< Job 40 >

1 Además, Yavé respondió a Job:
Yahweh aliendelea kuongea na Ayubu na kusema,
2 ¿El que contiende con ʼEL-Shadday lo corrige? El que argumenta con ʼEloah, responda.
“Je mtu yeyote anayetaka kukosoa na ajaribu kumsahihisha Mwenye enzi? Na yeye anayehojiana na Mungu, na ajibu yeye.”
3 Entonces Job respondió a Yavé:
Ndipo Ayubu akamjibu Yahweh na kusema, “
4 Ciertamente, soy insignificante. ¿Qué puedo responderte? Pongo mi mano sobre mi boca.
Tazama, mimi si mtu muhimu; je nawezaje kukujibu? Ninauweka mkono wangu juu ya mdomo wangu.
5 Una vez hablé, pero no responderé más. Y aun dos veces, pero nada.
Ninazungumza mara moja, na sitakujibu; hakika, mara mbili, lakini sitaendelea zaidi.”
6 Entonces Yavé respondió a Job desde el remolino de viento:
Kisha Yahweh akamjibu Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kusema,
7 Cíñete ahora tu cintura como varón. Yo te preguntaré, y tú me responderás:
“Jifunge sasa mkanda kiunoni mwako kama mwanaume, kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
8 ¿Invalidarás mi juicio? ¿Me condenarás para justificarte?
Je waweza kusema kwa hakika kwamba mimi si mwenye haki? Je utanihukumu mimi ili useme wewe ni mwenye haki?
9 Si tienes un brazo como el de ʼEL, y tu voz truena con una voz como la suya,
Je una mkono kama wa Mungu? Je waweza kutoa kishindo kwa sauti kama yeye?
10 adórnate de majestad y esplendor. Cúbrete de honra y majestad.
Jivike sasa katika utukufu na katika utu; jivalie mwenyewe heshima na enzi.
11 Derrama el ardor de tu ira, y abate con una mirada al soberbio.
Sambaza ziada ya hasira yako; mtazame kila mmoja mwenye kiburi na umshushe chini.
12 Observa a todo arrogante y humíllalo. Quebranta a los perversos en su sitio,
Mwangalie kila mmoja mwenye kiburi na umweke chini; wakanyage chini watu waovu mahali wanaposimama.
13 entiérralos juntos en el polvo y véndales los semblantes en la oscuridad.
Wazike ardhini pamoja; zifunge nyuso zao katika sehemu zilizositirika.
14 Entonces Yo también reconoceré que tu mano derecha puede salvarte.
Ndipo pia nitakapokubali ya kwamba mkono wako wa kulia waweza kukuokoa.
15 Contempla ahora al hipopótamo al cual hice como a ti. Come hierba como un buey.
Mwangalie sasa kiboko, ambaye niliwafanya kama nilivyokufanya wewe; anakula nyasi kama ng'ombe.
16 Ciertamente la fuerza está en sus lomos. Su vigor en su vientre musculoso
Ona sasa, nguvu zake ziko katika viuno vyake; nguvu zake zi katika mishipa ya tumbo lake.
17 cuando entiesa su cola como un cedro, y tensa los tendones de los muslos.
Yeye huuondoa mkia wake kama mti wa mwerezi; mishipa ya paja lake imeunganishwa pamoja.
18 Sus huesos son como tubos de bronce, su osamenta como barras de hierro.
Mifupa yake ni kama ya mirija ya shaba; na miguu yake ni kama kipande cha chuma.
19 Él es el principal de los procedimientos de ʼEL. Solo su Hacedor puede acercarle su espada.
Yeye ni mkuu wa viumbe vya Mungu. Ni Mungu pekee, ambaye alimwumba, anaweza kumshinda.
20 Las montañas producen hierba para él, y las bestias del campo retozan allí.
Kwa kuwa milima humpatia chakula; hayawani wa mashambani hucheza karibu.
21 Se recuesta debajo de las plantas de loto y se oculta entre los juncos del pantano.
Hujilaza chini ya mimiea ya kivuli katika makao ya mianzi, na katika bwawa la matope.
22 Lo cubren los lotos con su sombra y lo rodean los sauces del arroyo.
Miti yenye vivuli humfunika katika vivuli vyake; mierebi ya kijito inamzunguka pande zote.
23 Ciertamente, cuando el río se desborda, él no se alarma. Aunque el Jordán espumee contra su hocico, queda tranquilo
Tazama, kama mto utazigharikisha kingo zake, hatikisiki; yeye anajiamini, hata kama Mto wa Yordani unajaa hadi katika pua yake.
24 ¿Puede alguien vigilarlo y capturarlo al perforar sus fosas nasales con un garfio?
Je mtu yeyote aweza kumnasa kwa ndoano, au kuichoma pua yake kwa mtego?

< Job 40 >