< 2 Samuel 22 >
1 David pronunció las palabras de este cántico a Yavé el día cuando Yavé lo libró de la mano de Saúl y de todos sus enemigos:
Daudi akamwimbia Yahwe maneno ya wimbo huu siku ile Yahwe alipomwokoa katika mkono wa adui zake wote na katika mkono wa Sauli.
2 Yavé es mi Roca, mi Fortaleza, y mi Libertador.
Akaomba hivi, “Yahwe ni mwamba wangu, ngome yangu, aliyeniokoa.
3 ʼElohim es mi Roca, en Quien me refugio, Mi Escudo y el Fuerte de mi salvación, Mi alto Refugio y mi Salvador. De la violencia me libraste.
Mungu ni mwamba wangu. Yeye ni kimbilio langu. Ngao yangu, pembe ya wokovu wangu, ngome yangu na kimbilio langu, aniokoaye na mabaya yote.
4 Invoco a Yavé, Quien es digno de ser alabado Y soy salvo de mis enemigos.
Nitamwita Yahwe, astahiliye kutukuzwa, nami nitaokolewa kutoka kwa adui zangu.
5 Me rodearon ondas de muerte Y torrentes de perversidad me aterraron.
Maana mawimbi ya mauti yalinizunguka, mafuriko ya maji ya uharibifu yakanishinda.
6 Me ataron las cuerdas del Seol Y me alcanzaron las cuerdas de la muerte. (Sheol )
Vifungo vya kuzimu vilinizunguka; kamba za mauti zikaninasa. (Sheol )
7 En mi angustia invoqué a Yavé. Invoqué a mi ʼElohim. Oyó mi voz desde su Templo, Y mi grito de auxilio llegó a sus oídos.
Katika shida yangu nalimwita Yahwe; nilimwita Mungu wangu; akaisikia sauti yangu katika hekalu lake, na kilio changu cha msaada kikafika masikioni mwake.
8 La tierra fue conmovida y tembló. Se conmovieron los cimientos del cielo. Se estremecieron porque Él se airó.
Ndipo nchi ilipotikisika na kutetemeka. Misingi ya mbingu ikatetemeka na kutikiswa, kwa kuwa Mungu alikasirika.
9 Humo subió de su nariz Y de su boca salió un fuego abrasador Que encendió brasas.
Moshi ukatoka katika pua yake, na miale ya moto ikatoka katika kinywa chake. Makaa yakawashwa nayo.
10 Inclinó los cielos, Y descendió con espesa oscuridad debajo de sus pies.
Alizifungua mbingu akashuka, na giza totoro lilikuwa chini ya miguu yake.
11 Cabalgó sobre un querubín y voló. Voló sobre las alas del viento.
Alipanda juu ya kerubi na kuruka. Alionekana katika mawingu ya upepo.
12 Puso oscuridad alrededor de Él como escondedero, Oscuridad de aguas y densos nubarrones.
Naye akalifanya giza kuwa hema kumzunguka, akakusanya mawingu makubwa ya mvua angani.
13 Con el resplandor de su Presencia se encendieron brasas.
Makaa ya moto yalidondoka mbele zake kutoka katika radi.
14 Yavé tronó desde el cielo, ʼElyón dio su voz.
Yahwe alishuka kutoka katika mbingu. Aliyejuu alipiga kelele.
15 Disparó sus flechas y los dispersó. Lanzó relámpagos, y los destruyó.
Alipiga mishale na kuwatawanya adui zake—miale ya radi na kuwasambaratisha.
16 Entonces aparecieron los torrentes de las aguas Y quedaron descubiertos los cimientos del mundo a la reprensión de Yavé Por el soplo del aliento de su nariz.
Kisha njia za maji zikaonekana; misingi ya dunia ikawa wazi katika kilio cha vita ya Yahweh, katika sauti za pumzi ya pua zake.
