< Salmos 2 >

1 Por qué se enfurecen las naciones, ¿y los pueblos traman una cosa vana?
Kwa nini mataifa wanafanya dhoruba, kwa nini watu wanafanya njama ambazo zitafeli?
2 Los reyes de la tierra toman posición, y los gobernantes se aconsejan entre sí, contra Yahvé y contra su Ungido, diciendo,
Wafalme wa nchi kwa pamoja hushikilia misimamo yao na watawala kwa pamoja hufanya njama kinyume na Yahwe na kinyume na Masihi, wakisema,
3 “Rompamos sus vínculos, y arrojar sus cuerdas de nosotros”.
“Ngoja tuzikate pingu walizo tufingia sisi na kuzitupa pingu zao.”
4 El que está sentado en los cielos se reirá. El Señor se burlará de ellos.
Yeye aketie katika mbingu atacheka kwa dharau mbele yao; Bwana atawadhihaki wao.
5 Entonces les hablará en su ira, y aterrorizarlos en su ira:
Kisha ataongea nao katika hasira yake na kuwaogofya kwa gadhabu yake, akisema,
6 “Pero he puesto a mi Rey en mi santo monte de Sión”.
“Mimi mwenyewe nilimpaka mafuta mfalme wa Sayuni, mlima wangu mtakatifu.”
7 Voy a contar el decreto: Yahvé me dijo: “Tú eres mi hijo. Hoy me he convertido en tu padre.
Nami nitatangaza amri ya Yahwe. Yeye aliniambia, “wewe ni mwanangu! Leo hii nimekuwa baba yako.
8 Pídeme y te daré las naciones como herencia, los confines de la tierra para su posesión.
Uniombe, nami nitakupa wewe taifa kwa ajili ya urithi na mikoa ya nchi iliyo bora kwa ajili ya umiliki wako.
9 Los romperás con una vara de hierro. Los harás pedazos como una vasija de alfarero”.
Wewe utawavunja wao kwa fimbo ya chuma; kama vile mtungi wa mfinyanzi, wewe utawavunja wao vipande vipande.”
10 Ahora, pues, sed sabios, reyes. Instrúyanse, jueces de la tierra.
Hivyo sasa, ninyi wafalme; mchukue tahadhari; mjirekebishe.
11 Sirve a Yahvé con temor, y se regocija con el temblor.
Mwabuduni Yahwe kwa hofu na mfurahi mkitetemeka.
12 Dad un homenaje sincero al Hijo, no sea que se enfade y perezcáis en el camino, porque su ira pronto se encenderá. Dichosos los que se refugian en él.
Mumbusu mwana vinginevyo atawakasirikia, na mtakufa pale pale hasira yake ikiwaka. Ni jinsi gani wamebarikiwa wale wote watafutao usalama ndani yake.

< Salmos 2 >