< Job 14 >

1 El hombre nacido de mujer es corto de días y lleno de perturbaciones.
“Mwanadamu aliyezaliwa na mwanamke siku zake ni chache nazo zimejaa taabu.
2 Brota como una flor, pero es cortado. Pasa como una sombra y desaparece.
Huchanua kama ua kisha hunyauka; huwa kama kivuli kipitacho upesi, wala hadumu.
3 ¿Y sobre éste abres tus ojos y lo llevas a juicio contigo?
Je, unamwekea jicho lako mtu kama huyo? Je, utamleta mbele yako katika hukumu?
4 ¿Quién limpiará lo impuro? ¡Nadie!
Ni nani awezaye kutoa kitu safi kutoka kitu najisi? Hakuna awezaye!
5 Ciertamente sus días están determinados, y el número de sus meses depende de Ti. Tú le fijaste sus límites, de los cuales no pasará.
Siku za mwanadamu zimewekewa mpaka; umekwisha kutangaza idadi ya miezi yake na kuweka mpaka ambao hawezi kuuvuka.
6 Aparta de él tu mirada y que descanse hasta que complete su día como un jornalero.
Hivyo angalia mbali umwache, hadi awe amekamilisha muda wake kama mtu aliyeajiriwa.
7 Porque para el árbol hay esperanza: Si es cortado, retoñará, y sus ramas no cesarán.
“Kwa maana lipo tumaini kwa mti; kama ukikatwa utachipuka tena, nayo machipukizi yake mapya hayatakoma.
8 Aunque debajo de la tierra esté muerto su tronco, y en la tierra envejezca su raíz,
Mizizi yake yaweza kuchakaa ardhini na kisiki chake kufa udongoni,
9 al recibir el agua reverdecerá, y echará ramas como una planta.
lakini kwa kupata dalili ya maji utachipua na kutoa machipukizi kama mche.
10 Pero el hombre muere, y queda tendido. Expira el hombre, ¿y dónde está?
Lakini mwanadamu hufa, na huo ndio mwisho wake; hutoa pumzi ya mwisho, naye hayuko tena!
11 Como las aguas se van al mar, y un río se agota y se seca,
Kama vile maji yatowekavyo katika bahari, au mkondo wa mto ukaushwavyo na kuwa mkavu,
12 así el hombre queda tendido y no se levantará. Hasta que no haya cielo, no será despertado, ni lo levantarán de su sueño.
ndivyo mwanadamu alalavyo chini asiamke; hadi mbingu zitakapokuwa hazipo tena, wanadamu hawataamka au kuamshwa kutoka kwenye usingizi wao.
13 ¡Ojalá me escondas en el Seol mientras se aplaca tu ira, y me fijes un plazo y te acuerdes de mí! (Sheol h7585)
“Laiti kama ungenificha kaburini, na kunisitiri hadi hasira yako ipite! Laiti ungeniwekea wakati, na kisha ukanikumbuka! (Sheol h7585)
14 Si el hombre muere, ¿volverá a vivir? Todos los días de mi lucha y servicio esperaré hasta que llegue mi liberación.
Je, kama mtu akifa, aweza kuishi tena? Siku zote za kazi zangu ngumu nitangojea kufanywa upya kwangu.
15 Entonces llamarás y yo te responderé. Tendrás afecto a la hechura de tus manos.
Utaniita nami nitakuitika; utakionea shauku kiumbe ambacho mikono yako ilikiumba.
16 Porque ahora me cuentas los pasos y no das tregua a mi pecado.
Hakika ndipo utakapozihesabu hatua zangu, lakini hutazifuatia dhambi zangu.
17 Tienes mi transgresión sellada en un saco. Tú cubres mi iniquidad.
Makosa yangu yatafungiwa kwa lakiri kwenye mfuko, nawe utazifunika dhambi zangu.
18 Pero la montaña cae y se desmorona. Las rocas cambian de lugar.
“Lakini kama mlima umomonyokavyo na kufikichika na kama vile mwamba uondolewavyo mahali pake,
19 Las piedras se desgastan con el agua impetuosa que se lleva el polvo de la tierra. Así destruyes la esperanza del hombre.
kama maji yamalizavyo mawe, na mafuriko yachukuavyo udongo, ndivyo unavyoharibu tegemeo la mwanadamu.
20 Prevaleces para siempre contra él, y él se va. Desfiguras su rostro y lo despides.
Humshinda mara moja kwa daima, naye hutoweka; waibadilisha sura yake na kumwondoa.
21 Sus hijos obtendrán honores, pero él no lo sabrá. Si son humillados, no lo percibirá.
Kama wanawe wakipewa heshima, yeye hafahamu; kama wakidharauliwa, yeye haoni.
22 Pero su carne sobre él siente el tormento, y su alma gime por él.
Yeye hasikii kingine isipokuwa maumivu ya mwili wake mwenyewe, naye huomboleza kwa ajili yake mwenyewe.”

< Job 14 >