< Salmos 105 >
1 ¡Den gracias a Yahvé! ¡Invoca su nombre! Haz que se conozcan sus actos entre los pueblos.
Mshukuruni Bwana, liitieni jina lake, wajulisheni mataifa yale aliyoyatenda.
2 ¡Cantadle, cantadle alabanzas! Cuenta todas sus maravillosas obras.
Mwimbieni yeye, mwimbieni yeye sifa, waambieni matendo yake yote ya ajabu.
3 Gloria a su santo nombre. Que se alegre el corazón de los que buscan a Yahvé.
Lishangilieni jina lake takatifu, mioyo ya wale wamtafutao Bwana na ifurahi.
4 Busca a Yahvé y su fuerza. Busca su rostro para siempre.
Mtafuteni Bwana na nguvu zake, utafuteni uso wake siku zote.
5 Acuérdate de las maravillas que ha hecho: sus maravillas, y los juicios de su boca,
Kumbuka matendo ya ajabu aliyoyafanya, miujiza yake na hukumu alizozitamka,
6 tú, descendiente de Abraham, su siervo, vosotros, hijos de Jacob, sus elegidos.
enyi wazao wa Abrahamu mtumishi wake, enyi wana wa Yakobo, wateule wake.
7 Él es Yahvé, nuestro Dios. Sus juicios están en toda la tierra.
Yeye ndiye Bwana Mungu wetu, hukumu zake zimo duniani pote.
8 Se ha acordado de su pacto para siempre, la palabra que ordenó a mil generaciones,
Hulikumbuka agano lake milele, neno ambalo aliamuru, kwa vizazi elfu,
9 el pacto que hizo con Abraham, su juramento a Isaac,
agano alilolifanya na Abrahamu, kiapo alichomwapia Isaki.
10 y se lo confirmó a Jacob por un estatuto; a Israel por un pacto eterno,
Alilithibitisha kwa Yakobo kuwa amri, kwa Israeli liwe agano la milele:
11 diciendo: “A ti te daré la tierra de Canaán, el lote de tu herencia”.
“Nitakupa wewe nchi ya Kanaani kuwa sehemu utakayoirithi.”
12 cuando no eran más que unos pocos hombres, sí, muy pocos, y extranjeros en ella.
Walipokuwa wachache kwa idadi, wachache sana na wageni ndani yake,
13 Iban de nación en nación, de un reino a otro pueblo.
walitangatanga kutoka taifa moja hadi jingine, kutoka ufalme mmoja hadi mwingine.
14 No permitió que nadie les hiciera mal. Sí, reprendió a los reyes por su bien,
Hakuruhusu mtu yeyote awaonee; kwa ajili yao aliwakemea wafalme, akisema:
15 “¡No toquen a mis ungidos! No hagas daño a mis profetas”.
“Msiwaguse niliowatia mafuta; msiwadhuru manabii wangu.”
16 Convocó una hambruna en la tierra. Destruyó los suministros de alimentos.
Akaiita njaa juu ya nchi na kuharibu chakula chao chote,
17 Envió a un hombre delante de ellos. José fue vendido como esclavo.
naye akatuma mtu mbele yao, Yosefu, aliyeuzwa kama mtumwa.
18 Le magullaron los pies con grilletes. Su cuello fue encerrado con grilletes,
Walichubua miguu yake kwa minyororo, shingo yake ilifungwa kwa chuma,
19 hasta el momento en que ocurrió su palabra, y la palabra de Yahvé le dio la razón.
hadi yale aliyotangulia kusema yalipotimia, hadi neno la Bwana lilipomthibitisha.
20 El rey envió y lo liberó, incluso el gobernante de los pueblos, y déjalo libre.
Mfalme alituma watu wakamfungua, mtawala wa watu alimwachia huru.
21 Lo hizo señor de su casa, y gobernante de todas sus posesiones,
Alimfanya mkuu wa nyumba yake, mtawala juu ya vyote alivyokuwa navyo,
22 para disciplinar a sus príncipes a su antojo, y para enseñar la sabiduría a sus mayores.
kuwaelekeza wakuu wa mfalme apendavyo na kuwafundisha wazee wake hekima.
