< Números 33 >
1 Estas son las jornadas de los hijos de Israel cuando salieron de la tierra de Egipto en escuadrones, bajo el mando de Moisés y Aarón.
Hivi ndivyo vituo katika safari ya Waisraeli walipotoka Misri kwa vikosi chini ya uongozi wa Mose na Aroni.
2 Por mandato de Yavé, Moisés escribió los puntos de salida según sus jornadas. Estas son sus jornadas conforme a sus puntos de partida:
Kwa agizo la Bwana, Mose aliweka kumbukumbu ya vituo katika safari yao. Hivi ndivyo vituo katika safari yao:
3 Salieron de Rameses el día 15 del mes primero, la mañana siguiente de la Pascua. Los hijos de Israel salieron con mano poderosa a la vista de todos los egipcios,
Waisraeli walisafiri kutoka Ramesesi katika siku ya kumi na tano ya mwezi wa kwanza, siku iliyofuata Pasaka. Walitembea kwa ujasiri wazi mbele ya Wamisri wote,
4 mientras éstos enterraban a todos sus primogénitos, a los que Yavé hirió de muerte. También Yavé ejecutó actos justicieros contra sus ʼelohim.
waliokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza wote, ambao Bwana alikuwa amewaua katikati yao, kwa kuwa Bwana alikuwa ameleta hukumu juu ya miungu yao.
5 Los hijos de Israel salieron de Rameses y acamparon en Sucot.
Waisraeli waliondoka Ramesesi na kupiga kambi huko Sukothi.
6 Salieron de Sucot y acamparon en Etam, que está al borde del desierto.
Wakaondoka Sukothi na kupiga kambi huko Ethamu, pembeni mwa jangwa.
7 Salieron de Etam y se volvieron hacia Pi-hahirot, que está delante de Baalzefón, y acamparon frente a Migdol.
Wakaondoka Ethamu, wakageuka wakarudi Pi-Hahirothi, hadi mashariki ya Baal-Sefoni, wakapiga kambi yao karibu na Migdoli.
8 Salieron de Pi-hahirot y pasaron por medio del mar hacia el desierto. Anduvieron tres jornadas por el desierto de Etam, y acamparon en Mara.
Wakaondoka Pi-Hahirothi wakapita katikati ya bahari mpaka jangwani, na baada ya kusafiri kwa siku tatu katika Jangwa la Ethamu, walipiga kambi huko Mara.
9 Salieron de Mara y llegaron a Elim, donde había 12 fuentes de agua y 70 palmeras. Allí acamparon.
Wakaondoka Mara wakaenda Elimu, mahali ambapo palikuwa na chemchemi kumi na mbili na mitende sabini, huko wakapiga kambi.
10 Salieron de Elim y acamparon junto al mar Rojo.
Wakaondoka Elimu na kupiga kambi kando ya Bahari ya Shamu.
11 Salieron del mar Rojo y acamparon en el desierto de Sin.
Wakaondoka kando ya Bahari ya Shamu na kupiga kambi katika Jangwa la Sini.
12 Salieron del desierto de Sin y acamparon en Dofca.
Wakaondoka katika Jangwa la Sini, wakapiga kambi huko Dofka.
13 Salieron de Dofca y acamparon en Alús.
Wakaondoka Dofka, wakapiga kambi huko Alushi.
14 Salieron de Alús y acamparon en Refidim, donde no había agua para que el pueblo bebiera.
Wakaondoka Alushi, wakapiga kambi Refidimu, mahali ambapo hapakuwa na maji kwa ajili ya watu kunywa.
15 Salieron de Refidim y acamparon en el desierto de Sinaí.
Wakaondoka Refidimu na kupiga kambi katika Jangwa la Sinai.
16 Luego salieron del desierto de Sinaí y acamparon en Kibrot-hatava.
Wakaondoka katika Jangwa la Sinai na kupiga kambi huko Kibroth-Hataava.
17 Salieron de Kibrot-hatava y acamparon en Haserot.
Wakaondoka Kibroth-Hataava na kupiga kambi huko Haserothi.
