< San Mateo 22 >
1 Jesús les habló otra vez en parábolas:
Yesu alisema nao tena katika mifano, akisema,
2 El reino celestial puede compararse a un rey que hizo fiesta de bodas para su hijo.
“Ufalme wa mbinguni unafanana na mfalme aliyeandaa sherehe ya harusi ya mwanawe.
3 Envió a sus esclavos a llamar a los invitados a la fiesta de bodas, pero no quisieron ir.
Akawatuma watumishi wake kuwakaribisha waliokuwa wamealikwa kuja katika sherehe ya harusi, lakini hawakufika.
4 Volvió a enviar a otros esclavos y dijo: Anuncien a los invitados: Miren, preparé mi banquete. Sacrifiqué mis novillos y las reses engordadas. Todo está dispuesto. Vengan a la fiesta de bodas.
Mfalme aliwatuma tena watumishi wengine, akisema. “Waambieni wote walioalikwa, Angalieni, nimeandaa chakula. Fahali na ndama wangu wanono wamechinjwa, na mambo yote yako tayari, Njoni katika sherehe ya harusi.”
5 Pero ellos no tomaron en cuenta la invitación. Se fueron, uno a su campo, el otro a su negocio,
Lakini watu hao hawakuzingatia kwa dhati mwaliko wake. Baadhi walirejea katika mashamba yao, na wengine walirudi katika sehemu zao za biashara.
6 y los demás detuvieron a los esclavos [enviados], los maltrataron y los mataron.
Wengine waliwainukia watumishi wa mfalme na kuwadharirisha na kuwaua.
7 Entonces el rey se enfureció, envió sus ejércitos, mató a aquellos homicidas y quemó su ciudad.
Lakini mfalme alikasirika. Alituma jeshi lake, akawaua wale wauaji na kuuteketeza mji wao kwa moto.
8 Después dijo a sus esclavos: La boda a la verdad está preparada, pero los invitados no eran dignos.
Kisha aliwaambia watumishi wake, “Harusi iko tayari, lakini walioalikwa hawakustahili.
9 Por tanto vayan a las encrucijadas de los caminos y llamen a cuantos hallen a la fiesta de bodas.
Kwa hiyo nendeni kwenye makutano ya njia kuu, waalikeni watu wengi kadri iwezekanavyo waje kwenye sherehe ya harusi.”
10 Y cuando aquellos esclavos salieron a los caminos, reunieron a todos los que hallaron, tanto malos como buenos, y el salón de bodas se llenó de invitados.
Watumishi walienda njia kuu na kuwakaribisha watu wowote waliowaona, wema na wabaya. Hivyo ukumbi wa harusi ulijaa wageni.
11 Pero cuando el rey entró a ver a los invitados, encontró allí a un hombre que no estaba vestido con traje de boda.
Lakini mfalme alipoingia kuwatazama wageni, alimuona mtu mmoja ambaye hakuvaa vazi rasmi la harusi!
12 Y le dijo: Amigo, ¿cómo entraste aquí sin traje de boda? Pero él enmudeció.
Mfalme alimwuliza, 'Rafiki, ulipataje kufika hapa ndani bila vazi la harusi?' Na mtu huyo hakujibu chochote.
13 Entonces el rey dijo a los sirvientes: Átenlo de pies y manos y échenlo a la oscuridad de afuera. Allí será el llanto y el crujido de los dientes,
Ndipo mfalme alipowaambia watumishi wake, “Mfungeni mtu huyu mikono na miguu na mtupeni nje katika giza, huko ambako kutakuwa na kilio na kusaga meno.
14 porque muchos son [los] llamados, pero pocos [los ]escogidos.
Kwa kuwa watu wengi wanaitwa, lakini wateule ni wachache.”
15 Entonces los fariseos se fueron y deliberaron cómo enredarlo en alguna palabra.
Ndipo Mafarisayo waliondoka na kupanga jinsi ya kumkamata Yesu katika maneno yake mwenyewe.
16 Le enviaron a los discípulos de ellos con los herodianos para que dijeran: Maestro, sabemos que eres veraz y enseñas con verdad el camino de Dios. No te cuidas de nadie, pues no miras la apariencia de los hombres.
Ndipo walipowatuma wanafunzi wao pamoja na Maherode. Na walimwambia Yesu, “Mwalimu, tunajua kuwa wewe ni mtu wa kweli, na kwamba unafundisha matakwa ya Mungu katika ukweli. Haujali maoni ya mtu mwingine na hauoneshi upendeleo kwa watu.
17 Dinos. ¿Qué te parece? ¿Es lícito pagar tributo a César, o no?
Kwa hiyo tuambie, unafikiri nini? Je, ni sahihi kisheria kulipa kodi kwa Kaisari au hapana?”
18 Pero Jesús entendió la malicia de ellos y respondió: ¿Por qué me tientan, hipócritas?
Yesu alifahamu uovu wao na akasema, “Kwa nini mnanijaribu, enyi wanafiki?
19 Muéstrenme la moneda del tributo. Y ellos le presentaron un denario.
Nionesheni pesa itumikayo kulipia kodi.” Ndipo wakamletea dinari.
20 Les preguntó: ¿De quién es la imagen y la inscripción?
Yesu akawauliza, “Sura na jina hili ni vya nani?”
21 Contestaron: De César. Entonces les ordenó: Den, pues, a César lo de César, y a Dios lo de Dios.
Wakamjibu, “Vya Kaisari.” Ndipo Yesu akawaambia, “Mpeni Kaisari vitu vilivyo vyake na vya Mungu mpeni Mungu.”
