< Proverbios 10 >
1 Proverbios de Salomón. El hijo sabio alegra al padre, Pero el hijo necio es tristeza de su madre.
Mithali za Sulemani. Mwana mwenye hekima humfurahisha baba yake lakini mwana mpumbavu huleta majonzi kwa mama yake.
2 Los tesoros de perversidad no son de provecho, Pero la justicia libra de la muerte.
Hazina zilizolimbikizwa kwa uovu hakosa thamani, bali kwa kutenda haki hujilinda mbali na kifo.
3 Yavé no deja padecer hambre al justo, Pero impide que se sacie el apetito de los perversos.
Yehova hawaachi wale watendao haki wapate njaa, bali hamu ya waovu huizuia.
4 La mano negligente empobrece, Pero la mano de los diligentes enriquece.
Mkono mlegevu humfanya mtu awe masikini, bali mkono wa mtu mwenye bidii hupata utajiri.
5 El que recoge en verano es hijo sensato, Pero el que duerme en la cosecha es un hijo que avergüenza.
Mwana mwenye busara hukusanya mazao wakati wa kiangazi, bali ni aibu kwake alalaye wakati wa mavuno.
6 Hay bendiciones sobre la cabeza del justo, Pero la boca de los perversos oculta violencia.
Zawadi kutoka kwa Mungu zipo juu ya kichwa cha wale watendao haki; bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
7 La memoria del justo será bendita, Pero el nombre del perverso se pudrirá.
Mtu atendaye haki anatufurahisha tunapomkumbuka, bali jina la mwovu litaoza.
8 El sabio de corazón acepta los mandamientos, Pero el insensato charlatán se hunde.
Wale wenye akili hukubali maagiza, bali mpumbavu mwenye maneno mengi ataangamia.
9 El que camina en integridad anda confiado, Pero el que pervierte sus caminos será puesto en descubierto.
Yeye anayetembea katika uadilifu hutembea katika usalama, bali yule anayepotosha njia zake, ataonekana.
10 El que guiña el ojo causa tristeza, Pero el que reprende francamente hace la paz.
Yeye ambaye hukonyeza kwa jicho lake huleta majonzi, bali mpumbavu mwenye maneno mengi atatupwa chini.
11 La boca del justo es manantial de vida, Pero la boca del necio oculta violencia.
Kinywa cha mwenye kutenda haki ni kama chemchemi ya maji ya uzima, bali kinywa cha uovu hufunikwa kwa jeuri.
12 El odio provoca rencillas, Pero el amor cubre todas las faltas.
Chuki huchochea mafarakano, bali upendo hufunika juu ya makwazo yote.
13 La sabiduría está en los labios del entendido, Pero la vara es para la espalda del que carece de entendimiento.
Hekima inapatikana kwenye kinywa cha mtu mwenye ufahamu, bali fimbo ni kwa ajili ya mgongo wa yule asiye na akili.
14 Los sabios atesoran conocimiento, Pero la boca del necio es ruina cercana.
Watu wenye hekima hutunza maarifa, bali kinywa cha mpumbavu huleta uharibifu karibu.
15 La fortuna del rico es su fortaleza, La ruina de los necesitados es su pobreza.
Mali ya mtu tajiri ni mji wake mwenye ngome; ufukara wa masikini ni uharibifu wao.
16 El salario del justo es para vida, El lucro del perverso, para pecado.
Mshahara wa watenda haki huelekea kwenye uzima; manufaa ya waovu huelekea dhambini.
17 El que acepta la instrucción está en senda de vida, Pero el que desecha la reprensión se extravía.
Kuna njia kwenda kwenye uzima kwa yule anayefuata maongozo, bali anayekataa maonyo hupotea.
18 Los labios rectos aplacan el odio, Pero el que esparce calumnia es un necio.
Yeye afichaye chuki anamidomo ya uongo, na yeye anayesambaza kashfa ni mpumbavu.
19 En las muchas palabras no falta pecado, Pero el que refrena sus labios es prudente.
Katika maneno mengi, hapakosi uhalifu, bali aliyemwangalifu katika usemi wake ni mwenye busara.
20 La boca del justo es plata pura, Pero el corazón del perverso es nada.
Ulimi wa yule atendaye haki ni fedha safi; kuna thamani ndogo katika moyo wa mbaya.
21 Los labios del justo nutren a muchos, Pero los necios mueren por falta de entendimiento.
Midomo ya yule atendaye haki huwastawisha wengi, bali wapumbavu hufa kwa sababu ya kukosa akili.
22 La bendición de Yavé es la que enriquece, Y Él no le añade tristeza.
Zawadi njema za Yehova huleta utajiri na haweki maumivu ndani yake.
23 La perversidad es como deporte para el necio. Así es la sabiduría para el hombre de entendimiento.
Uovu ni mchezo achezao mpumbavu, bali hekima ni furaha kwa mtu mwenye ufahamu.
24 Lo que teme el perverso, eso le vendrá, Pero el deseo de los justos les será concedido.
Hofu ya mwenye uovu humkumba ghafla, bali shauku ya mwenye haki itatimizwa.
25 Cuando pasa el remolino de viento, desaparece el perverso, Pero el justo tiene fundamento eterno.
Waovu ni kama dhoruba inayopita, na hawapo tena, bali mwenye haki ni msingi unaodumu milele.
26 Como vinagre a los dientes y humo a los ojos, Así es el perezoso para quienes lo comisionan.
Kama siki kwenye meno na moshi kwenye macho, ndivyo alivyo mvivu kwa wale waliomtuma.
27 El temor a Yavé aumenta los días, Pero los años de los perversos serán acortados.
Hofu ya Yehova huongeza maisha, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
28 La esperanza de los justos es alegría, Pero la esperanza de los perversos perecerá.
Matumaini ya wale watendao haki ndiyo furaha yao, bali miaka ya waovu itakuwa mifupi.
29 El camino de Yavé es fortaleza para el íntegro, Pero ruina para los malhechores.
Njia ya Yehova huwalinda wale wenye uadilifu, bali kwa waovu ni uhalibifu.
30 El justo no será sacudido jamás, Pero los perversos no habitarán la tierra.
Wale watendao haki hawataondolewa, bali waovu hawatabaki katika nchi.
31 La boca del justo destila sabiduría, Pero la lengua perversa será cortada.
Katika kinywa cha wale watendao haki hutoka tunda la hekima, bali ulimi wa kupotosha utakatwa.
32 Los labios del justo destilan lo aceptable, Pero la boca de los perversos lo que es pervertido.
Midomo ya wale watendao mema huyajua yanayokubalika, bali kinywa cha waovu, huyajua yanayopotosha.