< Salmos 38 >

1 Un salmo de David, para una conmemoración. Yahvé, no me reprendas en tu ira, ni me castigues en tu caliente descontento.
Zaburi ya Daudi. Maombi. Ee Bwana, usinikemee katika hasira yako, wala kuniadhibu katika ghadhabu yako.
2 Porque tus flechas me han atravesado, tu mano me presiona con fuerza.
Kwa kuwa mishale yako imenichoma, na mkono wako umenishukia.
3 No hay solidez en mi carne a causa de tu indignación, ni hay salud en mis huesos a causa de mi pecado.
Hakuna afya mwilini mwangu kwa sababu ya ghadhabu yako, mifupa yangu haina uzima kwa sababu ya dhambi zangu.
4 Porque mis iniquidades han pasado por encima de mi cabeza. Como carga pesada, son demasiado pesados para mí.
Maovu yangu yamenifunika kama mzigo usiochukulika.
5 Mis heridas son repugnantes y corruptas a causa de mi estupidez.
Majeraha yangu yameoza na yananuka, kwa sababu ya upumbavu wa dhambi zangu.
6 Me duele y me inclino mucho. Voy de luto todo el día.
Nimeinamishwa chini na kushushwa sana, mchana kutwa nazunguka nikiomboleza.
7 Porque mi cintura está llena de ardor. No hay solidez en mi carne.
Viuno vyangu vimejaa maumivu yaunguzayo, hakuna afya mwilini mwangu.
8 Me siento débil y gravemente herido. He gemido por la angustia de mi corazón.
Nimedhoofika na kupondwa kabisa, nasononeka kwa maumivu makuu ya moyoni.
9 Señor, todo mi deseo está ante ti. Mi gemido no se te oculta.
Ee Bwana, yote ninayoyaonea shauku yako wazi mbele zako, kutamani kwangu sana hakufichiki mbele zako.
10 Mi corazón palpita. Me fallan las fuerzas. En cuanto a la luz de mis ojos, también me ha dejado.
Moyo wangu unapigapiga, nguvu zangu zimeniishia; hata macho yangu yametiwa giza.
11 Mis amantes y mis amigos se mantienen alejados de mi plaga. Mis parientes están lejos.
Rafiki na wenzangu wananikwepa kwa sababu ya majeraha yangu; majirani zangu wanakaa mbali nami.
12 También los que buscan mi vida ponen trampas. Los que buscan mi daño hablan cosas maliciosas, y meditar engaños todo el día.
Wale wanaotafuta uhai wangu wanatega mitego yao, wale ambao wangetaka kunidhuru huongea juu ya maangamizi yangu; hufanya shauri la hila mchana kutwa.
13 Pero yo, como un sordo, no oigo. Soy como un hombre mudo que no abre la boca.
Mimi ni kama mtu kiziwi, asiyeweza kusikia, ni kama bubu, asiyeweza kufungua kinywa chake,
14 Sí, soy como un hombre que no oye, en cuya boca no hay reproches.
nimekuwa kama mtu asiyesikia, ambaye kinywa chake hakiwezi kutoa jibu.
15 Porque espero en ti, Yahvé. Tú responderás, Señor mi Dios.
Ee Bwana, ninakungojea wewe, Ee Bwana Mungu wangu, utajibu.
16 Porque dije: “No dejes que se regodeen en mí, o se exaltan sobre mí cuando mi pie resbala”.
Kwa kuwa nilisema, “Usiwaache wafurahie, wala wasijitukuze juu yangu mguu wangu unapoteleza.”
17 Porque estoy dispuesto a caer. Mi dolor está continuamente ante mí.
Kwa maana ninakaribia kuanguka, na maumivu yangu yananiandama siku zote.
18 Porque declararé mi iniquidad. Me arrepentiré de mi pecado.
Naungama uovu wangu, ninataabishwa na dhambi yangu.
19 Pero mis enemigos son vigorosos y numerosos. Los que me odian sin razón son numerosos.
Wengi ni wale ambao ni adui zangu hodari, wale wanaonichukia bila sababu ni wengi.
20 Los que dan el mal por el bien son también adversarios míos, porque sigo lo que es bueno.
Wanaolipa maovu kwa wema wangu hunisingizia ninapofuata lililo jema.
21 No me abandones, Yahvé. Dios mío, no te alejes de mí.
Ee Bwana, usiniache, usiwe mbali nami, Ee Mungu wangu.
22 Date prisapara ayudarme, Señor, mi salvación.
Ee Bwana Mwokozi wangu, uje upesi kunisaidia.

< Salmos 38 >