< Salmos 101 >
1 Un salmo de David. Cantaré a la bondad amorosa y a la justicia. A ti, Yahvé, te cantaré alabanzas.
Nitaimba uaminifu wa agano lako na hukumu; kwako, Ee Yahwe, Nitakuimbia sifa.
2 Tendré cuidado de vivir una vida irreprochable. ¿Cuándo vas a venir a verme? Caminaré dentro de mi casa con un corazón irreprochable.
Nitatembea katika njia ya uadilifu. Oh, ni lini utakuja kwangu? Nitatembea kwa uadilifu ndani ya nyumba yangu.
3 No pondré ninguna cosa vil ante mis ojos. Odio los actos de los hombres sin fe. No se aferrarán a mí.
Sitaweka matendo maovu mbele ya macho yangu; ninachukia uovu usio na maana; hauta shikamana nami.
4 Un corazón perverso estará lejos de mí. No tendré nada que ver con el mal.
Watu waliopotoka wataniacha mimi; mimi sichangamani na uovu.
5 Yo silenciaré a quien calumnie en secreto a su prójimo. No toleraré a quien es arrogante y engreído.
Nitamwangamiza yeyote amsengenyaye jirani yake kwa siri. Sitamvumilia yeyote mwenye kiburi.
6 Mis ojos estarán sobre los fieles de la tierra, para que habiten conmigo. El que camina de manera perfecta, me servirá.
Nitawachagua walio waaminifu katika nchi wakae upande wangu. Wale watembeao katika njia ya uhadilifu watanitumikia.
7 El que practica el engaño no habitará en mi casa. El que habla con falsedad no será establecido ante mis ojos.
Watu wadanganyifu hawatabaki ndani ya nyumba yangu; waongo hawatakaribishwa mbele ya macho yangu.
8 Mañana tras mañana, destruiré a todos los malvados de la tierra, para cortar a todos los obreros de la iniquidad de la ciudad de Yahvé.
Asubuhi hata asubuhi nitawaangamiza waovu wote kutoka nchini; nitawaondoa watendao maovu wote katika mji wa Yahwe.