< Números 29 >
1 En el séptimo mes, el día primero del mes, tendrán santa convocación. No harán obra servil. Les será día de tocar las trompetas.
Katika siku ya kwanza, ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Katika siku hiyo hamtafanya kazi zenu za kila siku. Itakuwa siku ya kupiga matarumbeta.
2 Ofrecerán un holocausto de olor que apacigua a Yavé: un becerro de la manada vacuna, un carnero, siete corderos añales sin defecto,
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ya kufanya harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa sadaka ya fahari mchanga, kondoo dume mmoja na wanakondoo dume saba wa mwaka mmoja, kila mmoja mkamilifu.
3 con su ofrenda vegetal de flor de harina amasada con aceite, 6,6 litros por cada becerro, 4,4 litros por el carnero,
Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya huyo fahari, sehemu mbili za kumi kwa ajili ya huyo kondoo mume,
4 2,2 litros por cada uno de los siete corderos
na sehemu ya kumi ya kila hao wanakondoo waume saba.
5 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado para hacer sacrificio que apacigua a favor de ustedes.
Na mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi ili kufanya upatanisho kwa ajili yenu.
6 Además ofrecerán el holocausto de la nueva luna y su ofrenda vegetal, y el holocausto continuo y su ofrenda vegetal con sus libaciones, según su ordenanza, como sacrificio quemado de olor que apacigua a Yavé.
Toeni hizo sadaka katika mwezi wa saba kama nyongeza ya sadaka mtakazotoa kila mwanzo wa kila mwezi: pamoja na sadaka maalumu za kuteketezwa na sadaka za unga. Hizi zitakuwa nyongeza za sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji. Utakapokuwa ukiendelea na sadaka hizi, utakuwa ukitii kile kilichoamriwa kutoa harufu nzuri, sadaka iliyotengenezwa kwa moto kwa BWANA.
7 El día décimo de este mes séptimo tendrán una santa convocación y se humillarán. No harán obra.
Siku ya kumi ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu la kumwabudu BWANA. Mtajinyeneyekeza na hamtafanya kazi.
8 Ofrecerán en holocausto de olor que apacigua a Yavé un becerro de la manada vacuna, un carnero y siete corderos añales sin defecto.
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja mchanga ili kutoa harufu nzuri, kondoo mmoja mume, na wanakondoo saba waume wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
9 Su ofrenda vegetal será de 6,6 litros de flor de harina amasada con aceite por cada becerro, 4,4 litros por el carnero
Pamoja na sadaka hizo utatoa sadaka ya unga, unga mwembamba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa ajili ya fahari, sehemu mbili za kumi za kondoo dume mmoja,
10 y 2,2 litros por cada uno de los siete corderos.
na sehemu ya kumi ya efa moja kwa kila mwanakondoo wale saba.
11 También ofrecerán un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del sacrificio de olor que apacigua por el pecado y del holocausto continuo, de su ofrenda vegetal y sus libaciones.
Mtatatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya upatanisho. Hii itakuwa sadaka ya nyongeza ya upatanisho, ya sadaka ya kila siku ya kuteketezwa, pamoja na sadaka za unga, na sadaka zake za vinywaji.
12 El día 15 del mes séptimo tendrán una santa convocación. No harán obra servil. Celebrarán la fiesta solemne a Yavé durante siete días.
Siku ya kumi na tano ya mwezi wa saba, mtakuwa na kusanyiko takatifu lakumwabudu BWANA. Siku hiyo hamtafanya kazi za kila siku, na mtazitunza hizo sikukuu kwa muda wa siku saba kwa ajili ya BWANA.
13 Ofrecerán como holocausto, sacrificio quemado de olor que apacigua a Yavé, 13 becerros de la manada vacuna, dos carneros y 14 corderos añales. Serán sin defecto.
Mtatoa sadaka ya kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ilikutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa mafahari wachanga kumi na tatu, kondoo waume wawili, na wanakondoo waume kumi na nne wa mwaka mmoja. Wote wakamilifu.
14 Su ofrenda vegetal será de flor de harina amasada con aceite, 6,6 litros por cada uno de los 13 becerros, 4,4 litros por cada uno de los dos carneros
Pamoja na hao mtatoa sadaka ya unga, unga mwembaba uliochanganywa na mafuta, sehemu tatu za kumi za efa kwa kila fahari katika hao kumi na tatu, sehemu mbili za kumi kwa kila hao kondoo dume wawili,
15 y 2,2 litros por cada uno de los 14 corderos.
na sehemu ya kumi ya efa ya hao wanakondoo kumi na nne.
