< Job 15 >

1 Elifaz temanita respondió:
Ndipo Elifazi Mtemani alijibu na kusema,
2 ¿Responderá el sabio con conocimiento vano? ¿Llenará su vientre de viento del este?
Mtu mwenye hekima anapaswa kujibu kwa maarifa yasiyofaa na kujijaza mwenyewe na upepo wa mashariki?
3 ¿Argüirá con palabras inútiles o con palabras sin provecho?
Anapaswa kuhojiana na mazungumzo yasiyo na faida au na hotuba ambazo kwa hizo yeye hawezi kufanya mema?
4 Tú anulas la reverencia y menosprecias la oración ante ʼElohim,
Dhahiri, wewe wafifisha heshima ya Mungu; Wewe wazuia heshima kwa yeye,
5 porque tu iniquidad enseña tu boca, y adoptas la lengua del astuto.
kwa maana uovu wako hufundisha midomo yako; Wewe wachagua kuwa na ulimi wa mtu mwenye hila.
6 Tu boca te condena, y no yo. Tus labios testifican contra ti.
Mdomo wako mwenyewe hukukukumu wewe, siyo wangu; hakika, midomo yako mwenyewe hushuhudia dhidi yako wewe.
7 ¿Eres tú el primer hombre que nació? ¿Fuiste engendrado antes que las montañas?
Je, wewe ni mwanadamu wa kwanza ambaye aliyezaliwa? Wewe ulikuwepo kabla ya vilima kuwepo?
8 ¿Escuchaste el secreto de ʼElohim para que tú solo te apropies de la sabiduría?
Wewe Umewahi kusikia maarifa ya siri ya Mungu? Je, wewe wajihesabia mwenye hekima wewe mwenyewe?
9 ¿Qué sabes que nosotros no sepamos? ¿Qué entiendes que nosotros no entendamos?
Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho sisi hatukijui? Ni kitu gani unachokifahamu wewe ambacho hakiko katika sisi?
10 Cabezas canas y hombres muy ancianos, de más larga edad que tu padre, hay entre nosotros.
Pamoja nasi wapo pia wenye mvi na watu wazee sana ambao ni wazee zaidi kuliko baba yako.
11 ¿En tan poco tienes el consuelo de ʼElohim y la palabra que se te dice con dulzura?
Je, faraja ya Mungu ni ndogo sana kwako, maneno ambayo ni ya upole dhidi yako wewe?
12 ¿Por qué tu corazón te arrastra y por qué guiñan tus ojos?
Kwa nini moyo wako wewe unakupeleka mbali? Kwa nini macho yako yananga'ra,
13 ¿Por qué vuelves tu espíritu contra ʼElohim, y dejas salir esas palabras de tu boca?
ili ya kwamba kuirejesha roho yako kwa Mungu na kuyatoa maneno hayo kutoka katika mdomo wako?
14 ¿Qué es el hombre para que sea considerado puro, y el nacido de mujer para que sea considerado justo?
Je, mwanadamu yeye ni nini kwamba yeye anapaswa kuwa safi? Yeye mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke ni nini kwamba yeye anapaswa awe mwenye haki?
15 Mira, en sus santos no confía. Ante sus ojos ni aun el cielo es puro.
Tazama, Mungu haweki tumaini lake hata kwa mmoja wake aliye mtakatifu; Hakika, mbingu haziko safi machoni pake yeye;
16 ¡Cuánto menos el hombre repugnante y corrupto que bebe la iniquidad como agua!
jinsi gani asivyo safi ni mmoja aliye mbaya na mla rushwa, mtu ambaye hunywa uovu kama maji!
17 Escúchame, yo te informaré. Óyeme y lo que vi te contaré
Mimi nitakuonyesha wewe; Nisikilize mimi; Mimi nitakutangazia wewe vitu ambavyo nimeviona,
18 lo que los sabios informaron, sin ocultar lo de sus antepasados.
vitu ambavyo watu wenye hekima wamepita chini yake kutoka kwa baba zao, vile vitu ambavyo mababu zao hawakuvificha.
