< Job 10 >
1 ¡Mi alma está hastiada de mi vida! Daré rienda suelta a mi queja. Hablaré con la amargura de mi alma.
Nimechoka na maisha yangu; Nitanena wazi manung'uniko yangu; nitasema kwa uchungu wa roho yangu.
2 Diré a ʼElohim: ¡No me condenes! Hazme saber por qué contiendes conmigo.
Nitamwambia Mungu, 'Usinihukumie makosa; nionyeshe sababu za wewe kunilaumu mimi. Je
3 ¿En verdad, es justo para Ti oprimir, desechar la obra de tus manos y favorecer el designio de los perversos?
ni vizuri kwako wewe kunionea mimi, kudharau kazi ya mikono yako wakati unafurahia juu ya mipango ya waovu?
4 ¿Tienes ojos humanos y miras como mira el hombre?
Je wewe una macho ya kimwili? Je wewe unaona kama mtu aonavyo?
5 ¿Son tus días como los días del hombre o tus años como los años del hombre,
Je siku zako ni kama siku za wanadamu au miaka yako ni kama miaka ya watu,
6 para que indagues mi iniquidad e investigues mi pecado?
hata ukauliza habari za uovu wangu na kuitafuta dhambi yangu,
7 Tú sabes que no soy culpable, y que no hay quien libre de tu mano.
ingawa wewe wafahamu mimi sina kosa na hapana mwingine awezaye kuniokoa mimi na mkono wako?
8 Tus manos me hicieron y me formaron. ¿Y ahora me destruyes?
Mikono yako imeniumba na kunifinyanga kwa wakati mmoja nawe kunizunguka, hata hivyo unaniangamiza.
9 Recuerda, te ruego, que del barro me moldeaste. ¿Y al polvo me harás volver?
Kumbuka, nakuomba, ulivyonifinyanga kama vile udongo; je utanirudisha mavumbini tena?
10 ¿No me vertiste como leche y me cuajaste como queso?
Je wewe hukunimimina kama maziwa na kunigandisha mfano wa jibini?
11 Me cubriste de piel y de carne, con huesos y tendones me tejiste.
Umenivika ngozi na nyama na kuniunganisha pamoja kwa mifupa na misuli.
12 Me otorgaste vida y misericordia, y tu cuidado preservó mi espíritu.
Wewe umenizawadia mimi uhai na ahadi ya upendeleo na usaidizi wako umeilinda roho yangu.
13 Tenías estas cosas ocultas en tu corazón. Yo sé que esto estaba contigo.
Hata hivyo mambo haya uliyaficha moyoni mwako - nafahamu kwamba hivi ndivyo ufikirivyo:
14 Si peco, Tú me observas, y no me tendrás como limpio de mi culpa.
kuwa kama nimefanya dhambi, wewe utaizingatia; hutaniachilia na uovu wangu.
15 Si soy malo, ¡ay de mí! Y si soy justo, no levantaré mi cabeza. Estoy hastiado de la afrenta y de ver mi aflicción.
Kama mimi ni muovu, ole wangu; hata kama ni mwenye haki, sitaweza kuinua kichwa changu, kwa kuwa nimejaa aibu na kuyaangalia mateso yangu.
16 Si mi cabeza se levanta, me cazas como a león y vuelves a mostrar tus proezas en mí.
Kama kichwa changu kikijiinua chenyewe, waniwinda kama simba; tena wajionyesha mwenyewe kuwa ni mwenye nguvu kwangu.
17 Renuevas tus testigos contra mí y aumentas contra mí tu furor como tropas de relevo.
Wewe unaleta mashahidi wapya dhidi yangu na kuzidisha hasira zako dhidi yangu; wanishambulia na majeshi mapya.
18 ¿Por qué entonces me sacaste de la matriz? ¡Hubiera yo expirado sin que ningún ojo me viera!
Kwa nini, basi, ulinitoa tumboni? Natamani ningekata roho na ili jicho lolote lisinione.
19 Sería como si nunca hubiera existido, llevado del vientre a la tumba.
Ningelikuwa kama asiyekuwepo; ningelichukuliwa kutoka tumboni mpaka kaburini.
20 ¿No son pocos mis días? Cesa pues, y déjame, para que me consuele un poco
Je si siku zangu pekee ni chache? Acha basi, usinisumbue, ili kwamba nipate kupumzika kidogo
21 antes que me vaya a la región tenebrosa de la muerte para no volver,
kabla sijaenda huko ambako sitarudi, kwenye nchi ya giza na kivuli cha mauti,
22 tierra de oscuridad, lóbrega, lugar de sombra de muerte, sin orden, donde la luz es como densa oscuridad.
ni nchi ya giza kama usiku wa manane, nchi ya kivuli cha mauti, isiyokuwa na mpangilio, ambayo nuru yake ni kama usiku wa manane.'”