16 Ofrecerán un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo con su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi katika nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa, sadaka yake ya unga, pamoja na sadaka za vinywaji.
17 El segundo día, 12 becerros de la manada vacuna, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya pili ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi na mbili, kondoo dume wawili na wanakondoo dume kumi na mbili wa umri wa mwaka mmoja, wote wakamilifu.
18 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja nao mtatoa sadaka ya unga, na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na kwa ajili ya wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilvyoamriwa.
19 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kila siku, sadaka yake ya unga, na sadaka zake za vinywaji.
20 El tercer día, 11 becerros, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya tatu ya kusanyiko, mtatoa sadaka mafahari kumi na moja, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
21 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja na hizo sadaka mtatoa sadaka ya unga na sdaka ya vinywaji kwa wale mafahari, kwa wale kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, utoe sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
22 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, con su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa sadaka beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya zile sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
23 El cuarto día, diez becerros, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya nne ya kusanyiko, mtatoa mafahari kumi, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
24 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sdaka za vinywaji kwa wale mafahari, na kwa wale kondoo dume na kwa wale wanakodoo, mtatoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
25 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kuwa nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji
26 El quinto día, nueve becerros, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya tano ya kusanyiko, mtatoa mafahari tisa, kondoo dume wawili, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
27 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, kondoo dume, na wale wanakondoo, mkitoa sdaka nyingi kama ilivyoamriwa.
28 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kuteketezwa za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka za vinywaji.
29 El sexto día, ocho becerros, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya sita ya kusanyiko, mtatoa mafahari wanane, kondoo dume wawili, na wanakondoo kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
30 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja na sadaka hizo mtatoa sadaka za unga nasadaka za vinywaji kwa wale mafahari, kondoo wa dume na wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
31 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, su ofrenda vegetal y sus libaciones.
Mtatoa beberu kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku za kuteketezwa, sadaka zadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
32 El séptimo día, siete becerros, dos carneros, 14 corderos añales sin defecto,
Siku ya saba ya kusanyiko, mtatoa mafahari saba, kondoo dume saba, na wanakondoo dume kumi na nne wa mwaka mmoja, wakamilifu.
33 con su ofrenda vegetal y sus libaciones para los becerros, los carneros y los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Pamoja nao mtataengeneza sadaka ya unga na sadaka ya vinywaji kwa ajili ya wale mafahari, na kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkitoa sadaka nyingi kama ilivyoamriwa.
34 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, con su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka ya kuteketezwa ya kila siku, na sadaka yake ya unga, na sadaka yake ya vinywaji.
35 El octavo día tendrán una asamblea solemne. No harán obra servil.
Siku ya nane mtakuwa na kusanyiko lingine makini. Hamtafanya kazi zenu za kila siku.
36 Ofrecerán en holocausto, en sacrificio quemado de olor que apacigua a Yavé, un becerro, un carnero, siete corderos añales sin defecto,
Mtafanya sadaka za kuteketezwa, sadaka iliyotengenezwa kwa moto ili kutoa harufu nzuri kwa BWANA. Mtatoa fahari mmoja, kondoo mmoja dume, na wanakondoo saba dume wa umri wa mwaka mmoja, wakamilifu.
37 y su ofrenda vegetal y sus libaciones con el becerro, con el carnero y con los corderos, según el número de ellos, conforme a la ordenanza,
Mtatoa sadaka zake za unga na sadaka zake za vinywaji kwa ajili ya yule fahari, kondoo dume, na kwa wale wanakondoo, mkifanya sadaka nyingi kadri ilivyoamriwa.
38 y un macho cabrío como sacrificio por el pecado, además del holocausto continuo, con su ofrenda vegetal y su libación.
Mtatoa beberu mmoja kuwa sadaka ya dhambi kama nyongeza ya sadaka za kila siku, na sadaka zake za unga, na sadaka zake za vinywaji.
39 Estas cosas ofrecerán a Yavé en sus fiestas solemnes, aparte de sus votos y de sus ofrendas voluntarias, con sus holocaustos, sus ofrendas vegetales, sus libaciones y sus ofrendas de paz.
Hivi ndivyo utakavyotoa sadaka kwa BWANA katika sikukuu zenu za kila mwaka. Hivi vitakuwa nyongeza ya viapo vyenu na sadaka zenu za hiari. Mtavitoa hivi kama sadaka zenu za kuteketezwa, sadaka za unga, sadaka za vinywaji, na sadaka za amani.”
40 Y Moisés habló a los hijos de Israel conforme a todo lo que Yavé le ordenó.
Musa aliwaambia wana wa Israeli kila kitu ambacho BWANA alikuwa amemwamuru kusema.