< Job 39 >
1 ¿Sabes tú cuándo paren las cabras monteses? ¿Asististe al parto de las venadas?
“Je, wajua ni wakati gani mbuzi wa mlimani wanapozaa? Je, watambua ni wakati gani kulungu jike azaapo mtoto wake?
2 ¿Puedes contar los meses de su preñez y saber el tiempo cuando paren?
Je, waweza kuhesabu miezi hadi wazaapo? Je, unajua majira yao ya kuzaa?
3 Se encorvan, expulsan sus crías, se libran de sus dolores de parto.
Wao hujiinamisha na kuzaa watoto wao; utungu wa kuzaa unakoma.
4 Sus crías crecen, se fortalecen, salen a campo abierto y no vuelven.
Watoto wao hustawi na kuongezeka nguvu nyikani; huenda zao wala hawarudi tena.
5 ¿Quién dio al asno montés su libertad? ¿Quién soltó las ataduras del rebuznante,
“Ni nani aliyemwachia punda-mwitu awe huru? Ni nani aliyezifungua kamba zake?
6 a cual di el desierto como hogar y tierra salitrosa como vivienda?
Nimempa nchi isiyokaliwa na watu kuwa masikani yake, nchi ya chumvi kuwa makao yake.
7 Se burla del bullicio de la ciudad y no obedece los gritos del arriero,
Huzicheka ghasia za mji, wala hasikii kelele za mwendesha gari.
8 explora las montañas en busca de su pasto y rastrea toda cosa verde.
Huzunguka vilimani kwa ajili ya malisho na kutafuta kila kitu kibichi.
9 ¿Consentirá el búfalo en ser tu esclavo o pasará la noche en tu establo?
“Je, nyati atakubali kukutumikia? Atakaa karibu na hori lako usiku?
10 ¿Atarás al búfalo al arado con cuerdas? ¿Rastrillará los valles tras ti?
Je, waweza kumfungia kwenye matuta kwa kamba? Je, atalima mabonde nyuma yako?
11 ¿Confiarás en él porque es robusto y dejarás tu labor a su cuidado?
Je, utamtumainia kwa ajili ya nguvu zake nyingi? Utamwachia yeye kazi zako nzito?
12 ¿Confiarás en él para que te traiga tu cosecha y reúna el grano en tu era?
Utaweza kumwamini akuletee nafaka yako nyumbani kutoka shambani na kuikusanya kwenye sakafu yako ya kupuria?
13 Las alas del avestruz se agitan alegres, ¿pero son las alas y el plumaje del amor?
“Mbuni hupigapiga mabawa yake kwa furaha, lakini hayawezi kulinganishwa na mabawa na manyoya ya korongo.
14 Abandona sus huevos en la tierra, en el polvo los calienta
Huyataga mayai yake juu ya ardhi, na kuyaacha yapate joto mchangani,
15 y se olvida que un pie puede aplastarlos o una bestia salvaje pisotearlos.
bila kujali kuwa mguu waweza kuyaponda, kwamba baadhi ya wanyama wa porini wanaweza kuyakanyaga.
16 Es cruel con sus polluelos como si no fueran suyos. No le importa que se pierda su fatiga,
Yeye huyafanyia makinda yake ukatili kama vile si yake; hajali kwamba taabu yake inaweza ikawa bure,
17 porque ʼEloah lo privó de sabiduría y no lo dotó de entendimiento.
kwa kuwa Mungu hakumjalia hekima, wala hakumpa fungu la akili njema.
18 Pero cuando se yergue en alto, se burla del caballo y su jinete.
Lakini akunjuapo mabawa yake kukimbia, humcheka farasi pamoja na yeye aliyempanda.
19 ¿Diste al caballo su fuerza? ¿Cubriste tú su cuello con una melena?
“Je, wewe humpa farasi nguvu au kuivika shingo yake manyoya marefu?
20 ¿Lo harás brincar como langosta? Su majestuoso resoplido es terrible,
Je, wewe humfanya farasi aruke kama nzige, akistaajabisha kwa tishio la mlio wake wa majivuno?
21 escarba en el valle, se regocija en su fuerza, sale a encontrarse con las armas,
Huparapara bila woga, akizifurahia nguvu zake, husonga mbele kukabiliana na silaha.
22 se ríe del miedo y no se espanta ni retrocede ante la espada.
Huicheka hofu, haogopi chochote, wala haukimbii upanga.
23 La flecha resuena contra él. Fulguran lanzas y arma arrojadiza,
Podo hutoa sauti kando yake, pamoja na mkuki unaongʼaa na fumo.
24 con ímpetu y furor devora la distancia, sin que le importe el sonido de la trompeta.
Bila woga na kwa ghadhabu huimeza nchi, wala tarumbeta iliapo yeye hawezi kusimama.
25 Parece que dice entre clarines: ¡Ea! Olfatea desde lejos la batalla, el grito de los comandantes y el grito de guerra.
Asikiapo sauti ya baragumu yeye hulia, ‘Aha!’ Hunusa harufu ya vita toka mbali, sauti ya mtoa amri na ukelele wa vita.
26 ¿Vuela el halcón y extiende sus alas hacia el sur por tu sabiduría?
“Je, mwewe huruka kwa hekima yako na kuyakunjua mabawa yake kuelekea kusini?
27 ¿Por tu mandato se remonta el águila y pone su nido en la altura?
Je, tai hupaa juu kwa amri yako na kujenga kiota chake mahali pa juu?
28 Vive y tiene su habitación en la roca, en la cumbre del peñasco, en lugar inaccesible.
Huishi juu ya miamba mirefu na kukaa huko usiku; majabali yenye ncha kali ndiyo ngome yake.
29 Desde allí acecha la presa. Sus ojos la divisan desde muy lejos.
Kutoka huko hutafuta chakula chake; macho yake hukiona kutoka mbali.
30 Sus polluelos chupan la sangre. Donde hay carroña, allí está ella.
Makinda yake hujilisha damu, na pale palipo na machinjo, ndipo yeye alipo.”