< Josué 19 >
1 La segunda suerte tocó a la tribu de los hijos de Simeón según sus familias. Su herencia estaba en medio de la heredad de los hijos de Judá.
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 En su heredad tenían Beerseba, Seba, Molada,
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Hasar-sual, Bala, Esem,
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Heltolad, Betul, Horma,
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Siclag, Bet-marcabot, Hasar-susa,
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Bet-lebaot y Saruhén: 13 ciudades con sus aldeas.
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Y Aín, Rimón, Eter y Asán: cuatro ciudades con sus aldeas.
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 Todas las aldeas que estaban alrededor de estas ciudades hasta Balat-beer, que es Ramat del Neguev. Esta es la heredad de la tribu de los hijos de Simeón, según sus familias.
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 De la porción de los hijos de Judá se tomó la heredad de los hijos de Simeón, ya que la parte de los hijos de Judá era muy grande para ellos. Así que los hijos de Simeón tuvieron su heredad en medio de la herencia de aquéllos.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 La tercera suerte tocó a los hijos de Zabulón, según sus familias, y el límite de su heredad llegaba hasta Sarid.
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 Por el oeste su límite subía hasta Marala y llegaba hasta Dabeset, y de allí hasta el arroyo que está delante de Jocneam,
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 de Sarid volvía hacia el este, hacia donde sale el sol, hasta el lindero de Quislot-tabor, salía a Daberat y subía a Jafía.
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 De allí pasaba al este, a Gat-jefer, hasta Et-cazín, y se extendía hasta Rimón, la cual limita con Nea.
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 Después el límite giraba al norte, hacia Hanatón, e iba a salir al valle de Jefte-el,
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 donde están Catat, Nahalal, Simrón, Ideala y Belén: 12 ciudades con sus aldeas.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 Esta es la heredad de los hijos de Zabulón según sus familias. Estas ciudades con sus aldeas.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 La cuarta suerte salió para Isacar, para los hijos de Isacar según sus familias.
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Su territorio fue Jezreel, Quesulot, Sunem,
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hafaráim, Sihón, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remet, En-ganim, En-hada y Bet-pases.
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 El límite llegaba hasta Tabor, Sahasima y Bet-semes, y su lindero terminaba en el Jordán: 16 ciudades con sus aldeas.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Isacar según sus familias. Esas ciudades con sus aldeas.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 La quinta suerte salió para la tribu de los hijos de Aser, según sus familias.
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Su territorio fue: Helcat, Halí, Betén, Acsaf,
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Alamelec, Amad y Miseal, y llegaba hasta el oeste de la montaña Carmelo y a Sihor-libnat.
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 Después volvía hacia donde sale el sol hasta Bet-dagón, llegaba hasta Zabulón y al valle de Jefte-el, hacia el norte de Bet-emec y a Neiel, y salía por el norte a Cabul,
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 a Hebrón, a Rehob, a Hamón y a Caná, hasta la gran Sidón.
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 De allí el límite volvía hacia Ramá y hacia la ciudad fortificada de Tiro, regresaba hacia Hosa, y salía al mar por el territorio de Aczib,
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 Uma, Afec y Rehob: 22 ciudades con sus aldeas.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Aser según sus familias. Esas ciudades con sus aldeas.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 La sexta suerte tocó a los hijos de Neftalí según sus familias.
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Su lindero iba desde Hélef, Alón-saananim, Adami-néqueb y Jabneel, hasta Lacum, y salía al Jordán.
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 Desde allí el límite volvía hacia el oeste hasta Aznot-tabor, y de allí a Hucoc, y llegaba hasta Zabulón por el sur, y por el oeste limitaba con Aser y con Judá en el Jordán, hacia donde sale sol.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 Y las ciudades fortificadas eran: Sidim, Ser, Hamat, Racat, Cineret,
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
37 Cedes, Edrei, En-hazor,
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Irón, Migdal-el, Horem, Bet-anat y Bet-semes: 19 ciudades con sus aldeas.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 Esta es la heredad de la tribu de los hijos de Neftalí según sus familias. Esas ciudades con sus aldeas.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 La séptima suerte salió para la tribu de los hijos de Dan por sus familias.
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 El territorio de su herencia fue Zora, Estaol, Ir-semes,
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Saalabín, Ajalón, Jetla,
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
44 Elteque, Gibetón, Baalat,
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jehúd, Bene-berac, Gat-rimón,
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Me-harcón, y Racón, con el territorio que está frente a Jope.
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 El territorio de los hijos de Dan se amplió, pues subieron y atacaron a Lesem. La capturaron, la pasaron a filo de espada, la poseyeron y se establecieron en ella. A Lesem la llamaron Dan, por el nombre de su antepasado Dan.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 Esta es la heredad de la tribu de los hijos de Dan según sus familias, esas ciudades con sus aldeas.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 Cuando acabaron de distribuir la tierra según sus límites, los hijos de Israel dieron heredad a Josué, hijo de Nun, en medio de ellos.
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 Según el mandamiento de Yavé, le dieron la ciudad que él pidió: Timnat-sera, en la región montañosa de Efraín. Él reedificó la ciudad y vivió en ella.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 Estas son las heredades que el sacerdote Eleazar y Josué, hijo de Nun, y los jefes de las casas paternas repartieron por sorteo entre las tribus de los hijos de Israel en Silo, en presencia de Yavé, en la entrada del Tabernáculo de Reunión. Así acabaron de repartir la tierra.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.