< Job 12 >
Ndipo Ayubu akajibu na kusema,
2 Entonces ciertamente ustedes son el pueblo, y con ustedes se acaba la sabiduría.
“Hakuna shaka ninyi wanadamu; Hekima mtakufa nayo.
3 Pero yo tengo entendimiento como ustedes. No soy menos que ustedes. ¿Quién no sabe tales cosas?
Lakini nina ufahamu kama vile ninyi; Mimi siyo duni kwenu. Ni dhhiri, ni nani asiyefahamu vitu hivyo kama hivi?
4 Yo soy alguien que para su amigo es motivo de risa, uno que clamó a ʼElohim y le respondió. ¡El justo e intachable es un payaso!
Mimi ni kitu cha kuchekwa na jirani-Mimi, ni mmoja aliyemwita Mungu na ambaye alijibiwa na yeye! Mimi, ni mwenye haki na mtu asiyekuwa na hatia-Mimi sasa nimekuwa kitu cha kuchekwa.
5 El que tiene bienestar desprecia la calamidad como algo preparado para aquellos que resbalan.
Katika mawazo yake mtu fulani aliye katika kufurahi, kuna kudharau kwa mashaka; hufikiri katika njia ambayo huleta mambo mabaya zaidi kwa wale ambao miguu yao inateleza.
6 Prosperan las tiendas de los ladrones y los que provocan a ʼEL están seguros, aquellos que ʼEloah trae a su poder.
Hema za wezi hufanikiwa, na wale ambao humkasirisha Mungu huhisi salama; mikono yao wenyewe ni miungu wao.
7 En efecto, pregunta ahora a las bestias, y ellas te enseñarán, a las aves del cielo, y ellas te lo dirán.
Lakini sasa waulize hao wanyama wa mwituni, na watakufundisha wewe; waulize ndege wa angani, na watakuambia wewe.
8 O habla a la tierra, y te enseñará. Los peces del mar también te lo declararán.
Au iambie ardhi, na itakufundisha wewe; samaki wa baharini watakutangazia wewe.
9 ¿Cuál de ellos no sabe que la mano de Yavé hizo esto,
Ni myama yupi miongoni mwa hawa asiyefahamu kuwa mkono wa Yahwe umetenda haya?
10 que en su mano está la vida de todo viviente y el hálito de toda la humanidad?
Katika mkono wake mna uzima wa kila kiumbe hai na pumzi ya wanadamu wote.
11 ¿No distingue el oído las palabras y el paladar prueba la comida?
Je, sikio haliyajaribu maneno kama vile kaakaa lionjavyo chakula chake?
12 En los ancianos está la sabiduría y en la larga edad el entendimiento.
Kwa wazee mna hekima; katika wingi wa siku mna ufahamu.
13 Con Él están la sabiduría y el poder. Suyos son el consejo y el entendimiento.
Pamoja na Mungu mna hekima na ukuu; yeye anayo mashauri na ufahamu.
14 Si Él derriba, no será reedificado. Si Él encierra al hombre, no hay liberación.
Tazama, yeye huangusha chini, na haiwezekani kujengwa tena; kama yeye akimtia gerezani mtu yeyote, hakutakuwa tena kufunguliwa.
15 Si Él retiene las aguas, se secan, y si las suelta, inundan la tierra.
Tazama, kama yeye akiyazuia maji, yanakauka; na kama akiyaachilia nje yanaitaabisha ardhi.
16 Con Él están la fortaleza y la sana sabiduría. Suyos son el que yerra y el que hace errar.
Pamoja na yeye mna nguvu na hekima; watu ambao wamedanganywa na mdanganyi wote pamoja wako katika nguvu zake.
17 Hace andar descalzos a los consejeros y entontece a los jueces.
Yeye huwaongoza washauri mbali bila kuvaa viatu katika huzuni; huwarudisha hakimu katika upumbavu.
18 Suelta las ataduras que imponen los reyes y ata con una cuerda sus cinturas.
Yeye Huondoa minyororo ya mamlaka kutoka kwa wafalme; yeye hufunika viuno vyao kwa nguo.
19 Hace ir descalzos a los sacerdotes y derriba a los poderosos.
Yeye huwaongoza makuhani mbali bila kuvaa viatu na kuwapindua watu wakuu.
20 Priva del habla a los de confianza, y del discernimiento a los ancianos.
Yeye huondoa hotuba ya wale waliokuwa wameaminiwa na huondoa mbali ufahamu wa wazee.
21 Derrama desprecio sobre los nobles y afloja el cinturón de los fuertes.
Yeye humwaga aibu juu ya binti za wafalme na hufungua mishipi ya watu wenye nguvu.
22 Descubre las profundidades de la oscuridad y saca a la luz la sombra de muerte.
Yeye huweka wazi vitu vya kina kutoka katika giza na kuvileta nje kumuika vivuli mahali ambapa watu waliokufa wapo.
23 Engrandece las naciones y las destruye. Ensancha los pueblos y los suprime.
Yeye huyafanya mataifa kuwa na nguvu, na pia huyaharibu; Yeye pia huyakuza mataifa, na pia yeye huyaongoza mbali kama wafungwa.
24 Priva de discreción a los caudillos de los pueblos de la tierra y los hace deambular por un desierto sin camino.
Yeye huondoa mbali ufahamu kutoka kwa viongozi wa watu wa nchi; huwafanya wao kutangatanga msituni mahali pasipo na njia.
25 No tienen luz. Palpan en la oscuridad, y los hace tambalearse como ebrios.
Wao wanapapasa katika giza bila kuwa na mwanga; yeye huwafanya wao kuweweseka kama mtu mlevi.