22 Al oír [esto] se maravillaron, lo dejaron y salieron.
Waliposikia hivyo walishangaa. Kisha walimwacha na kwenda zao.
23 Aquel día se le acercaron [los] saduceos, quienes dicen que no hay resurrección, y le preguntaron:
Siku hiyo baadhi ya Masadukayo walikuja kwa Yesu, wale wasemao kuwa hakuna ufufuo wa wafu. Wakamwuliza,
24 Maestro, Moisés dijo: Si alguno muere y no tiene hijos, su hermano se casará con la esposa de él y levantará descendencia a su hermano.
wakisema, “Mwalimu, Musa alisema, Ikiwa mtu amefariki bila kuzaa watoto, ndugu yake na amrithi huyo mwanamke na ampatie mtoto kwa ajili ya ndugu yake.
25 Ahora bien, había entre nosotros siete hermanos. El primero que se casó, murió, y como no tenía descendencia, dejó su esposa a su hermano.
Walikuwapo ndugu saba. Wa kwanza alioa na kisha akafariki bila kuzaa watoto. Akamwachia mke nduguye.
26 De la misma manera, también el segundo y el tercero, hasta el séptimo.
Kisha ndugu yake wa pili naye akafanya vivyo hivyo, kisha yule wa tatu, ikawa hivyo hadi kwa yule wa saba.
27 Al final de todos, murió la mujer.
Baada ya kufanya hivyo wote, yule mwanamke naye alifariki.
28 En la resurrección, ¿de cuál de los siete será esposa? Porque todos la tuvieron.
Sasa katika ufufuo huyo mwanamke atakuwa mke wa nani katika ndugu hao saba? Kwa sababu wote walimuoa.”
29 Jesús les respondió: Están errados porque no entienden las Escrituras ni el poder de Dios.
Lakina Yesu aliwajibu na kuwaambia, “Mnakosea, kwa sababu hamjui Maandiko wala nguvu za Mungu.
30 Porque en la resurrección, no se casan ni son dados en casamiento, sino son como los ángeles en el cielo.
Kwa kuwa katika ufufuo, watu hawaoi wala kuolewa. Badala yake watu huwa kama malaika huko mbinguni.
31 Pero en cuanto a la resurrección de los muertos, ¿no leyeron lo dicho por Dios a ustedes:
Lakini kuhusu ufufuo wa wafu, hamjawahi kusoma kile ambacho Mungu alikisema kwenu, akisema,
32 Yo soy el Dios de Abraham, de Isaac, y de Jacob? Dios no es Dios de muertos sino de vivos.
Mimi ni Mungu wa Ibrahimu, Mungu wa Isaka, na Mungu wa Yakobo? Mungu si Mungu wa wafu, bali ni Mungu wa walio hai.”
33 La multitud oyó y se maravilló de su doctrina.
Wakati kusanyiko waliposikia hili, waliyashangaa mafundisho yake.
34 Entonces, al oír los fariseos que [Jesús] silenció a los saduceos, se pusieron de acuerdo.
Lakini Mafarisayo waliposikia kuwa Yesu amewanyamazisha Masadukayo, walijikusanya wao wenyewe kwa pamoja.
35 Uno de ellos, para tentarlo, le preguntó:
Mmoja wao, akiwa mwana sheria, alimwuliza swali kwa kumjaribu.
36 Maestro, ¿cuál es [el ]gran Mandamiento en la Ley?
“Mwalimu, ni amri ipi iliyo kuu kuliko zote katika sheria?”
37 Le respondió: Amarás al Señor tu Dios con todo tu corazón, con toda tu alma y con toda tu mente.
Yesu akamjibu, “Lazima umpende Bwana kwa moyo wako wote, kwa roho yako yote, na kwa akili zako zote.
38 Éste es el grande y primer Mandamiento,
Hii ndiyo amri iliyo kuu na ya kwanza.
39 y el segundo es semejante a éste: Amarás a tu prójimo como a ti mismo.
Na ya pili inafanana na hiyo- Ni lazima kumpenda jirani yako kama unavyojipenda mwenyewe.
40 De estos dos Mandamientos dependen toda la Ley y los profetas.
Sheria zote na Manabii hutegemea amri hizi mbili.”
41 Se reunieron los fariseos y Jesús les preguntó:
Na Mafarisayo walipokuwa bado wamejikusanya pamoja, Yesu aliwauliza swali.
42 ¿Qué piensan ustedes del Cristo? ¿De quién es Hijo? Le respondieron: De David.
Akisema, “J! e, Mwafikiri nini juu ya Kristo? Yeye ni Mwana wa nani?” Nao wakamjibu, “Ni mwana wa Daudi.”
43 Les preguntó: ¿Pues cómo David en espíritu lo llama Señor? Dice:
Yesu akawajibu, “Ni kwa namna gani Daudi katika Roho anamwita Bwana, akisema,
44 Dijo el Señor a mi Señor: Siéntate a mi mano derecha Hasta que ponga a tus enemigos debajo de tus pies.
'Bwana alimwambia Bwana wangu, “Kaa mkono wangu wa kuume, hadi nitakapowafanya maadui zako wawekwe chini ya miguu yako.”'?”
45 Pues si David lo llama Señor, ¿cómo es su Hijo?
Kama Daudi anamwita Kristo “Bwana,” jinsi gani atakuwa mtoto wake?”
46 Nadie le podía responder, y desde aquel día nadie más se atrevió a preguntarle algo.
Hakuna aliyeweza kumjibu neno tena, na hakuna aliyethubutu tena kumwuliza maswali zaidi tangu siku hiyo na kuendelea.