18 Salieron de Haserot y acamparon en Ritma.
Wakaondoka Haserothi na kupiga kambi huko Rithma.
19 Salieron de Ritma y acamparon en Rimón-peres.
Wakaondoka Rithma na kupiga kambi huko Rimon-Peresi.
20 Salieron de Rimón-peres y acamparon en Libna.
Wakaondoka Rimon-Peresi na kupiga kambi huko Libna.
21 Salieron de Libna y acamparon en Rissa.
Wakaondoka Libna na kupiga kambi huko Risa.
22 Salieron de Rissa y acamparon en Ceelata.
Wakaondoka Risa na kupiga kambi huko Kehelatha.
23 Salieron de Ceelata y acamparon en la montaña Sefer.
Wakaondoka Kehelatha na kupiga kambi kwenye mlima Sheferi.
24 Salieron de la montaña Sefer y acamparon en Harada.
Wakaondoka kwenye mlima Sheferi na kupiga kambi huko Harada.
25 Salieron de Harada y acamparon en Macelot.
Wakaondoka Harada na kupiga kambi huko Makelothi.
26 Salieron de Macelot y acamparon en Tahat.
Wakaondoka Makelothi na kupiga kambi huko Tahathi.
27 Salieron de Tahat y acamparon en Tara.
Wakaondoka Tahathi na kupiga kambi huko Tera.
28 Salieron de Tara y acamparon en Mitca.
Wakaondoka Tera na kupiga kambi huko Mithka.
29 Salieron de Mitca y acamparon en Hasmona.
Wakaondoka Mithka na kupiga kambi huko Hashmona.
30 Salieron de Hasmona y acamparon en Moserot.
Wakaondoka Hashmona na kupiga kambi Moserothi.
31 Salieron de Moserot y acamparon en Beney-jaacán.
Wakaondoka Moserothi na kupiga kambi huko Bene-Yakani.
32 Salieron de Beney-jaacán y acamparon en la montaña Gidgad.
Wakaondoka Bene-Yakani na kupiga kambi huko Hor-Hagidgadi.
33 Salieron de la montaña Gidgad y acamparon en Jotbata.
Wakaondoka Hor-Hagidgadi na kupiga kambi huko Yotbatha.
34 Salieron de Jotbata y acamparon en Abrona.
Wakaondoka Yotbatha na kupiga kambi huko Abrona.
35 Salieron de Abrona y acamparon en Ezión-geber.
Wakaondoka Abrona na kupiga kambi huko Esion-Geberi.
36 Salieron de Ezión-geber y acamparon en el desierto de Sin, que es Cades.
Wakaondoka Esion-Geberi na kupiga kambi huko Kadeshi katika Jangwa la Sini.
37 Salieron de Cades y acamparon en la montaña Hor, en la frontera de la tierra de Edom.
Wakaondoka Kadeshi na kupiga kambi kwenye Mlima Hori, mpakani mwa Edomu.
38 Por la Palabra de Yavé, el sacerdote Aarón subió a la montaña Hor. Allí murió, a los 40 años de la salida de los hijos de Israel de la tierra de Egipto, el mes quinto, el día primero del mes.
Kwa amri ya Bwana, kuhani Aroni alipanda Mlima Hori, mahali alipofia katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano, mwaka wa arobaini baada ya Waisraeli kutoka Misri.
39 Aarón tenía 123 años cuando murió en la montaña Hor.
Aroni alikufa juu ya Mlima Hori akiwa na umri wa miaka 123.
40 Entonces, el rey de Arad, cananeo, que habitaba en el Neguev, en la tierra de Canaán, oyó acerca de la llegada de los hijos de Israel.
Mfalme Mkanaani wa Aradi, ambaye aliishi huko Negebu ya Kanaani, akasikia kwamba Waisraeli wanakuja.
41 Salieron de la montaña Hor y acamparon en Zalmona.
Wakaondoka kwenye mlima Hori na kupiga kambi huko Salmona.