19 Solo a ellos fue dada la tierra, y ningún extraño pasó entre ellos.
Hawa walikuwa mababu zao, ambao kwao pekee nchi walipewa, na miongoni mwao hakuna mgeni aliyepita.
20 Todos sus días sufre tormento el perverso, y contados años le están reservados al tirano.
Mtu mwovu hupitia katika maumivu siku zake zote, idadi ya miaka iliyowekwa juu kwa mtesaji kuteseka.
21 Voces espantosas resuenan en sus oídos. El destructor vendrá sobre él en la paz.
Sauti ya vitisho katika masikio yake; pindi yeye yuko katika kufanikiwa, mharibu atakuja juu yake yeye.
22 No cree que volverá de la oscuridad. Está destinado para la espada.
Yeye hafikiri kwamba yeye atarudi kutoka katika giza; Upanga humngojea yeye.
23 Vaga en busca del pan y dice: ¿Dónde está? Sabe que el día de la oscuridad está cerca.
Yeye huenda sehemu mbali mbali kwa ajili ya mkate, akisema, 'Kiko wapi? ' Yeye anatambua kuwa siku ya giza iko mkononi.
24 La tristeza y la aflicción lo turban, como un rey listo para la batalla,
Dhiki na mateso makali humfanya aogope; wao hushinda dhidi yake yeye, kama mfalme tayari kwa vita.
25 porque extendió su mano contra ʼEL. Se portó con soberbia contra ʼEL-Shadday.
Kwa sababu yeye ameunyosha mkono wake dhidi ya Mungu na ameishi kwa kiburi dhidi ya aliye mkuu,
26 Indómito embistió contra Él con la espesa barrera de su escudo,
huyu mtu mwovu hukimbia kwa Mungu na shingo ngumu, kwa vifundo vikubwa vya ngao.
27 con su cara cubierta, con los pliegues de su cintura aumentados de grasa.
Hii ni kweli, hata ingawa yeye amefunika uso wake kwa mafuta yake na amekusanya mafuta juu ya viuno vyake,
28 Vivirá en ciudades destruidas, en casas no habitadas, destinadas a ser ruinas.
na ameishi katika miji yenye ukiwa; katika nyumba ambazo hakuna mwanadamu anayeishi humo sasa na ambazo zilikuwa tayari kuwa magofu.
29 No enriquecerá, ni durará su hacienda, ni se extenderán sus posesiones en la tierra.
Yeye hatakuwa tajiri; utajiri wake yeye hautadumu; hata kivuli chake hakitadumu katika nchi.
30 No escapará de la oscuridad. La llama consumirá sus ramas. Por el aliento de su boca perecerá.
Yeye hatatoka nje ya giza; mwali wa moto utakausha matawi yake; katika pumzi ya kinywa cha Mungu yeye ataenda zake.
31 No confíe en la vanidad, ni se engañe a sí mismo, porque la vanidad será su recompensa.
Mwacheni yeye asitumaini katika vitu visivyofanya kazi, akijidanganya yeye mwenyewe; maana upuuzi utakuwa mshahara wake yeye.
32 Se marchitará antes de su tiempo, y sus ramas no reverdecerán.
Itatokea kabla ya wakati wake yeye atapaswa kufa; tawi lake halitakuwa kijani.
33 Será vid que dejará caer sus uvas no maduras, olivo que echa de él sus flores.
Yeye atazipukutisha zabibu zake zisizovunwa kama mzabibu; yeye atayaondoa maua yake kama mti wa mzeituni.
34 La compañía del impío es estéril, y el fuego consume las tiendas del corrupto.
Kwa maana msaada wa watu wasiomcha Mungu utakuwa tasa; moto utateketeza hema za rushwa.
35 Conciben travesura, dan a luz iniquidad y su mente prepara el engaño.
Wao wanabeba mimba yenye ubaya na kuzaa uovu; tumbo lao hutunga mimba ya udanganifu.

< Job 15 >