< Salmos 34 >

1 Por David; cuando fingió estar loco ante Abimelec, quien lo expulsó, y él se marchó. Bendeciré a Yahvé en todo momento. Su alabanza siempre estará en mi boca.
Nitamsifu Yahwe wakati wote, siku zote sifa zake zitakuwa mdomoni mwangu.
2 Mi alma se jactará en Yahvé. Los humildes lo oirán y se alegrarán.
Nitamsifu Yahwe! walio onewa wasikie na kufurahi.
3 Oh, engrandece a Yahvé conmigo. Exaltemos juntos su nombre.
Msifuni Yahwe pamoja nami, kwa pamoja tuliinue jina lake.
4 Busqué a Yahvé y me respondió, y me libró de todos mis temores.
Nilimuomba Yahwe msaada naye akanijibu, akanipa ushindi juu ya hofu yangu yote.
5 Lo miraron y quedaron radiantes. Sus rostros nunca se cubrirán de vergüenza.
Wale wanao mtazama yeye wana furaha, na nyuso zao hazina aibu.
6 Este pobre hombre clamó, y Yahvé lo escuchó, y lo salvó de todos sus problemas.
Huyu mtu aliye onewa alilia na Yahwe akamsikia na kumuokoa kwenye matatizo yake yote.
7 El ángel de Yahvé acampa alrededor de los que le temen, y los entrega.
Malaika wa Yahwe huweka kambi wakiwazunguka wale wanao muogopa yeye na kuwaokoa.
8 Oh, probad y ved que Yahvé es bueno. Dichoso el hombre que se refugia en él.
Onjeni muone Yahwe ni mzuri. Amebarikiwa mtu yule ambaye Yahwe ni kimbilio lake.
9 Temed a Yahvé, vosotros sus santos, porque no hay falta con los que le temen.
Muogopeni Yahwe, ninyi watu watakatifu wake. Hakuna kupungukikwa kwa wale wanao mhofu yeye.
10 Los leones jóvenes carecen y sufren hambre, pero a los que buscan a Yahvé no les faltará nada bueno.
Simba wadogo wakati mwingine hukosa chakula na kuteseka kwa njaa, bali wale wamtafutao Yahwe hawatapungukiwa chochote kilicho kizuri.
11 Venid, niños, escuchadme. Te enseñaré el temor de Yahvé.
Njoni, wana, mnisikilize mimi. nitawafundisha ninyi hofu ya Yahwe.
12 Que es alguien que desea la vida, y ama muchos días, para que vea el bien?
Mtu nani aliyepo ambaye anatamani maisha na anapenda kuwa na siku nyingi, ili kwamba aweze kuona vizuri?
13 Guarda tu lengua del mal, y tus labios de decir mentiras.
Hivyo uepushe ulimi wako na uovu na uilinde midomo yako kuongea uongo.
14 Apártate del mal y haz el bien. Busca la paz y persíguela.
Uache uovu na utende mema. Uitafute amani na kuiendea amani.
15 Los ojos de Yahvé están hacia los justos. Sus oídos escuchan su grito.
Macho ya Yahwe yako kwenye haki na masikio yake huelekea kulia kwao.
16 El rostro de Yahvé está contra los que hacen el mal, para cortar su memoria de la tierra.
Uso wa Yahwe uko kinyume na wale watendao uovu, kuikatilia mbali kumbukumbu yao duniani.
17 Los justos claman, y Yahvé los escucha, y los libra de todos sus problemas.
Wenye haki hulia na Yahwe husikia na kuwaokoa kwenye matatizo yao yote.
18 Yahvé está cerca de los que tienen el corazón roto, y salva a los que tienen el espíritu abatido.
Yahwe yu karibu nao waliovunjika moyo, naye huwaokoa waliogandamizwa rohoni.
19 Muchas son las aflicciones de los justos, pero Yahvé lo libra de todos ellos.
Mateso ya wenye haki ni mengi, bali Yahwe huwaokoa nayo yote.
20 Protege todos sus huesos. Ninguno de ellos está roto.
Yeye huitunza mifupa yake yote, hakuna hata mmoja wao utavunjika.
21 El mal matará a los malvados. Los que odian a los justos serán condenados.
Uovu utawauwa waovu. Wale wachukiao haki watahukumiwa.
22 Yahvé redimeel alma de sus siervos. Ninguno de los que se refugian en él será condenado.
Yahwe huokoa maisha ya watumishi wake. Hakuna atakaye hukumiwa hata mmoja atafutaye usalama katika yeye.

< Salmos 34 >