< Proverbios 8 >
1 ¿No grita la sabiduría? ¿La comprensión no levanta la voz?
Je hekima haiti? Je ufahamu hapazi sauti yake?
2 En la cima de los lugares altos por cierto, donde los caminos se encuentran, ella se para.
Juu ya kilima kando ya barabara, kwenye njia panda, hekima anasimama.
3 Junto a las puertas, a la entrada de la ciudad, en las puertas de entrada, llora en voz alta:
Kando ya njia ya kuingilia mjini, karibu na milango ya mji, anaita kwa sauti.
4 “¡Os llamo a vosotros, hombres! Envío mi voz a los hijos de la humanidad.
Watu, ninawaita ninyi na ninapaza sauti yangu kwa wana wa wanadamu.
5 ¡Tú, simple, entiende la prudencia! ¡Necios, tened un corazón comprensivo!
Ninyi wajinga, jifunzeni hekima, na ninyi mnaochukia maarifa, lazima mjipatieni moyo wa ufahamu.
6 Escuchad, porque voy a hablar de cosas excelentes. La apertura de mis labios es para las cosas correctas.
Sikiliza na mimi nitasema mambo mazuri na nifumbuapo midomo yangu nitaongea haki.
7 Porque mi boca dice la verdad. La maldad es una abominación para mis labios.
Maana kinywa changu hunena uaminifu na midomo yangu huchukia uovu.
8 Todas las palabras de mi boca son en justicia. No hay nada torcido ni perverso en ellos.
Maneno ya kinywa changu yote ni haki; hakuna kilichogeuzwa wala kupotoshwa.
9 Todo está claro para el que entiende, derecho a los que encuentran el conocimiento.
Maneno yangu yote yamenyooka kwa yule mwenye kuelewa; maneno yangu ni haki kwa wale wanaotafuta maarifa.
10 Recibe mi instrucción antes que la plata, conocimiento más que el oro de la elección.
Chagua fundisho langu badala ya fedha na maarifa kuliko dhahabu safi.
11 Porque la sabiduría es mejor que los rubíes. Todas las cosas que se puedan desear no se pueden comparar con ella.
Maana mimi, hekima ni bora kuliko vito; hakuna unachokitamani kinaweza kulinganishwa na mimi.
12 “Yo, la sabiduría, he hecho de la prudencia mi morada. Descubra el conocimiento y la discreción.
Mimi, hekima, naishi kwa utaratibu, na ninamiliki maarifa na busara.
13 El temor a Yahvé es odiar el mal. Odio el orgullo, la arrogancia, el mal camino y la boca perversa.
Hofu ya Mungu ni kuchukia uovu- nachukia majivuno na kiburi, njia ya uovu, na kauli iliyopotoka- hivyo ninavichukia.
14 El consejo y el buen conocimiento son míos. Tengo comprensión y poder.
Ninaushauri mzuri na hekima sahihi; mimi ni busara; nguvu zipo kwangu.
15 Por mí reinan los reyes, y los príncipes decretan la justicia.
Kwa njia yangu wafalme hutawala- pia na waungwana, na wote ambao hutawala kwa haki.
16 Por mí gobiernan los príncipes, nobles, y todos los gobernantes justos de la tierra.
Kwa njia yangu wafalme hutawala na waungwana na wote wanaotawala kwa haki.
17 Yo amo a los que me aman. Los que me buscan con diligencia me encontrarán.
Nawapenda wale wanaonipenda, na wale wanaonitafuta kwa bidii, wataniona.
18 Conmigo están las riquezas, el honor, riqueza duradera y prosperidad.
Kwangu kunautajiri na heshima, utajiri wa kudumu na haki.
19 Mi fruto es mejor que el oro, sí, que el oro fino, mi rendimiento que la plata de elección.
Tunda langu ni bora kuliko dhahabu, bora hata kuliko dhahabu safi.
20 Yo ando en el camino de la justicia, en medio de los caminos de la justicia,
Ninazalisha kilicho bora kuliko fedha safi. Natembea katika njia ya haki,
21 para dar riqueza a los que me aman. Lleno sus tesoros.
katika mapito ambayo huelekea kwenye haki, ili niwape urithi wale wanaonipenda na kuzijaza hazina zao.
22 “Yahvé me poseyó en el comienzo de su obra, ante sus hazañas de antaño.
Yehova aliniumba tokea mwanzo- mwazoni mwa matendo yake ya nyakati za kale.
23 Fui establecido desde siempre, desde el principio, antes de que la tierra existiera.
Tokea enzi za kale niliwekwa katika nafasi- tokea kwanza, tokea mwanzo wa dunia.
24 Cuando no había profundidades, nací yo, cuando no había manantiales que abundaran en agua.
Kabla ya bahari, mimi nilizaliwa- kabla ya kuwepo chemchemi zenye maji tele.
25 Antes de que las montañas se asentaran en su lugar, antes de las colinas, nací yo;
Kabla ya milima na vilima kuwekwa, mimi nilizaliwa.
26 cuando aún no había hecho la tierra ni los campos, ni el principio del polvo del mundo.
Nilizaliwa kabla ya Yehova hajaiumba dunia wala makonde, hata mavumbi ya kwanza katika dunia.
27 Cuando estableció los cielos, yo estaba allí. Cuando estableció un círculo en la superficie de las profundidades,
Nilikuwepo alipoziimarisha mbingu, wakati alipochora mstari katika sura ya kilindi.
28 cuando estableció las nubes de arriba, cuando los manantiales de las profundidades se hicieron fuertes,
Nilikuwepo alipoimarisha anga la juu na wakati wa kutengeneza kina cha chemchemi.
29 cuando le dio al mar su límite, para que las aguas no violen su mandamiento, cuando marcó los cimientos de la tierra,
Nilikuwepo alipotengeneza mipaka ya bahari, ili maji yasisambae kuvuka pale alipoyaamuru, na wakati anaamuru misingi ya dunia sehemu ya kukaa.
30 entonces yo era el artesano a su lado. Era una delicia día a día, siempre regocijándose ante él,
Nilikuwa kando yake, kama fundistadi mkuu, na mimi nilikuwa furaha yake siku kwa siku, nikifurahi mbele zake daima.
31 regocijo en todo su mundo. Mi deleite fue con los hijos de los hombres.
Nilikuwa nikifurahi katika dunia yake yote na furaha yangu ilikuwa kwa wana wa wanadamu.
32 “Ahora, pues, hijos míos, escuchadme, porque son dichosos los que guardan mis caminos.
Na sasa, wanangu, nisikilizeni, maana wale wazishikao njia zangu watakuwa na furaha.
33 Escucha la instrucción y sé sabio. No lo rechaces.
Sikilizeni fundisho langu na mpate hekima; wala msilipuuze.
34 Dichoso el hombre que me escucha, vigilando diariamente a mis puertas, esperando en los puestos de mi puerta.
Anisikilizaye atakuwa na furaha- kila siku akitazama katika malango yangu, akinisubiri pembeni mwa milango ya masikani yangu.
35 Porque quien me encuentra, encuentra la vida, y obtendrá el favor de Yahvé.
Maana yeyote anionaye mimi, anapata uzima, naye atapata kibali kwa Yehova.
36 Pero el que peca contra mí hace daño a su propia alma. Todos los que me odian aman la muerte”.
Na yeyote asiyeniona mimi, hujiumiza mwenyewe, wote wanaonichukia hupenda mauti.