< Génesis 14 >
1 Aconteció en los días de Amrafel, rey de Sinar, Arioc, rey de Elasar, Quedorlaomer, rey de Elam, y Tidal, rey de los Goyim,
Wakati huu Amrafeli mfalme wa Shinari, Arioko mfalme wa Elasari, Kedorlaoma mfalme wa Elamu, na Tidali mfalme wa Goimu
2 que estos reyes hicieron guerra contra Bera, rey de Sodoma, Birsa, rey de Gomorra, Sinab, rey de Adma, Semeber, rey de Zeboim, y contra el rey de Bela, la cual es Zoar.
kwa pamoja walikwenda kupigana vita dhidi ya Bera mfalme wa Sodoma, Birsha mfalme wa Gomora, Shinabu mfalme wa Adma, Shemeberi mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari).
3 Todos estos se unieron en el valle de Sidim, que es el mar Salado.
Hawa wote waliotajwa mwishoni waliunganisha majeshi yao kutoka Bonde la Sidimu (yaani Bahari ya Chumvi).
4 Habían servido a Quedorlaomer 12 años, pero el año 13 se rebelaron.
Walikuwa wametawaliwa na Mfalme Kedorlaoma kwa miaka kumi na miwili, lakini mwaka wa kumi na tatu waliasi.
5 El año 14 Quedorlaomer y los reyes que estaban con él llegaron y derrotaron a los refaítas en Astarot-carnaim, a los zuzitas en Ham, a los emitas en Save-quiriataim
Mnamo mwaka wa kumi na nne, Mfalme Kedorlaoma na wafalme waliojiunga naye walikwenda kupigana na kuwashinda Warefai katika Ashtaroth-Kanaimu, Wazuzi katika Hamu, Waemi katika Shawe-Kiriathaimu,
6 y a los hurritas en las montañas de Seír hasta El-parán, que está junto al desierto.
na Wahori katika nchi ya kilima cha Seiri, hadi El-Parani karibu na jangwa.
7 Luego se volvieron a En-mispat, o Cades. Arrasaron todo el territorio del amalecita y también el del amorreo, que habitaba en Hazezón-tamar.
Kisha wakarudi wakaenda En-Misfati (yaani Kadeshi), wakashinda nchi yote ya Waamaleki, pamoja na Waamori waliokuwa wakiishi Hasason-Tamari.
8 Entonces salieron los reyes de Sodoma, Gomorra, Adma, Zeboim y de Bela, la cual es Zoar. Dispusieron batalla contra ellos en el valle de Sidim,
Ndipo mfalme wa Sodoma, mfalme wa Gomora, mfalme wa Adma, mfalme wa Seboimu, na mfalme wa Bela (yaani Soari) wakatoka kupanga majeshi yao kwenye Bonde la Sidimu
9 esto es, contra Quedorlaomer, rey de Elam, Tidal, rey de los Goyim, Amrafel, rey de Sinar, y Arioc, rey de Elasar, cuatro reyes contra cinco.
dhidi ya Kedorlaoma, mfalme wa Elamu, Tidali mfalme wa Goimu, Amrafeli mfalme wa Shinari, na Arioko mfalme wa Elasari, yaani wafalme wanne dhidi ya wafalme watano.
10 El valle de Sidim estaba lleno de pozos de asfalto. Al huir el rey de Sodoma y el de Gomorra, cayeron en ellos, y los que quedaron huyeron hacia la montaña.
Basi Bonde la Sidimu lilikuwa limejaa mashimo ya lami, nao wafalme wa Sodoma na wa Gomora walipokimbia, baadhi ya watu walitumbukia huko na wengine wakakimbilia vilimani.
11 Entonces tomaron todos los bienes de Sodoma y Gomorra, y todo su alimento y salieron.
Wale wafalme wanne wakateka mali yote ya Sodoma na Gomora pamoja na vyakula vyao vyote, kisha wakaenda zao.
12 Tomaron a Lot, sobrino de Abram, y sus bienes, y salieron, pues él vivía en Sodoma.
Pia walimteka Loti mwana wa ndugu yake Abramu pamoja na mali zake, kwa kuwa alikuwa akiishi Sodoma.
