< Génesis 11 >

1 Entonces toda la tierra tenía una sola lengua y las mismas palabras.
Wakati huo dunia yote ilikuwa na lugha moja na msemo mmoja.
2 Aconteció que al salir hacia el oriente, encontraron una llanura en la tierra de Sinar y se establecieron allí.
Watu walipoelekea upande wa mashariki, wakafika kwenye tambarare katika nchi ya Shinari nao wakaishi huko.
3 Entonces se dijeron unos a otros: Vengan, fabriquemos adobes y quemémoslos con fuego. El ladrillo les sirvió en lugar de piedra, y el asfalto en lugar de argamasa.
Wakasemezana wao kwa wao, “Njooni, tufyatue matofali na tuyachome vizuri kwa moto.” Walitumia matofali badala ya mawe, na lami kwa ajili ya kushikamanishia hayo matofali.
4 Y dijeron: Vengan, construyámonos una ciudad y una torre cuya cúspide llegue al cielo. Hagámonos un nombre, en caso de que seamos esparcidos por la superficie de toda la tierra.
Ndipo wakasema, “Njooni, tujijengee mji wenye mnara ambao utafika hadi mbinguni, ili tujipatie jina tusije tukatawanyika usoni pa dunia yote.”
5 Pero Yavé descendió para ver la ciudad y la torre que edificaban los hijos de los hombres.
Lakini Bwana akashuka ili auone mji na mnara ambao wanadamu waliokuwa wanaujenga.
6 Y Yavé dijo: Ciertamente son un pueblo y todos ellos tienen la misma lengua. Éste es solo el principio de su obra y nada les hará desistir de lo que planean hacer.
Bwana akasema, “Ikiwa kama taifa moja wanaozungumza lugha moja wameanza kufanya hili, basi hakuna lolote watakalopanga kufanya ambalo halitawezekana kwao.
7 Vamos, descendamos ya y confundamos allí su lengua para que nadie entienda el lenguaje del otro.
Njooni, tushuke tuvuruge lugha yao ili wasielewane wao kwa wao.”
8 Yavé los dispersó de allí por toda la superficie de la tierra, y desistieron de construir la ciudad.
Hivyo Bwana akawatawanya kutoka mahali pale kwenda katika dunia yote, nao wakaacha kuujenga huo mji.
9 Por eso lo llamó Babel, porque allí Yavé confundió la lengua de toda la tierra. Desde allí Yavé los esparció por la superficie de toda la tierra.
Ndiyo maana pakaitwa Babeli, kwa sababu hapo ndipo Bwana alipoivuruga lugha ya dunia nzima. Kutoka hapo Bwana akawatawanya katika uso wa dunia yote.
10 Estos son los descendientes de Sem: Cuando Sem tenía 100 años engendró a Arfaxad, dos años después del diluvio.
Hivi ndivyo vizazi vya Shemu. Miaka miwili baada ya gharika, Shemu alipokuwa na miaka 100, akamzaa Arfaksadi.
11 Sem vivió después de engendrar a Arfaxad 500 años, y engendró hijos e hijas.
Baada ya kumzaa Arfaksadi, Shemu aliishi miaka 500, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
12 Arfaxad vivió 35 años y engendró a Sala.
Wakati Arfaksadi alipokuwa na miaka thelathini na mitano, akamzaa Shela.
13 Arfaxad vivió 403 años después que engendró a Sala, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Arfaksadi kumzaa Shela, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
14 Sala vivió 30 años y engendró a Heber.
Shela alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Eberi.
15 Sala vivió después de engendrar a Heber 403 años, y engendró hijos e hijas.
Shela baada ya kumzaa Eberi, aliishi miaka 403, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
16 Heber vivió 34 años y engendró a Peleg.
Eberi alipokuwa na miaka thelathini na minne, akamzaa Pelegi.
17 Heber vivió después de engendrar a Peleg 430 años, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Eberi kumzaa Pelegi, aliishi miaka 430, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
18 Peleg vivió 30 años y engendró a Reú.
Pelegi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Reu.
19 Peleg vivió 209 años después de engendrar a Reú, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Pelegi kumzaa Reu, aliishi miaka 209, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
20 Reú vivió 32 años y engendró a Serug.
Reu alipokuwa na miaka thelathini na miwili, akamzaa Serugi.
21 Reú vivió después de engendrar a Serug 207 años, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Reu kumzaa Serugi, aliishi miaka 207, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
22 Serug vivió 30 años y engendró a Nacor.
Serugi alipokuwa na miaka thelathini, akamzaa Nahori.
23 Después de engendrar a Nacor, Serug vivió 200 años, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Serugi kumzaa Nahori, aliishi miaka 200, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
24 Nacor vivió 29 años y engendró a Taré.
Nahori alipokuwa na miaka ishirini na tisa, akamzaa Tera.
25 Nacor vivió después de engendrar a Taré 119 años, y engendró hijos e hijas.
Baada ya Nahori kumzaa Tera, aliishi miaka 119, akazaa watoto wengine wa kiume na wa kike.
26 Y Taré vivió 70 años y engendró a Abram, a Nacor y a Harán.
Tera alipokuwa na miaka sabini, akamzaa Abramu, Nahori na Harani.
27 Estos son los descendientes de Taré: Taré engendró a Abram, a Nacor y a Harán. Harán engendró a Lot.
Hawa ndio wazao wa Tera. Tera aliwazaa Abramu, Nahori na Harani. Harani akamzaa Loti.
28 Pero Harán murió antes que su padre Taré en la tierra de su nacimiento, Ur de los caldeos.
Tera alipokuwa bado hai, Harani akafa huko Uru ya Wakaldayo, nchi alimozaliwa.
29 Abram y Nacor tomaron para ellos esposas. El nombre de la esposa de Abram era Saray y el de la esposa de Nacor era Milca, hija de Harán, padre de Milca y de Isca.
Abramu na Nahori walioa. Mke wa Abramu aliitwa Sarai, na mke wa Nahori aliitwa Milka; Milka na Iska walikuwa watoto wa Harani.
30 Saray era estéril. No tenía hijos.
Sarai alikuwa tasa, hakuwa na watoto.
31 Taré tomó a Abram, su hijo, a Lot, su nieto, hijo de Harán, y a Saray, su nuera, esposa de su hijo Abram, y salieron de Ur de los caldeos para ir a la tierra de Canaán. Pero llegaron hasta Harán y se establecieron allí.
Tera akamchukua Abramu mwanawe, Loti mwana wa Harani mwanawe, na Sarai mkwewe, mke wa Abramu mwanawe, wakatoka kwa pamoja katika Uru ya Wakaldayo kwenda nchi ya Kanaani. Lakini walipofika Harani, wakaishi huko.
32 Los días de Taré fueron 205 años, y murió en Harán.
Tera alikufa huko Harani akiwa na miaka 205.

< Génesis 11 >