< Ezequiel 45 >

1 Cuando repartan por suertes la tierra de la herencia, ofrecerán para Yavé una parcela que la consagrarán, de 75 kilómetros de longitud y de 30 kilómetros de anchura. Todo ese territorio será sagrado.
Wakati mtakapogawanya nchi kama urithi, mtafanya sadakwa kwa Yahwe; sadaka hiyo itakuwa sehemu takatifu ya nchi, dhiraa elfu ishirini na tano urefu, na dhiraa elfu kumi upana. Patakuwa patakatifu, ndani ya mipaka yake yote.
2 De ella se tomará para el Santuario un cuadro de 1,5 kilómetros de longitud y de anchura, y un campo alrededor de 25 metros.
Kutoka hapa kutakuwa na dhiraa mia tano kwa dhiraa mia tano za mraba kuzunguka mahali patakatifu, kwa kuuzunguka mpaka dhiraa hamsini upana.
3 De esta área medirás una parcela de 12,5 kilómetros de longitud y 5 kilómetros de anchura, en la cual estará el Santuario y el Lugar Santísimo.
Kutoka hili eneo utapima fungu ambalo ni dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana; patakuwa patakatifu; mahali patakatifu palipo tukuka.
4 Lo consagrado de esta tierra será para los sacerdotes ministros del Santuario, quienes se acercan para ministrar a Yavé. Servirá de lugar para sus casas y el lugar sagrado para el Santuario.
Patakuwa patakatifu katika nchi kwa ajili ya makuhani wanaomtumikia Yahwe, ajaye kwa Yahwe kumtumikia. Patakuwa mahali kwa ajili ya nyumba na eneo takatifu kwa ajili mahali patakatifu.
5 También habrá un sector de 75 kilómetros de longitud y 30 kilómetros de anchura con 20 cámaras para los levitas ministros de la Casa, como posesión para ellos.
Hivyo itakuwa dhiraa elfu ishirini na tano urefu na elfu kumi upana, patakuwa kwa ajili ya miji ya Walawi wanaotumika kwenye nyumba.
6 Para propiedad de la ciudad señalarán [una parcela] de 2,5 kilómetros de anchura y 12,5 kilómetros de longitud, junto a lo que se apartó para el Santuario. Será para toda la Casa de Israel.
Mtadhihirisha eneo moja kwa ajili ya mji, dhiraa elfu tano na urefu ishirini na tano, hapo patakuwa kando kando ya eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu; huu mji utakuwa wa mali ya nyumba yote ya Israeli.
7 La parte del gobernante estará a ambos lados de lo que se apartó para el Santuario y de la posesión de la ciudad, a lo largo de lo que se apartó para el Santuario, y frente a la posesión de la ciudad. Su longitud corresponderá a una de las porciones, desde sus límites occidental y oriental.
Nchi ya mwana mfalme itakuwa kwa pande zote za eneo lililohifadhiwa kwa ajili ya mahali patakatifu na mji. Patakuwa kwa upande wao wa magaharibi na upande wa mashariki. Urefu utalingana na urefu wa moja ya hayo mafungu, kutoka magaribi hata mashariki.
8 Esta tierra será su posesión en Israel, y nunca más mis gobernantes oprimirán a mi pueblo. El resto de la tierra lo darán a la Casa de Israel según sus tribus.
Hii nchi itakuwa mali ya mwana mfalme katika Isaraeli. Wana wafalme hawatawakandamiza watu wangu; badala yake, watawapatia nchi kwa nyumba ya Israeli, kwa ajili ya makabila yao.
9 ʼAdonay Yavé dice: Basta ya, oh gobernantes de Israel. Dejen la violencia y la rapiña. Hagan juicio y justicia, y quiten sus imposiciones de encima de mi pueblo, dice ʼAdonay Yavé.
Bwana Yahwe asema hivi: Inatosha kwa ajili yenu, mwana mfalme wa Israeli! Ondoa dhuluma na mgogoro; fanya hukumu na haki! Usiwafukuze wapangaji wa watu wangu! -hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
10 Tendrán balanzas justas, efa justo y bato justo.
Mtakuwa na mzani sahihi, efa sahihi, na bathi sahihi!
11 El efa y el bato serán de una misma medida: que el bato tenga la décima parte del homer, y el efa la décima parte del homer; la medida de ellos será según el homer.
Efa na bathi zitakuwa kiasi kile kile, ili kwamba bathi iwe zaka ya homeri; efa itakuwa zaka ya hamori moja. Vipimo vyao vitakuwa vinafanana na homeri.
12 El siclo será de 20 geras. 20 siclos más 25 siclos más 15 siclos, les serán una mina.
Shekeli zitakuwa gera ishirini, shekeli sita zitakuwa mane yenu.
13 Ésta será la ofrenda que ofrecerán: la sexta parte de una medida de 22 litros por cada homer del trigo, y la sexta parte de una medida de 22 litros por cada homer de la cebada.
Hili ndilo toleo mtakalotoa: efa sita kwa kila homeri ya ngano, na mtatoa efa sita kwa kila homeri ya shayiri.
