< Job 7 >
1 ¿No es el destino del hombre en la tierra una lucha? ¿No son sus días como los de un jornalero,
“Je, mwanadamu hana kazi ngumu duniani? Siku zake si kama zile za mtu aliyeajiriwa?
2 Como el esclavo que anhela la sombra o como un jornalero que espera su pago?
Kama mtumwa anavyovionea shauku vivuli vya jioni, au mtu aliyeajiriwa anavyoungojea mshahara wake,
3 Así yo heredé meses sin provecho y me fueron asignadas noches de aflicción.
ndivyo nilivyogawiwa miezi ya ubatili, nami nimeandikiwa huzuni usiku hata usiku.
4 Cuando estoy acostado digo: ¿Cuándo me levantaré? Y la noche se alarga, y me lleno de inquietudes hasta el alba.
Wakati nilalapo ninawaza, ‘Itachukua muda gani kabla sijaamka?’ Usiku huwa mrefu, nami najigeuzageuza hadi mapambazuko.
5 Mi carne está cubierta de gusanos y de costras de polvo. Mi piel se agrieta y supura.
Mwili wangu umevikwa mabuu na uchafu, ngozi yangu imetumbuka na kutunga usaha.
6 Mis días se me van más veloces que la lanzadera y se me acaban sin esperanza.
“Siku zangu zinapita upesi kuliko mtande wa kufuma, nazo zinafikia mwisho wake bila matumaini.
7 Acuérdate que mi vida es un soplo. Mis ojos no volverán a ver el bien.
Kumbuka, Ee Mungu, maisha yangu ni kama pumzi; macho yangu kamwe hayataona tena raha.
8 El ojo del que me ve ya no me verán. Tus ojos se fijarán en mí, pero no existiré.
Lile jicho linaloniona sasa halitaniona tena; utanitafuta, wala sitakuwepo.
9 Como la nube se deshace y se va, así el que baja al Seol no subirá. (Sheol )
Kama vile wingu liondokavyo na kutoweka, vivyo hivyo yeye ashukaye kaburini harudi tena. (Sheol )
10 No regresa a su vivienda y ya no lo reconoce su lugar.
Kamwe harudi tena nyumbani mwake; wala mahali pake hapatamjua tena.
11 Por tanto, no refrenaré mi boca. Hablaré en la angustia de mi espíritu. Me quejaré en la amargura de mi alma.
“Kwa hiyo sitanyamaza; nitanena kutokana na maumivu makuu ya roho yangu, nitalalama kwa uchungu wa nafsi yangu.
12 ¿Soy yo el mar o el monstruo marino para que asignes guardia sobre mí?
Je, mimi ni bahari, au mnyama mkubwa mno akaaye vilindini, hata uniweke chini ya ulinzi?
13 Si digo: Me consolará mi lecho, mi cama aliviará mi queja,
Ninapofikiri kwamba kitanda changu kitanifariji, nacho kiti changu cha fahari kitapunguza malalamiko yangu,
14 entonces me aterras con sueños y me turbas con visiones.
ndipo wanitisha kwa ndoto na kunitia hofu kwa maono,
15 De manera que mi alma prefiere la asfixia, la muerte más bien que mis huesos.
hivyo ninachagua kujinyonga na kufa, kuliko huu mwili wangu.
16 Repugno la vida. No voy a vivir para siempre. Déjame, mis días son vanidad.
Ninayachukia maisha yangu; nisingetamani kuendelea kuishi. Niache; siku zangu ni ubatili.
17 ¿Qué es el hombre para que lo engrandezcas, para que te preocupes por él,
“Mwanadamu ni kitu gani hata umjali kiasi hiki, kwamba unamtia sana maanani,
18 para que lo examines cada mañana y lo pruebes en todo momento?
kwamba unamwangalia kila asubuhi na kumjaribu kila wakati?
19 ¿Hasta cuándo no apartarás tu mirada de mí, ni me soltarás para que trague saliva?
Je, hutaacha kamwe kunitazama, au kuniacha japo kwa kitambo kidogo tu?
20 Si pequé, ¿cuál [daño] te hago a Ti, oh Guardián de los hombres? ¿Por qué me pones como blanco tuyo hasta convertirme en una carga para mí mismo?
Ikiwa nimetenda dhambi, nimekufanyia nini, Ewe mlinzi wa wanadamu? Kwa nini umeniweka niwe shabaha yako? Je, nimekuwa mzigo kwako?
21 ¿Por qué no quitas mi rebelión y perdonas mi iniquidad? Porque ahora me acostaré en el polvo. Tú me buscarás, pero no estaré.
Kwa nini husamehi makosa yangu na kuachilia dhambi zangu? Kwa kuwa hivi karibuni nitalala mavumbini; nawe utanitafuta, wala sitakuwepo.”