17 Envió desde lo alto y me tomó. Me sacó de entre las aguas caudalosas.
Kutoka juu alifika chini; akanishikilia! Aliniondoa katika vilindi vya maji.
18 Me libró de un poderoso enemigo, Y de los que me aborrecían, Aunque eran más fuertes que yo.
Aliniokoa kutoka kwa adui zangu wenye nguvu, kwao walionichukia, kwa maana walikuwa na nguvu sana kwangu.
19 Me enfrentaron en el día de mi quebranto, Pero Yavé fue mi Apoyo
Walikuja kinyume changu siku ya shida yangu, lakini Yahwe alikuwa msaada wangu.
20 Y me sacó a lugar espacioso. Me libró, porque se agradó de mí.
Pia aliniweka mahali panapo nafasi. Aliniokoa kwa kuwa alipendezwa nami.
21 Yavé me premió según mi rectitud Y recompensó la pureza de mis manos,
Yahwe amenituza kwa kipimo cha haki yangu; amenirejesha kwa kiwango cha usafi wa mikono yangu.
22 Porque guardé los caminos de Yavé Y no me aparté impíamente de mi ʼElohim.
Kwa maana nimezishika njia za Yahwe na sijafanya uovu kwa kugeuka kutoka kwa Mungu.
23 Pues todos sus Preceptos estuvieron delante de mí, Y no me aparté de sus Estatutos.
Kwa kuwa maagizo yake yote ya haki yamekuwa mbele yangu; kwa kuwa sheria zake, sikujiepusha nazo.
24 Fui recto ante Él Y me guardé de mi maldad.
Nimekuwa bila hatia mbele zake pia, na nimejiepusha na dhambi.
25 Yavé me recompensó según mi rectitud Según la pureza de mis manos ante Él.
Kwa hiyo Yahwe amenirejesha kwa kiasi cha uadilifu wangu, kwa kipimo cha usafi wangu mbele zake.
26 Con el misericordioso te muestras misericordioso, Y recto con el hombre íntegro.
Kwa mwaminifu, unajionesha kuwa mwaminifu; kwake asiye na hatia; unajionesha kuwa hauna hatia.
27 Limpio te muestras con el limpio, Y sagaz con el perverso.
Kwa usafi unajionesha kuwa msafi, lakini kwa wakaidi unajionesha kuwa mkaidi.
28 Tú salvas al pueblo afligido, Pero tus ojos están sobre los altivos para humillarlos.
Unaokoa walioteswa, lakini macho yako ni kinyume cha wenye kiburi, unawashusha chini.
29 ¡Tú eres mi Lámpara, oh Yavé! ¡Oh Yavé, Tú alumbras mi oscuridad!
Kwa maana wewe ni taa yangu, Yahwe. Yahwe huangaza katika giza langu.
30 Porque contigo puedo asaltar un ejército. Con mi ʼElohim puedo saltar sobre un muro.
Maana kwa ajili yake ninaweza kupita vipingamizi; kwa msaada wa Mungu wangu naweza kuruka juu ya ukuta.
31 En cuanto a ʼEL, perfecto es su camino, Y acrisolada es la Palabra de Yavé. ʼEL es Escudo a todos los que se refugian en Él.
Maana njia za Mungu ni kamilifu. Neno la Yahwe ni safi. Yeye ni ngao yao wanaomkimbilia.
32 Porque ¿quién es ʼEL, excepto Yavé? ¿Y cuál roca hay además de nuestro ʼElohim?
Maana ni nani aliye Mungu isipokuwa Yahwe? Na ni nani aliyemwamba isipokuwa Mungu?
33 ʼEL es el que me ciñe de vigor Y perfecciona mi camino.
Mungu ni kimbilio langu, na umwongoza katika njia yake mtu asiye na hatia.
34 ʼEL hace que mis pies sean como los de venados Y me establece en mis alturas.