42 Salieron de Zalmona y acamparon en Funón.
Wakaondoka Salmona, wakapiga kambi huko Punoni.
43 Salieron de Funón y acamparon en Obot.
Wakaondoka Punoni, wakapiga kambi huko Obothi.
44 Salieron de Obot y acamparon en Ije-abarim, en la frontera de Moab.
Wakaondoka Obothi, wakapiga kambi huko Iye-Abarimu, mipakani mwa Moabu.
45 Salieron de Ije-abarim y acamparon en Dibóngad.
Wakaondoka Iye-Abarimu, wakapiga kambi huko Dibon-Gadi.
46 Salieron de Dibóngad y acamparon en Almóndiblataim.
Wakaondoka Dibon-Gadi na kupiga kambi huko Almon-Diblathaimu.
47 Salieron de Almóndiblataim y acamparon en las montañas de Abarim, delante de la montaña Nebo.
Wakaondoka Almon-Diblathaimu na kupiga kambi katika milima ya Abarimu, karibu na Nebo.
48 Salieron de las montañas de Abarim y acamparon frente a Jericó en las llanuras de Moab, junto al Jordán.
Wakaondoka kwenye milima ya Abarimu na kupiga kambi kwenye tambarare ya Moabu, kando ya Yordani ngʼambo ya Yeriko.
49 Finalmente, acamparon junto al Jordán, desde Betjesimot hasta Abel-Sitim, en las llanuras de Moab.
Huko kwenye tambarare za Moabu walipiga kambi kandokando ya Mto Yordani, kuanzia Beth-Yeshimothi mpaka Abel-Shitimu.
50 Yavé habló a Moisés frente a Jericó en las llanuras de Moab, junto al Jordán:
Katika tambarare za Moabu kando ya Yordani kuvukia Yeriko, Bwana akamwambia Mose,
51 Habla a los hijos de Israel: Cuando crucen el Jordán hacia la tierra de Canaán,
“Sema na Waisraeli uwaambie: ‘Mtakapovuka Mto Yordani kuingia Kanaani,
52 echarán a todos los habitantes de la tierra de delante de ustedes. Destruirán todas sus esculturas y todas sus imágenes de fundición, y destruirán todos sus lugares altos.
wafukuzeni wakazi wote wa nchi iliyo mbele yenu. Haribuni sanamu zao zote za kuchongwa, na sanamu zilizotengenezwa kwa kuyeyusha chuma, na kupabomoa mahali pao pa ibada.
53 Tomarán posesión de la tierra y vivirán en ella, porque Yo les di esa tierra para que la posean.
Mtaimiliki nchi hiyo na kukaa huko, kwa kuwa nimewapeni ninyi kuimiliki.
54 Heredarán la tierra por sorteo según sus familias. Al grande aumentarán su posesión, y al pequeño se la disminuirán. Aquello que le caiga en suerte a cada uno será suyo. Tomarán posesión según las tribus de sus antepasados.
Mtaigawanya nchi hiyo kwa kupiga kura, kufuatana na koo zenu. Kwa kundi kubwa zaidi toa urithi mkubwa zaidi, na kwa kundi dogo zaidi urithi mdogo zaidi. Chochote kinachowaangukia kwa kura kitakuwa chao. Mtaigawanya nchi kufuatana na makabila ya babu zenu.
55 Pero si no echan de delante de ustedes a los habitantes de la tierra, sucederá que los que queden de ellos serán como aguijones en sus ojos y como espinas en sus costados. Los acosarán en la tierra donde vivan.
“‘Lakini kama hamkuwafukuza wenyeji wakaao katika nchi hiyo, wale mtakaowaruhusu wabaki watakuwa kama sindano kwenye macho yenu na miiba kwenu kila upande. Watawasumbua katika nchi mtakayoishi.
56 Como Yo planeo hacerles a ellos, así les haré a ustedes.
Kisha nitawatenda ninyi kile ambacho nimepanga kuwatenda wao.’”