< Salmos 107 >

1 Dad gracias a Yahvé, porque es bueno, porque su bondad es eterna.
Mshukuruni Bwana, kwa kuwa yeye ni mwema, upendo wake wadumu milele.
2 Que lo digan los redimidos por Yahvé, a quienes ha redimido de la mano del adversario,
Waliokombolewa wa Bwana na waseme hivi, wale aliowaokoa kutoka mkono wa adui,
3 y recogido de las tierras, desde el este y desde el oeste, desde el norte y desde el sur.
wale aliowakusanya kutoka nchi mbalimbali, kutoka mashariki na magharibi, kutoka kaskazini na kusini.
4 Vagaron por el desierto, por un camino desértico. No encontraron ninguna ciudad en la que vivir.
Baadhi yao walitangatanga jangwani, hawakuona njia ya kuwafikisha mji ambao wangeweza kuishi.
5 Hambre y sed, su alma se desmayó en ellos.
Walikuwa na njaa na kiu, nafsi zao zikadhoofika.
6 Entonces clamaron a Yahvé en su angustia, y los libró de sus angustias.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
7 También los condujo por un camino recto, para que puedan ir a una ciudad a vivir.
Akawaongoza kwa njia iliyo sawa hadi mji ambao wangeweza kuishi.
8 Que alaben a Yahvé por su amorosa bondad, ¡por sus maravillosos hechos a los hijos de los hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
9 Porque él satisface el alma anhelante. Llena de bien el alma hambrienta.
kwa maana yeye humtosheleza mwenye kiu, na kumshibisha mwenye njaa kwa vitu vyema.
10 Algunos se sentaron en la oscuridad y en la sombra de la muerte, estando atado en la aflicción y el hierro,
Wengine walikaa gizani na katika huzuni kuu, wafungwa wakiteseka katika minyororo,
11 porque se rebelaron contra las palabras de Dios, y condenó el consejo del Altísimo.
kwa sababu walikuwa wameasi dhidi ya maneno ya Mungu na kudharau shauri la Aliye Juu Sana.
12 Por lo tanto, hizo caer su corazón con el trabajo. Se cayeron, y no había nadie para ayudar.
Aliwatumikisha kwa kazi ngumu; walijikwaa na hapakuwepo yeyote wa kuwasaidia.
13 Entonces clamaron a Yahvé en su angustia, y los salvó de sus angustias.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
14 Los sacó de las tinieblas y de la sombra de la muerte, y rompió sus cadenas.
Akawatoa katika giza na huzuni kuu na akavunja minyororo yao.
15 Que alaben a Yahvé por su amorosa bondad, ¡por sus maravillosos hechos a los hijos de los hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu,
16 Porque ha roto las puertas de bronce, y cortar a través de barras de hierro.
kwa kuwa yeye huvunja malango ya shaba na kukata mapingo ya chuma.
17 Los tontos son afligidos a causa de su desobediencia, y por sus iniquidades.
Wengine wakawa wapumbavu kutokana na uasi wao, wakapata mateso kwa sababu ya uovu wao.
18 Su alma aborrece toda clase de alimentos. Se acercan a las puertas de la muerte.
Wakachukia kabisa vyakula vyote, wakakaribia malango ya mauti.
19 Entonces claman a Yahvé en su angustia, y los salva de sus angustias.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawaokoa kutoka taabu yao.
20 Envía su palabra y los cura, y los libera de sus tumbas.
Akalituma neno lake na kuwaponya, akawaokoa kutoka maangamizo yao.
21 Que alaben a Yahvé por su amorosa bondad, ¡por sus maravillosos hechos a los hijos de los hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
22 Que ofrezcan los sacrificios de acción de gracias, y declaren sus hazañas con cantos.
Na watoe dhabihu za kushukuru, na wasimulie matendo yake kwa nyimbo za furaha.
23 Los que bajan al mar en barcos, que hacen negocios en aguas grandes,
Wengine walisafiri baharini kwa meli, walikuwa wafanyabiashara kwenye maji makuu.