Huifanya myepesi miguu yangu kama kurungu na kuniweka katika vilima virefu.
35 El que adiestra mis manos para la batalla Y mis brazos para tensar el arco de bronce.
Huifundisha mikono yangu kwa vita, na viganja vyangu kupinda upinde wa shaba.
36 Me diste también el escudo de tu salvación Y me engrandeció tu benignidad.
Umenipa ngao ya wokovu wako, na matakwa yako yamenifanya mkuu.
37 Ensanchas mis pasos debajo de mí, Y no resbalan mis pies.
Umeitengenezea miguu yangu nafasi chini yangu, hivyo miguu yangu haikujikwaa.
38 Perseguí a mis enemigos y los destruí, Y no regresé hasta que fueron acabados.
Niliwafuatia adui zangu na kuwaangamiza. Sikurudi nyuma hadi walipoangamizwa.
39 Los destruí, los destrocé para que no se levanten. Cayeron bajo mis pies.
Niliwararua na kuwasambaratisha; hawawezi kuinuka. Wameanguka chini ya miguu yangu.
40 Pues Tú me dotaste de fuerza para la batalla. Doblegaste a mis enemigos debajo de mí.
Unaweka nguvu ndani yangu kama mkanda kwa vita; unawaweka chini yangu wanaoinuka kinyume changu.
41 También hiciste que mis enemigos me volvieran la espalda, Para que yo destruya a los que me aborrecen.
Ulinipa migongo ya shingo za adui zangu; niliwaangamiza kabisa wale wanaonichukia.
42 Clamaron, y no hubo quien salvara. Aun [clamaron] a Yavé, pero no los escuchó.
Walilia kwa msaada, lakini hakuna aliyewaokoa; walimlilia Yahwe, lakini hakuwajibu.
43 Los molí como polvo de la tierra. Los pisé y los trituré como el lodo de las calles.
Niliwaponda katika vipande kama mavumbi juu ya ardhi, niliwakanyaga kama matope mitaani.
44 Tú me libraste de las contiendas de mi pueblo. Me guardaste para ser jefe de naciones. Pueblo que yo no conocía me sirvió.
Umeniokoa pia kutoka katika mashutumu ya watu wangu. Umeniweka kama kichwa cha mataifa. Watu nisiowajua wananitumikia.
45 Los hijos de extranjeros se someten a mí. Al oír de mí, me obedecen.
Wageni walishurutishwa kuniinamia. Mara waliposikia kuhusu mimi, walinitii.
46 Los extranjeros se debilitan Y salen temblorosos de sus encierros.
Wageni walikuja wakitetemeka kutoka katika ngome zao.
47 ¡Viva Yavé! ¡Bendita sea mi Roca! ¡Engrandecido sea ʼElohim, la Roca de mi salvación!
Yahwe anaishi! Mwamba wangu atukuzwe. Mungu na ainuliwe, mwamba wa wokovu wangu.
48 El ʼEL que ejecuta venganza por mí, Y somete pueblos a mí.
Huyu ndiye Mungu anilipiaye kisasi, awawekaye watu chini yangu.
49 El que también me saca de entre los enemigos, Y aun me exalta por encima de los que se levantan contra mí.
Uniweka huru mbali na adui zangu. Hakika, uliniinua juu yao walioinuka kinyume changu. Uliniokoa kutoka kwa watu wenye ghasia.
50 Por tanto yo te alabaré, oh Yavé, entre las naciones. Cantaré alabanzas a tu Nombre.
Kwa hiyo nitakushukuru, Yahwe, kati ya mataifa; nitaliimbia sifa jina lako.
51 Él engrandece las victorias de su rey, Y muestra misericordia a su ungido: A David y a sus descendientes para siempre.
Mungu hutoa ushindi mkuu kwa mfalme wake, na uonesha uaminifu wake wa kiagano kwa mtiwa mafuta wake, kwa Daudi na uzao wake daima.”