< Proverbios 20 >

1 El vino es burlador y alborotador el licor, Y cualquiera que en ello se desvía no es sabio.
Mvinyo ni mdhihaki na kileo ni mgomvi; yeyote apotoshwaye navyo hana hekima.
2 Como rugido de león es la ira del rey, El que provoca su ira expone su propia vida.
Ghadhabu ya mfalme ni kama ngurumo ya simba; yeye amkasirishaye hupoteza uhai wake.
3 Honra del hombre es evitar la contienda, Pero todo insensato se envolverá en ella.
Ni kwa heshima ya mtu kujitenga ugomvi, bali kila mpumbavu ni mwepesi kugombana.
4 En otoño no ara el holgazán, Rebuscará en la cosecha y nada hallará.
Mvivu halimi kwa majira; kwa hiyo wakati wa mavuno hutazama lakini hapati chochote.
5 Como agua profunda es el propósito en el corazón del hombre, Pero el hombre entendido logrará extraerlo.
Makusudi ya moyo wa mwanadamu ni maji yenye kina, lakini mtu mwenye ufahamu huyachota.
6 Muchos hombres proclaman su propia bondad, Pero un hombre fiel, ¿quién lo hallará?
Watu wengi hujidai kuwa na upendo usiokoma, bali mtu mwaminifu ni nani awezaye kumpata?
7 El justo camina en su integridad, Después de él, sus hijos son muy dichosos.
Mtu mwenye haki huishi maisha yasiyo na lawama, wamebarikiwa watoto wake baada yake.
8 Un rey sentado en el tribunal, Con su mirada disipa toda maldad.
Wakati mfalme aketipo katika kiti chake cha enzi kuhukumu, hupepeta ubaya wote kwa macho yake.
9 ¿Quién podrá decir: Tengo mi conciencia limpia, Estoy purificado de mi pecado?
Ni nani awezaye kusema, “Nimeuweka moyo wangu safi; mimi ni safi na sina dhambi?”
10 Pesa falsa y medida falsa, Ambas son repugnancia a Yavé.
Mawe ya kupimia yaliyo tofauti na vipimo tofauti, Bwana huchukia vyote viwili.
11 Aun el muchacho es conocido por sus hechos, Si su conducta es limpia y recta.
Hata mtoto hujulikana kwa matendo yake, kama tabia yake ni safi na adili.
12 El oído que oye y el ojo que ve, Ambas cosas las hizo Yavé.
Masikio yasikiayo na macho yaonayo, Bwana ndiye alivifanya vyote viwili.
13 No ames el sueño No sea que te empobrezcas. Abre tus ojos y te saciarás de pan.
Usiupende usingizi la sivyo utakuwa maskini, uwe macho nawe utakuwa na chakula cha akiba.
14 Es malo, es malo, dice el comprador, Pero cuando se va, se jacta.
“Haifai, haifai!” asema mnunuzi, kisha huondoka akijisifia ununuzi wake.
15 Existe el oro y multitud de piedras preciosas, Pero los labios sabios son algo más precioso.
Dhahabu kunayo, na marijani kwa wingi, lakini midomo inenayo maarifa ni kito cha thamani kilicho adimu.
16 Tómale la ropa al que salió fiador de un extraño, Y tómale prenda cuando da garantía a los forasteros.
Chukua vazi la yule awekaye dhamana kwa ajili ya mgeni; lishikilie iwe dhamana kama anafanya hivyo kwa ajili ya mwanamke mpotovu.
17 Sabroso es al hombre el pan mal adquirido, Pero después su boca estará llena de fragmentos de piedra.
Chakula kilichopatikana kwa hila ni kitamu kwa mwanadamu, bali huishia na kinywa kilichojaa changarawe.
18 Confirma los planes por medio del consejo, Y con sabias estrategias haz la guerra.
Fanya mipango kwa kutafuta mashauri, ukipigana vita, tafuta maelekezo.
19 El que revela secretos levanta calumnia, Por tanto, no te metas con un chismoso.
Maneno ya kusengenya husababisha kutokuaminika, kwa hiyo mwepuke mtu anayezungumza kupita kiasi.
20 Al que insulte a su padre o a su madre, Se le apagará su lámpara en medio de la oscuridad.
Ikiwa mtu atamlaani baba yake au mama yake, taa yake itazimwa katika giza nene.
21 Herencia adquirida con robo al comienzo, Al fin no será bendita.
Urithi upatikanao haraka mwanzoni, hautabarikiwa mwishoni.
22 No digas: Yo me vengaré. Espera a Yavé, y Él te salvará.
Usiseme, “Nitakulipiza kwa ajili ya kosa hili!” Mngojee Bwana, naye atakuokoa.
23 Las pesas desiguales son repugnancia a Yavé, Y una balanza con trampa no es buena.
Bwana anachukia sana mawe ya kupimia ya udanganyifu, nazo mizani zisizo halali hazimpendezi.
24 De Yavé son los pasos del hombre, ¿Cómo, pues, podrá el hombre entender su camino?
Hatua za mtu huongozwa na Bwana. Anawezaje basi mtu yeyote kuelewa njia yake mwenyewe?
25 Trampa es al hombre el voto apresurado, Y después de hacerlo, reflexionar.
Ni mtego kwa mtu kuweka wakfu kitu kwa haraka na baada ya kitambo kidogo kufikiria tena nadhiri zake.
26 El rey sabio dispersa a los perversos, Y hace pasar sobre ellos la rueda de trillar.
Mfalme mwenye hekima hupepeta waovu, hulipitisha gurudumu la kupuria juu yao.
27 Lámpara de Yavé es el espíritu del hombre, Que escudriña lo más recóndito del ser.
Taa ya Bwana huchunguza roho ya mwanadamu, huchunguza utu wake wa ndani.
28 Misericordia y verdad preservan al rey, Y la clemencia sustenta su trono.
Upendo na uaminifu humweka mfalme salama, kwa njia ya upendo, kiti chake cha enzi huwa salama.
29 La gloria de los jóvenes es su fortaleza, Y el esplendor de los ancianos, sus canas.
Utukufu wa vijana ni nguvu zao, mvi ni fahari ya uzee.
30 Las marcas de los azotes purifican del mal, Y los golpes llegan a lo íntimo del corazón.
Mapigo na majeraha huusafisha ubaya, nayo michapo hutakasa utu wa ndani.

< Proverbios 20 >