13 Pero un fugitivo fue e informó a Abram el hebreo, pues él vivía en el robledal de Mamre. El amorreo, hermano de Escol y hermano de Aner, habían hecho un pacto con Abram.
Mtu mmoja aliyekuwa ametoroka akaja kumpa Abramu Mwebrania taarifa. Wakati huu Abramu alikuwa anaishi karibu na mialoni ya Mamre Mwamori, aliyekuwa ndugu yake Eshkoli na Aneri, ambao wote walikuwa wameungana na Abramu.
14 Cuando Abram oyó que su pariente fue llevado cautivo, movilizó a 318 de sus esclavos nacidos en su casa, y los persiguió hasta Dan.
Abramu alipopata habari kwamba jamaa yake amechukuliwa mateka, akawaita watu 318 wa nyumbani mwake waliokuwa wamefunzwa kupigana vita, wakawafuatilia hadi Dani.
15 Él y sus esclavos se desplegaron contra ellos de noche y los atacaron. Los persiguieron hasta Hoba, que está al norte de Damasco.
Wakati wa usiku Abramu aliwagawa watu wake katika vikosi ili awashambulie, na akawafuatilia, akawafukuza hadi Hoba, kaskazini ya Dameski.
16 Recuperó todos los bienes, y también a su pariente Lot y sus bienes, así como a las mujeres y al pueblo.
Akarudisha mali zote, na akamrudisha Loti jamaa yake na mali zake, pamoja na wanawake na watu wengine.
17 Cuando [Abram] regresaba de derrotar a Quedorlaomer y a los reyes que estaban con él, el rey de Sodoma salió a su encuentro en el valle de Savé, que es el valle del Rey.
Abramu aliporudi baada ya kumshinda Mfalme Kedorlaoma na wale wafalme waliojiunga naye, mfalme wa Sodoma akatoka kwenda kumlaki katika Bonde la Shawe (yaani Bonde la Mfalme).
18 Pero Melquisedec, rey de Salem, sacerdote del ʼElohim Altísimo, sacó pan y vino,
Ndipo Melkizedeki mfalme wa Salemu alipoleta mkate na divai. Alikuwa kuhani wa Mungu Aliye Juu Sana.
19 y lo bendijo: ¡Sea bendecido Abram por el ʼElohim Altísimo, Creador de los cielos y de la tierra,
Naye akambariki Abramu, akisema, “Abarikiwe Abramu na Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na nchi.
20 Y bendito sea el ʼElohim Altísimo, Quien entregó a tus adversarios en tu mano! Y [Abram] le entregó el diezmo de todo.
Abarikiwe Mungu Aliye Juu Sana, ambaye amewaweka adui zako mkononi mwako.” Ndipo Abramu akampa Melkizedeki sehemu ya kumi ya kila kitu.
21 Entonces el rey de Sodoma dijo a Abram: Dame las personas y toma para ti los bienes.
Mfalme wa Sodoma akamwambia Abramu, “Nipe hao watu na hizo mali uchukue wewe mwenyewe.”
22 Pero Abram respondió al rey de Sodoma: Levanté mi mano a Yavé el ʼElohim Altísimo, Creador de los cielos y de la tierra,
Lakini Abramu akamwambia mfalme wa Sodoma, “Nimeinua mkono wangu kwa Bwana, Mungu Aliye Juu Sana, Muumba wa mbingu na dunia, na nimeapa
23 que de todo lo que es tuyo, no tomaré ni un hilo ni una correa de sandalia para que no digas: Yo enriquecí a Abram,
kwamba sitapokea kitu chochote kilicho chako, hata kama ni uzi au gidamu ya kiatu, ili kamwe usije ukasema, ‘Nimemtajirisha Abramu.’
24 con la sola excepción de lo que comieron los jóvenes, y la porción de Aner, Escol y Mamre, los hombres que vinieron conmigo. Solo ellos tomarán su parte.
Sitapokea chochote, ila kile tu watu wangu walichokula na sehemu ambayo ni fungu la watu waliokwenda pamoja nami, ambao ni Aneri, Eshkoli na Mamre. Wao na wapewe fungu lao.”