14 La Ordenanza para un bato de aceite, es decir 22 litros de aceite, será que ofrezcan la décima parte de un coro (equivalente a 220 litros). Diez batos son un homer, porque 220 litros son un homer.
Sadaka ya kawaida ya mafuta itakuwa zaka ya bathi kwa kila kori (ambazo ni bathi), au kwa kila hamori, kwa kuwa hamori moja ni bathi kumi pia.
15 Y ofrecerán una cordera del rebaño de 200 de las engordadas por Israel para el sacrificio, el holocausto, las ofrendas de paz y el sacrificio que apacigua por ellos, dice ʼAdonay Yavé.
Kondoo mmoja au mbuzi kutoka mifugo kwa kila wanyama mia mbili kutoka malisho ya maji ya mikoa ya Israeli yatatumika kwa sadaka ya kuteketezwa yoyote au sadaka ya amani kufanya upatanisho kwa ajili ya watu-hivi ndivyo Bwana Yahwe asemavyo.
16 Que todo el pueblo de la tierra dé esta ofrenda para el gobernante de Israel.
Watu wote wa nchi watatoa hii sadaka kwa mwana mfalme wa Israeli.
17 El gobernante deberá proveer el holocausto, el sacrificio y la libación en las fiestas solemnes, en las lunas nuevas, en los sábados y en todas las fiestas de la Casa de Israel. Él dispondrá el sacrificio que apacigua, la ofrenda, el holocausto y las ofrendas de paz, para hacer el sacrificio que apacigua por la Casa de Israel.
Utakuwa wajibu wa mwana mfalme kutoa wanyama kwa ajili ya sadaka za kuteketezwa, sadaka ya unga, sadaka ya kinywaji, katika siku za sikukuu na sherehe za mwezi mpya, na katika siku za Sabato-sikukuu zote za kudumu za nyumba ya Israeli. Ataandaa kwa ajili ya sadaka za dhambi, sadaka za unga, sadaka za kuteketezwa, na sadaka za amani kwa ajili ya upatanisho badala ya nyumba ya Israeli.
18 ʼAdonay Yavé dice: El día primero del mes primero, tomarás un becerro sin defecto y purificarás el Santuario.
Bwana Yahwe asema hivi: Katika mwezi wa kwanza, siku ya kwanza ya mwezi, utachukua ng'ombe mmoja asiyekuwa na dosari kutoka kwenye kundi na kufanya sadaka ya dhambi kwa ajili ya patakatifu.
19 El sacerdote tomará de la sangre del sacrificio que apacigua y untará las jambas de la puerta de la Casa, las cuatro esquinas del zócalo del altar y las jambas de las puertas del patio interno.
Kuhani atachukua baadhi ya damu ya sadaka ya dhambi na kuiweka juu ya miimo ya mlango na kwenye pembe nne za mpaka wa madhabahu, na miimo ya lango la uzio wa ndani.
20 El séptimo día del mes harás esto por los que pecaron por error o engaño. Harás el sacrificio que apacigua por el Templo.
Utafanya hivyo siku ya saba ya mwezi kwa dhambi ya kila mtu kwa ajali au ujinga; katika njia hii mtaipatanisha hekalu.
21 A los 14 días del mes primero celebrarán la Pascua, fiesta solemne de siete días. Se comerá pan sin levadura.
Katika siku ya mwezi siku ya kumi na nne ya mwezi, mtakuwa na sikukuu, sikukuu ya siku saba. Matakula makate usiotiwa chachu.
22 Aquel día el gobernante sacrificará un becerro por el pecado por él mismo y por todo el pueblo de la tierra.
Siku hiyo, mwana mfalme ataandaa ng'ombe kwa ajili yake na kwa ajili ya watu wote wa nchi kama sadaka ya dhambi.
23 Durante los siete días de la fiesta solemne, cada uno de los siete días ofrecerá diariamente el holocausto ante Yavé: siete becerros y siete carneros sin defecto, y un macho cabrío como ofrenda por el pecado.
Kwa siku saba za sikukuu, mwana wa mfalme ataandaa sadaka ya kuteketezwa kwa ajili ya Yahwe: ng'ombe saba na kondoo dume saba zisizokuwa na dosari kila siku kwa mda wa siku saba, na mbuzi dume kila siku kama sadaka ya dhambi.
24 Ofrecerá con cada becerro y cada carnero una ofrenda de 22 litros de aceite. Por cada cantidad de 22 litros de aceite, agregará 3,66 litros de aceite.
Kisha mwana mfalme atatengeneza sadaka ya chakula ya efa moja kwa kila ng'ombe na efa moja kwa kila kondoo dume pamoja na hini ya mafuta kwa kila efa.
25 El mes séptimo, en la solemnidad a los 15 días del mes, hará como en estos siete días en cuanto a ofrenda por el pecado, el holocausto, la ofrenda vegetal y el aceite.
Katika siku ya saba ya mwezi siku ya kumi na tano ya mwezi, katika sikukuu, mwana wa mfalme atafanya matoleo katika siku hizi saba: sadaka za dhambi, sadaka za kuteketezwa, sadaka za chakula, na sadaka za mafuta.

< Ezequiel 45 >