< Hebreos 13 >

1 Permanezca el amor fraternal.
Endeleeni kupendana kama ndugu.
2 No olviden la hospitalidad, porque por medio de ésta algunos hospedaron ángeles sin saberlo.
Msisahau kuwakaribisha wageni, kwa kuwa kwa kufanya hivyo, watu wengine waliwakaribisha malaika pasipo kujua.
3 Acuérdense de los presos, como presos juntamente con ellos, y de los maltratados, por que también ustedes están en el cuerpo.
Wakumbukeni wale waliofungwa gerezani kana kwamba ninyi mmefungwa pamoja nao. Pia wakumbukeni wale wanaotendewa vibaya, kana kwamba ni ninyi wenyewe mnateswa.
4 Honroso sea el matrimonio en todos y el lecho conyugal sin mancha, porque Dios juzgará también a los inmorales sexuales y adúlteros.
Ndoa na iheshimiwe na watu wote, nayo malazi yawe safi, kwa kuwa Mungu atawahukumu wazinzi na waasherati wote.
5 Sean sus costumbres sin avaricia. Estén satisfechos con lo que tienen, porque Él mismo dijo: Que de ningún modo te abandone. Que de ningún modo te desampare.
Yalindeni maisha yenu msiwe na tabia ya kupenda fedha, bali mridhike na vile mlivyo navyo, kwa sababu Mungu amesema, “Kamwe sitakuacha, wala sitakupungukia.”
6 De manera que decimos confiadamente: [El] Señor es mi Ayudador, no temeré. ¿Qué podrá hacerme un ser humano?
Kwa hiyo tunaweza kusema kwa ujasiri, “Bwana ni msaada wangu; sitaogopa. Mwanadamu anaweza kunitenda nini?”
7 Acuérdense de sus líderes, quienes les hablaron la Palabra de Dios. Cuando consideren cuál fue el resultado de su conducta, imiten su fe.
Wakumbukeni viongozi wenu, wale waliowaambia neno la Mungu. Angalieni matokeo ya mwenendo wa maisha yao mkaiige imani yao.
8 Jesucristo es el mismo ayer, hoy y por los siglos. (aiōn g165)
Yesu Kristo ni yeye yule jana, leo na hata milele. (aiōn g165)
9 No sean llevados por enseñanzas diversas y extrañas, pues es bueno fortalecer el corazón en la gracia, no con comidas que en nada beneficiaron.
Msichukuliwe na kila aina ya mafundisho ya kigeni. Ni vyema mioyo yenu iimarishwe kwa neema, wala si kwa sheria kuhusu utaratibu wa vyakula, ambavyo havina faida kwa wale wanaozishika hizo sheria.
10 Tenemos un altar del cual los que sirven al Tabernáculo no tienen derecho de comer,
Sisi tunayo madhabahu ambayo wale wanaohudumu katika hema hawana haki ya kula vile vitu vilivyowekwa juu yake.
11 porque estos cuerpos de animales, cuya sangre el sumo sacerdote lleva al Santuario como ofrenda por [el] pecado, son quemados fuera del campamento.
Kuhani mkuu huchukua damu ya wanyama na kuiingiza Patakatifu pa Patakatifu, kama sadaka ya dhambi, lakini miili ya hao wanyama huteketezwa nje ya kambi.
12 Por lo cual también Jesús padeció fuera de la puerta para santificar al pueblo por medio de su propia sangre.
Vivyo hivyo, Yesu naye aliteswa nje ya lango la mji ili awatakase watu kwa damu yake mwenyewe.
13 Así que salgamos a Él fuera del campamento y llevemos su reproche.
Kwa hiyo, basi na tumwendee nje ya kambi, tukiichukua aibu aliyobeba.
14 Porque no tenemos aquí una ciudad permanente, sino buscamos la que viene.
Kwa kuwa hapa hatuna mji udumuo, bali tunautafuta ule ujao.
15 Por medio de Él ofrezcamos siempre a Dios sacrificio de alabanza, es decir, fruto de labios que confiesen su Nombre.
Basi kwa njia ya Yesu, tuzidi kumtolea Mungu dhabihu ya sifa, yaani matunda ya midomo inayolikiri Jina lake.
16 No se olviden de hacer bien y de ser generosos, porque a Dios le agradan estos sacrificios.
Na msiache kutenda mema na kushirikiana vile vitu mlivyo navyo, kwa kuwa dhabihu kama hizo ndizo zinazompendeza Mungu.
17 Obedezcan a sus líderes y sujétense a ellos, porque ellos velan por sus almas y darán cuenta a Dios por ustedes, a fin de que lo hagan con gozo, sin queja, porque esto no es provechoso.
Watiini viongozi wenu na kujinyenyekeza chini ya mamlaka yao. Kwa maana wao wanakesha kwa ajili yenu kama watu watakaopaswa kutoa hesabu. Watiini ili wafanye kazi yao kwa furaha, wala si kama mzigo, maana hiyo haitakuwa na faida kwenu.
18 Hablen con Dios por nosotros, pues confiamos en que tenemos buena conciencia, y deseamos conducirnos bien en todo.
Tuombeeni. Tuna hakika kuwa tunayo dhamiri safi na shauku ya kuishi kwa uadilifu kwa kila njia.
19 Ruego que hagan esto mucho más, a fin de que pronto [yo] sea restituido para ustedes.
Ninawasihi zaidi mniombee ili nipate kurudishwa kwenu upesi.
20 El Dios de paz, Quien resucitó de entre [los] muertos a nuestro Señor Jesús, el excelente Pastor de las ovejas, por [la] sangre del Pacto eterno, (aiōnios g166)
Basi Mungu wa amani, ambaye kwa damu ya Agano la milele alimleta tena kutoka kwa wafu Bwana wetu Yesu, yule Mchungaji Mkuu wa kondoo, (aiōnios g166)
21 los haga completos en todo lo bueno para que hagan la voluntad de Él, y [Él] haga en ustedes lo agradable delante de Él por medio de Jesucristo, a Quien sea la gloria por los siglos. Amén. (aiōn g165)
awafanye ninyi wakamilifu mkiwa mmekamilishwa katika kila jambo jema ili mpate kutenda mapenzi yake, naye atende ndani yetu kile kinachompendeza machoni Pake, kwa njia ya Yesu Kristo, ambaye utukufu una yeye milele na milele. Amen. (aiōn g165)
22 Les ruego, hermanos, que soporten esta Palabra de exhortación, porque les escribí brevemente.
Ndugu zangu, nawasihi mchukuliane na maneno yangu ya maonyo, kwa kuwa nimewaandikia waraka mfupi tu.
23 Sepan que nuestro hermano Timoteo fue liberado. Si viene pronto, iremos a visitarlos.
Nataka ninyi mjue kwamba ndugu yetu Timotheo amefunguliwa kutoka gerezani. Akifika mapema, nitakuja pamoja naye kuwaona.
24 Saluden a todos los que los dirigen y a todos los santos. Los de Italia los saludan.
Wasalimuni viongozi wenu wote na watakatifu wote. Wale wa kutoka Italia wanawasalimu.
25 La gracia sea con todos ustedes.
Neema iwe nanyi nyote. Amen.

< Hebreos 13 >