24 estos ven las obras de Yahvé, y sus maravillas en las profundidades.
Waliziona kazi za Bwana, matendo yake ya ajabu kilindini.
25 Porque él manda y levanta el viento tempestuoso, que levanta sus olas.
Kwa maana alisema na kuamsha tufani iliyoinua mawimbi juu.
26 Suben al cielo; bajan de nuevo a las profundidades. Su alma se derrite por los problemas.
Yakainuka juu mbinguni, yakashuka chini hadi vilindini, katika hatari hii ujasiri wao uliyeyuka.
27 Se tambalean de un lado a otro y se tambalean como un borracho, y no saben qué hacer.
Walipepesuka na kuyumbayumba kama walevi, ujanja wao ukafikia ukomo.
28 Entonces claman a Yahvé en su aflicción, y los saca de su angustia.
Ndipo walipomlilia Bwana katika shida yao, naye akawatoa kwenye taabu yao.
29 Él hace de la tormenta una calma, para que sus ondas estén quietas.
Akatuliza dhoruba kwa mnongʼono, mawimbi ya bahari yakatulia.
30 Entonces se alegran porque hay calma, por lo que los lleva a su refugio deseado.
Walifurahi ilipokuwa shwari, naye akawaongoza hadi bandari waliyoitamani.
31 Que alaben a Yahvé por su amorosa bondad, ¡por sus maravillosas obras para los hijos de los hombres!
Basi na wamshukuru Bwana kwa upendo wake usiokoma, na kwa matendo yake ya ajabu kwa wanadamu.
32 Que lo exalten también en la asamblea del pueblo, y alabarlo en la sede de los ancianos.
Na wamtukuze yeye katika kusanyiko la watu, na wamsifu katika baraza la wazee.
33 Convierte los ríos en un desierto, el agua brota en una tierra sedienta,
Yeye aligeuza mito kuwa jangwa, chemchemi za maji zitiririkazo kuwa ardhi yenye kiu,
34 y una tierra fructífera en un despojo de sal, por la maldad de los que la habitan.
nchi izaayo ikawa ya chumvi isiyofaa, kwa sababu ya uovu wa wale walioishi humo.
35 Convierte un desierto en un estanque de agua, y una tierra seca en manantiales de agua.
Aligeuza jangwa likawa madimbwi ya maji, nayo ardhi kame kuwa chemchemi za maji zitiririkazo;
36 Allí hace vivir a los hambrientos, para que preparen una ciudad en la que vivir,
aliwaleta wenye njaa wakaishi humo, nao wakajenga mji wangeweza kuishi.
37 sembrar campos, plantar viñedos, y cosechar los frutos del aumento.
Walilima mashamba na kupanda mizabibu, nayo ikazaa matunda mengi,
38 También los bendice, para que se multipliquen en gran medida. No permite que su ganado disminuya.
Mungu aliwabariki, hesabu yao ikaongezeka sana, wala hakuruhusu mifugo yao kupungua.
39 Nuevamente, se ven disminuidos e inclinados a través de la opresión, los problemas y el dolor.
Kisha hesabu yao ilipungua, na walinyenyekeshwa kwa kuonewa, maafa na huzuni.
40 Derrama desprecio sobre los príncipes, y les hace vagar por un desierto sin huellas.
Yeye ambaye huwamwagia dharau wakuu, aliwafanya watangetange nyikani isiyo na njia.
41 Sin embargo, levanta a los necesitados de su aflicción, y aumenta sus familias como un rebaño.
Lakini yeye aliwainua wahitaji katika taabu zao, na kuongeza jamaa zao kama makundi ya kondoo.
42 Los rectos lo verán y se alegrarán. Todos los malvados cerrarán la boca.
Wanyofu wataona na kufurahi, lakini waovu wote watafunga vinywa vyao.
43 El que sea sabio prestará atención a estas cosas. Considerarán las bondades amorosas de Yahvé.
Yeyote aliye na hekima, ayasikie mambo haya, na atafakari upendo mkuu wa Bwana.

< Salmos 107 >