< Salmos 83 >
1 Una canción. Un salmo de Asaf. Dios, no guardes silencio. No te quedes callado, y no te quedes quieto, Dios.
Ee Mungu, usikae kimya! usitupuuze na kustarehe, Ee Mungu.
2 Porque, he aquí, tus enemigos están agitados. Los que te odian han levantado la cabeza.
Tazama, adui zako wanafanya vurugu, na wale wakuchukiao wameinua vichwa vyao.
3 Conspiran con astucia contra tu pueblo. Conspiran contra tus seres queridos.
Wanafanya hila juu ya watu wako na kwa pamoja kupanga njama dhidi ya wale uwalindao. Wamesema,
4 “Vamos”, dicen, “destruyámoslos como nación, para que el nombre de Israel no sea más recordado”.
“Njoni na tuwaangamize wao kama taifa. Kisha jina la Israeli halitakumbukwa.”
5 Porque han conspirado juntos con una sola mente. Forman una alianza contra ti.
Wamepanga njama pamoja wakiwa na mkakati mmoja; wamefanya muungano dhidi yako.
6 Las tiendas de Edom y de los ismaelitas; Moab, y los Hagritas;
Hii inajumuisha hema za Edomu na Waishmaeli, na watu wa Moabu na Wahagari, ambao wamepanga njama pamoja nao
7 Gebal, Amón y Amalec; Filistea con los habitantes de Tiro;
Gebal, Amoni, Amaleki; pia inajumuisha Filisti na wenyeji wa Tiro.
8 También Asiria se une a ellos. Han ayudado a los hijos de Lot. (Selah)
Ashuri pia ameshirikina nao; wanawasaidia wana wa Lutu. Serah
9 Haz con ellos lo que hiciste con Madián, como a Sísara, como a Jabín, en el río Cisón;
Ufanye kwao kama ulivyofanya kwa Midiani, kama ulivyofanya kwa Sisera na kwa Yabini kwenye Mto Kishoni.
10 que perecieron en Endor, que se convirtió en estiércol para la tierra.
Waliangamizwa kule Endori na wakawa kama mbolea juu ya chi.
11 Haz que sus nobles sean como Oreb y Zeeb, sí, todos sus príncipes como Zebah y Zalmunna,
Uvifanye vyeo vyao kama Oreb na Zeeb, na wakuu wao wote kama Zeba na Zalmuna.
12 que dijo: “Tomemos posesión de las tierras de pastoreo de Dios”.
Wao walisema, natujimilikishe malisho ya Mungu.”
13 Dios mío, haz que sean como una planta rodadora, como paja ante el viento.
Ee Mungu wangu, uwafanye kama mavumbi ya kisulisuli, kama makapi mbele ya upepo,
14 Como el fuego que quema el bosque, como la llama que incendia las montañas,
Kama moto uteketezao msitu, na kama miali ya moto iwakayo milimani.
15 así que persíguelos con tu tempestad, y aterrorízalos con tu tormenta.
Uwafuatie kwa tufani yako, na kuwafadhaisha kwa dhoruba yako.
16 Llena sus rostros de confusión, para que busquen tu nombre, Yahvé.
Uwajaze nyuso zao kwa aibu ili kwamba waweze kulitafuta jina lako, Yahwe.
17 Que queden desilusionados y consternados para siempre. Sí, que se confundan y perezcan;
Nao waaibishwe na kufadhaishwa milele; waangamizwe katika aibu.
18 para que sepan que sólo tú, cuyo nombre es Yahvé, eres el Altísimo sobre toda la tierra.
Kisha watajua kwamba ni wewe pekee, Yahwe, Uliye Juu ya nchi yote.