijana ni nguvu zao na fahari ya watu wazee ni mvi zao.
30 Las marcas de los azotes purifican del mal, Y los golpes llegan a lo íntimo del corazón.
Mapigo yanayoleta kidonda huusafisha ubaya na vichapo hufanya sehemu za ndani kabisa kuwa safi.