< Job 40 >
1 Además, Yavé respondió a Job:
Bwana akamwambia Ayubu:
2 ¿El que contiende con ʼEL-Shadday lo corrige? El que argumenta con ʼEloah, responda.
“Je, mwenye kushindana na Mwenyezi aweza kumsahihisha? Mwenye kumlaumu Mungu na ajibu.”
3 Entonces Job respondió a Yavé:
Ndipo Ayubu akamjibu Bwana:
4 Ciertamente, soy insignificante. ¿Qué puedo responderte? Pongo mi mano sobre mi boca.
“Mimi sistahili kabisa: ninawezaje kukujibu wewe? Nauweka mkono wangu juu ya kinywa changu.
5 Una vez hablé, pero no responderé más. Y aun dos veces, pero nada.
Nimesema mara moja, lakini sina jibu; naam, nimesema mara mbili, lakini sitasema tena.”
6 Entonces Yavé respondió a Job desde el remolino de viento:
Ndipo Bwana akasema na Ayubu kutoka upepo wa kisulisuli:
7 Cíñete ahora tu cintura como varón. Yo te preguntaré, y tú me responderás:
“Jikaze kama mwanaume; nitakuuliza maswali, nawe yakupasa unijibu.
8 ¿Invalidarás mi juicio? ¿Me condenarás para justificarte?
“Je, utabatilisha hukumu yangu? Utanilaumu mimi ili kujihesabia haki mwenyewe?
9 Si tienes un brazo como el de ʼEL, y tu voz truena con una voz como la suya,
Je, una mkono kama wa Mungu, nawe waweza kutoa sauti ya ngurumo kama yake?
10 adórnate de majestad y esplendor. Cúbrete de honra y majestad.
Basi jivike mwenyewe utukufu na fahari, nawe uvae heshima na enzi.
11 Derrama el ardor de tu ira, y abate con una mirada al soberbio.
Fungulia ukali wa ghadhabu yako, mtafute kila mwenye kiburi umshushe,
12 Observa a todo arrogante y humíllalo. Quebranta a los perversos en su sitio,
mwangalie kila mtu mwenye kiburi na umnyenyekeze, waponde waovu mahali wasimamapo.
13 entiérralos juntos en el polvo y véndales los semblantes en la oscuridad.
Wazike wote mavumbini pamoja; wafunge nyuso zao kaburini.
14 Entonces Yo también reconoceré que tu mano derecha puede salvarte.
Ndipo mimi mwenyewe nitakukubalia kuwa mkono wako mwenyewe wa kuume unaweza kukuokoa.
15 Contempla ahora al hipopótamo al cual hice como a ti. Come hierba como un buey.
“Mwangalie mnyama aitwaye Behemothi, niliyemuumba kama nilivyokuumba wewe, anayekula majani kama ngʼombe.
16 Ciertamente la fuerza está en sus lomos. Su vigor en su vientre musculoso
Tazama basi nguvu alizo nazo kwenye viuno vyake, uwezo alio nao kwenye misuli ya tumbo lake!
17 cuando entiesa su cola como un cedro, y tensa los tendones de los muslos.
Mkia wake hutikisika kama mwerezi; mishipa ya mapaja yake imesukwa pamoja.
18 Sus huesos son como tubos de bronce, su osamenta como barras de hierro.
Mifupa yake ni bomba za shaba, maungo yake ni kama fito za chuma.
19 Él es el principal de los procedimientos de ʼEL. Solo su Hacedor puede acercarle su espada.
Yeye ni wa kwanza miongoni mwa kazi za Mungu, lakini Muumba wake anaweza kumsogelea kwa upanga wake.
20 Las montañas producen hierba para él, y las bestias del campo retozan allí.
Vilima humletea yeye mazao yake, nao wanyama wote wa porini hucheza karibu naye.
21 Se recuesta debajo de las plantas de loto y se oculta entre los juncos del pantano.
Hulala chini ya mimea ya yungiyungi, katika maficho ya matete kwenye matope.
22 Lo cubren los lotos con su sombra y lo rodean los sauces del arroyo.
Hiyo mimea ya yungiyungi humficha kwenye vivuli vyake; miti mirefu karibu na kijito humzunguka.
23 Ciertamente, cuando el río se desborda, él no se alarma. Aunque el Jordán espumee contra su hocico, queda tranquilo
Wakati mto ufurikapo, yeye hapati mshtuko wa hofu; yeye yu salama, hata kama Yordani ingefurika hadi kwenye kinywa chake.
24 ¿Puede alguien vigilarlo y capturarlo al perforar sus fosas nasales con un garfio?
Je, mtu yeyote anaweza kumkamata yeye akiwa macho, au kumnasa kwa mtego na kutoboa pua yake?