< Salmos 76 >
1 Para el músico jefe. Con instrumentos de cuerda. Un salmo de Asaf. Una canción. En Judá, Dios es conocido. Su nombre es grande en Israel.
Kwa mwimbishaji. Kwa ala za nyuzi za muziki. Zaburi ya Asafu. Wimbo. Katika Yuda, Mungu anajulikana, jina lake ni kuu katika Israeli.
2 Su tabernáculo está también en Salem. Su morada en Sión.
Hema lake liko Salemu, makao yake katika Sayuni.
3 Allí rompió las flechas de fuego del arco, el escudo, la espada y las armas de guerra. (Selah)
Huko alivunja mishale imetametayo, ngao na panga, silaha za vita.
4 Glorioso eres, y excelente, más que montañas de caza.
Wewe unangʼaa kwa mwanga, mwenye fahari zaidi ya milima yenye utajiri wa wanyama pori.
5 Los hombres valientes yacen saqueados, han dormido su último sueño. Ninguno de los hombres de guerra puede levantar las manos.
Mashujaa hulala wametekwa nyara, hulala usingizi wao wa mwisho; hakuna hata mmoja wa watu wa vita anayeweza kuinua mikono yake.
6 Ante tu reprimenda, Dios de Jacob, tanto el carro como el caballo son arrojados a un sueño muerto.
Kwa kukemea kwako, Ee Mungu wa Yakobo, farasi na gari la vita vilikaa kimya.
7 Tú, incluso tú, eres de temer. ¿Quién puede estar a tu vista cuando estás enfadado?
Wewe peke yako ndiye wa kuogopwa. Ni nani awezaye kusimama mbele yako unapokasirika?
8 Tú pronunciaste el juicio desde el cielo. La tierra temió y guardó silencio,
Kutoka mbinguni ulitamka hukumu, nayo nchi ikaogopa, ikawa kimya:
9 cuando Dios se levantó para juzgar, para salvar a todos los afligidos de la tierra. (Selah)
wakati wewe, Ee Mungu, ulipoinuka kuhukumu, kuwaokoa wote walioonewa katika nchi.
10 Ciertamente la ira del hombre te alaba. Los supervivientes de tu ira están contenidos.
Hakika ghadhabu yako dhidi ya wanadamu inakuletea sifa, na masalia ya ghadhabu yako unajifunga mshipi.
11 ¡Haz votos a Yahvé, tu Dios, y cúmplelos! Que todos sus vecinos le traigan regalos a quien debe ser temido.
Wekeni nadhiri kwa Bwana Mungu wenu na kuzitimiza; nchi zote za jirani na walete zawadi kwa Yule astahiliye kuogopwa.
12 cortará el espíritu de los príncipes. Es temido por los reyes de la tierra.
Huvunja roho za watawala; anaogopwa na wafalme wa dunia.