< Levítico 3 >
1 Si su ofrenda es un sacrificio de paz, si ofrece de la manada de ganado vacuno, sea macho o hembra, lo presentará sin defecto a Yavé.
“‘Kama sadaka ya mtu ni sadaka ya amani, naye akatoa ngʼombe kutoka kundi, akiwa dume au jike, atamleta mnyama asiye na dosari mbele za Bwana.
2 Pondrá su mano sobre la cabeza del animal y lo degollará en la entrada del Tabernáculo de Reunión. Los sacerdotes hijos de Aarón rociarán la sangre sobre el altar por todos los lados.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake na kumchinja penye ingilio la Hema la Kukutania. Ndipo makuhani wana wa Aroni watanyunyiza damu yake pande zote za madhabahu.
3 Del sacrificio de la ofrenda de paz, presentarán una ofrenda quemada a Yavé con la grasa que cubre los intestinos, toda la que hay sobre los órganos internos,
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yote ya mnyama yafunikayo sehemu za ndani, ama yanayoungana na hizo sehemu za ndani,
4 los dos riñones y la grasa que los cubre, y sobre las ijadas y la grasa del hígado, la cual quitará junto con los riñones.
figo zote pamoja na mafuta yote yanayozizunguka karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
5 Los hijos de Aarón harán arder esto en el altar, encima del holocausto que estará sobre la leña en el fuego. Es ofrenda quemada de olor que apacigua a Yavé.
Kisha wana wa Aroni wataiteketeza juu ya madhabahu, juu ya ile sadaka ya kuteketezwa iliyoko juu ya kuni zinazowaka, kama sadaka ya kuteketezwa kwa moto, harufu nzuri ya kumpendeza Bwana.
6 Si su ofrenda para el sacrificio de ofrenda de paz a Yavé es del rebaño, lo presentará sin defecto, macho o hembra.
“‘Kama akitoa kondoo au mbuzi kutoka kundi kama sadaka ya amani kwa Bwana, atamtoa dume au jike asiye na dosari.
7 Si lleva un cordero como ofrenda, lo presentará delante de Yavé,
Kama akimtoa mwana-kondoo, atamleta mbele za Bwana.
8 pondrá su mano sobre la cabeza del animal y lo degollará delante del Tabernáculo de Reunión. Luego, los hijos de Aarón rociarán su sangre sobre el altar por todos los lados.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa cha sadaka yake, naye atamchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
9 Del sacrificio de la ofrenda de paz presentarán como ofrenda quemada a Yavé la grasa y la cola entera, cortada desde el espinazo, así como la grasa que cubre los intestinos, toda la grasa que hay sobre los órganos internos,
Kutoka kwenye hiyo sadaka ya amani ataleta dhabihu iliyotolewa kwa Bwana kwa moto: mafuta yake, mafuta yote ya mkia uliokatwa karibu na uti wa mgongo, mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani au yale yanayounganika nazo,
10 los dos riñones, la grasa que los cubre, y sobre las ijadas y la grasa del hígado, la cual quitará con los riñones.
figo mbili pamoja na mafuta yanayozizunguka yaliyo karibu na kiuno na yale yanayofunika ini, ambayo atayatoa pamoja na figo.
11 El sacerdote los hará arder sobre el altar como alimento de ofrenda quemada a Yavé.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa Bwana kwa moto.
12 Si su ofrenda es una cabra, la presentará a Yavé,
“‘Kama sadaka yake ni mbuzi, ataileta mbele za Bwana.
13 pondrá su mano sobre la cabeza de ella y la degollará delante del Tabernáculo de Reunión. Después los hijos de Aarón rociarán su sangre sobre el altar por todos los lados.
Ataweka mkono wake juu ya kichwa chake na kumchinja mbele ya Hema la Kukutania. Kisha wana wa Aroni watanyunyiza damu yake kwenye madhabahu pande zote.
14 Después ofrecerá de ella su ofrenda quemada a Yavé: la grasa que cubre los órganos internos, toda la grasa que cubre las vísceras,
Kutokana na ile sadaka anayotoa, atatoa sadaka hii kwa Bwana kwa moto: mafuta yote yanayofunika sehemu za ndani na yale yanayoungana nazo,
15 los dos riñones con la grasa que los cubre y sobre las ijadas, y la grasa del hígado, la cual quitará con los riñones.
figo zote mbili pamoja na mafuta yaliyo juu yake karibu na kiuno na yanayofunika ini, ambayo atayaondoa pamoja na figo.
16 Luego el sacerdote los hará arder sobre el altar. Es ofrenda quemada, alimento de olor que apacigua a Yavé. Toda la grasa es de Yavé.
Kuhani ataviteketeza juu ya madhabahu kama chakula, sadaka iliyotolewa kwa moto, harufu nzuri. Mafuta yote ya mnyama ni ya Bwana.
17 Es estatuto perpetuo para sus generaciones dondequiera que vivan: no comerán grasa ni sangre.
“‘Hii ni kanuni ya kudumu kwa vizazi vijavyo, popote muishipo: Msile mafuta yoyote ya mnyama wala damu.’”