23 Israel también llegó a Egipto. Jacob vivía en la tierra de Cam.
Kisha Israeli akaingia Misri, Yakobo akaishi kama mgeni katika nchi ya Hamu.
24 Aumentó su pueblo en gran medida, y los hizo más fuertes que sus adversarios.
Bwana aliwafanya watu wake kuzaana sana, akawafanya kuwa wengi sana kuliko adui zao,
25 Hizo que su corazón se volviera a odiar a su pueblo, para conspirar contra sus sirvientes.
ndiye aliigeuza mioyo yao iwachukie watu wake, wakatenda hila dhidi ya watumishi wake.
26 Envió a Moisés, su siervo, y Aarón, a quienes había elegido.
Akamtuma Mose mtumishi wake, pamoja na Aroni, aliyemchagua.
27 Hicieron milagros entre ellos, y maravillas en la tierra de Jamón.
Walifanya ishara zake za ajabu miongoni mwao, miujiza yake katika nchi ya Hamu.
28 Envió las tinieblas y las hizo oscuras. No se rebelaron contra sus palabras.
Alituma giza na nchi ikajaa giza, kwani si walikuwa wameyaasi maneno yake?
29 Convirtió sus aguas en sangre, y mató a sus peces.
Aligeuza maji yao kuwa damu, ikasababisha samaki wao kufa.
30 Su tierra se llenó de ranas, incluso en las habitaciones de sus reyes.
Nchi yao ilijaa vyura tele, ambao waliingia hadi kwenye vyumba vya kulala vya watawala wao.
31 Habló, y vinieron enjambres de moscas, y piojos en todas sus fronteras.
Alisema, yakaja makundi ya mainzi, na viroboto katika nchi yao yote.
32 Les dio granizo como lluvia, con un rayo en su tierra.
Alibadilisha mvua yao ikawa mvua ya mawe, yenye umeme wa radi nchini yao yote,
33 Hirió sus vides y también sus higueras, y destrozaron los árboles de su país.
akaharibu mizabibu yao na miti ya tini, na akaangamiza miti ya nchi yao.
34 Él habló, y las langostas vinieron con los saltamontes, sin número.
Alisema, nzige wakaja, tunutu wasio na idadi,
35 Se comieron todas las plantas de su tierra, y comieron el fruto de su tierra.
wakala kila jani katika nchi yao, wakala mazao ya ardhi yao.
36 También hirió a todos los primogénitos de su tierra, las primicias de toda su hombría.
Kisha akawaua wazaliwa wote wa kwanza katika nchi yao, matunda ya kwanza ya ujana wao wote.
37 Los sacó con plata y oro. No había una sola persona débil entre sus tribus.
Akawatoa Israeli katika nchi wakiwa na fedha na dhahabu nyingi, wala hakuna hata mmoja kutoka kabila zao aliyejikwaa.
38 Egipto se alegró cuando partieron, porque el miedo a ellos había caído sobre ellos.
Misri ilifurahi walipoondoka, kwa sababu hofu ya Israeli ilikuwa imewaangukia.
39 Extendió una nube como cobertura, fuego para dar luz en la noche.
Alitandaza wingu kama kifuniko, na moto kuwamulikia usiku.
40 Le pidieron, y trajo codornices, y los satisfizo con el pan del cielo.
Waliomba, naye akawaletea kware, akawashibisha kwa mkate wa mbinguni.
41 Abrió la roca y las aguas brotaron. Corrían como un río en los lugares secos.
Alipasua mwamba, maji yakabubujika, yakatiririka jangwani kama mto.
42 Porque se acordó de su santa palabra, y Abraham, su siervo.
Kwa maana alikumbuka ahadi yake takatifu, aliyompa Abrahamu mtumishi wake.
43 Sacó a su pueblo con alegría, su elegido con el canto.
Aliwatoa watu wake kwa furaha, wateule wake kwa kelele za shangwe,
44 Les dio las tierras de las naciones. Tomaron el trabajo de los pueblos en posesión,
akawapa nchi za mataifa, wakawa warithi wa mali wengine walikuwa wameitaabikia:
45 para que cumplan sus estatutos, y observar sus leyes. ¡Alabado sea Yah!
alifanya haya ili wayashike mausia yake na kuzitii sheria zake. Msifuni Bwana.