< Job 33 >
1 Sin embargo, Job, escucha ahora mis razones y atiende todas mis palabras.
“Lakini Ayubu, sasa, sikiliza maneno yangu; zingatia kila kitu nitakachosema.
2 Ciertamente ahora abro mi boca. Mi lengua habla en mi paladar.
Karibu nitafungua kinywa changu; maneno yangu yapo katika ncha ya ulimi wangu.
3 Mis palabras declararán la rectitud de mi corazón y lo que saben mis labios lo dicen con sinceridad:
Maneno yangu yanatoka katika moyo mnyofu; midomo yangu hunena kwa uaminifu yale niyajuayo.
4 El Espíritu de ʼElohim me hizo y el soplo de ʼEL-Shadday me dio vida.
Roho wa Mungu ameniumba; pumzi ya Mwenyezi hunipa uhai.
5 Respóndeme si puedes. Alístate y ponte en pie ante mí.
Unijibu basi, kama unaweza; jiandae kunikabili mimi.
6 Ciertamente pertenezco a ʼEL, como tú. Del barro también fui formado.
Mimi ni kama wewe mbele za Mungu; mimi pia nimetolewa kwenye udongo.
7 Ciertamente mi terror no te espantará, ni mi mano será demasiado pesada sobre ti.
Huna sababu ya kuniogopa, wala mkono wangu haupaswi kukulemea.
8 En verdad tú dijiste a oídos míos. Yo oí el sonido de tus palabras:
“Lakini umesema nikiwa ninakusikia, nami nilisikia maneno yenyewe:
9 Limpio soy, sin transgresión. Soy inocente y no hay culpa en mí.
‘Mimi ni safi na sina dhambi; mimi ni safi na sina hatia.
10 Ciertamente Él inventa pretextos contra mí y me considera su enemigo.
Lakini bado Mungu amepata dosari kwangu, naye ananiona kama adui yake.
11 Puso mis pies en el cepo y vigila todos mis pasos.
Ananifunga miguu kwa pingu, tena anaziangalia njia zangu zote kwa karibu.’
12 Ciertamente yo te respondo: En esto no eres justo, porque ʼElohim es mayor que el hombre.
“Lakini mimi ninakuambia, katika jambo hili wewe una makosa, kwa maana Mungu ni mkuu kuliko mwanadamu.
13 ¿Por qué contiendes con ʼEL? Pues Él no da cuenta de ninguna de sus obras.
Kwa nini unamlalamikia kwamba yeye hamjibu mwanadamu?
14 Porque ʼElohim habla de una manera o de otra, pero nadie lo percibe:
Kwa kuwa Mungu husema, wakati huu kwa njia moja, au wakati mwingine kwa njia nyingine, ingawa mwanadamu anaweza asielewe.
15 En sueño, en visión nocturna, cuando el sopor cae sobre los hombres, mientras se adormecen en la cama,
Mungu husema na mwanadamu katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito uwaangukiapo wanadamu wasinziapo vitandani mwao,
16 Él abre el oído de los hombres y sella su instrucción para ellos,
anaweza akasemea masikioni mwao, na kuwatia hofu kwa maonyo,
17 a fin de apartar al hombre de su obra y destruir la soberbia del varón,
ili kumgeuza mtu kutoka kwenye kutenda mabaya na kumwepusha na kiburi,
18 para librar su alma del sepulcro y que su vida no perezca a filo de espada.
kuiokoa nafsi yake na shimo, uhai wake usiangamizwe kwa upanga.
19 También sobre su cama es reprendido con dolores, con el dolor incesante de sus huesos,
Mtu anaweza kutiwa adabu kwa maumivu kitandani mwake, kwa dhiki za mfululizo katika mifupa yake,
20 lo cual hace que le repugne el pan, y aun el manjar más delicado.
kiasi kwamba maisha yake yenyewe yanakataa chakula nayo nafsi yake ikakichukia kabisa hata chakula kizuri.
21 Su carne se consume hasta que no se ve, y sus huesos, que no se veían, aparecen.
Nyama ya mwili wake huisha kwa kukonda, nayo mifupa yake ambayo mwanzoni ilikuwa imefichika, sasa inatokeza nje.
22 Su alma se acerca al sepulcro y su vida a los que causan la muerte.
Nafsi yake inakaribia kaburi, nao uhai wake karibu na wajumbe wa kifo.
23 Si hay un ángel que sea mediador para él, muy escogido entre 1.000, que recuerda al hombre lo correcto para él,
“Kama bado kuna malaika upande wake kama mtetezi, mmoja miongoni mwa elfu, wa kumwambia mwanadamu lililo jema kwake,
24 tenga compasión de él y diga: Líbrenlo de bajar al sepulcro, pues le hallé un rescate.
kumwonea huruma na kusema, ‘Mwokoe asije akatumbukia shimoni; nimepata ukombozi kwa ajili yake’:
25 Entonces su carne sería más tierna que la de un joven que vuelve al vigor de los días de su juventud.
ndipo nyama ya mwili wake hufanywa mpya kama ya mtoto; hurudishwa upya kama siku za ujana wake.
26 Invocaría a ʼEloha. Él le haría sacrificio que apacigua, para que vea el semblante de ʼEL con gozo y Él le restaure su justicia al hombre.
Humwomba Mungu, akapata kibali kwake, huuona uso wa Mungu na kushangilia kwa furaha; Mungu humrudisha katika hali yake ya uadilifu.
27 Él mira a los hombres y al que dice: Pequé y pervertí lo recto, pero nada me aprovechó,
Ndipo huja mbele za watu na kusema, ‘Nilitenda dhambi na kupotosha kilichokuwa haki, lakini sikuadhibiwa kama nilivyostahili.
28 Él le redimirá su alma para que no baje al sepulcro, y su vida verá la luz.
Alinikomboa nafsi yangu nisitumbukie shimoni, nami nitaishi ili kuufurahia mwanga.’
29 En verdad ʼEL hace todas estas cosas con el hombre dos veces, y aun tres,
“Mungu hufanya haya yote kwa mwanadamu; mara mbili hata mara tatu,
30 para rescatar su alma del sepulcro e iluminarlo con la luz de la vida.
ili aigeuze nafsi yake toka shimoni, ili nuru ya uzima imwangazie.
31 Presta atención, Job, escúchame. Calla, y permíteme hablar.
“Ayubu, zingatia, nisikilize mimi; nyamaza, nami nitanena.
32 Si tienes palabras, respóndeme. Habla, porque yo quiero declararte justo.
Kama unalo lolote la kusema, unijibu; sema, kwa maana ninataka uonekane huna hatia.
33 Si no, escúchame. Calla, y yo te enseñaré sabiduría.
Lakini kama huna la kusema, basi nisikilize mimi; nyamaza, nami nitakufundisha hekima.”