< Proverbios 31 >

1 Las palabras del rey Lemuel: la revelación que le enseñó su madre:
Maneno ya mfalme Lemueli - mausia aliyofundishwa na mama yake.
2 “¡Oh, hijo mío! ¡Oh, hijo de mi vientre! ¡Oh, hijo de mis votos!
Mwanangu nini? Na ni nini mwana wa tumbo langu? Na ni nini mwana wa nadhiri zangu?
3 No des tu fuerza a las mujeres, ni tus caminos a lo que destruye a los reyes.
Nguvu zako usiwape wanawake; au wenye kuharibu wafalme njia zako.
4 No es para reyes, Lemuel, no es para los reyes beber vino, ni que los príncipes digan: “¿Dónde está la bebida fuerte?
Lemueli, kunywa divai, siyo kwa ajili ya wafalme, wala kwa watawala kuuliza, “kileo kikali kiko wapi?”
5 para que no beban y se olviden de la ley, y pervierten la justicia debida a quien está afligido.
Kwa sababu kama watakunywa, watasahau sheria ni nini, na kupotosha haki za wote walioonewa.
6 Da de beber fuerte al que está a punto de perecer, y el vino a los amargados de alma.
Wape kileo kikali watu wanaopotea na mvinyo kwa wale wenye kutaabika kwa uchungu.
7 Que beba y se olvide de su pobreza, y no recordar más su miseria.
Atakunywa na kusahau umasikini wake na hataikumbuka taabu yake.
8 Abre la boca para el mudo, en la causa de todos los que quedan desolados.
Ongea kwa ajili yao wasioweza kuongea, kwa madai ya wote wanaopotea.
9 Abre tu boca, juzga con justicia, y servir de justicia a los pobres y necesitados”.
Ongea na uhukumu kwa vipimo vya haki na utetee dai la masikini na watu wahitaji.
10 ¿Quién puede encontrar una mujer digna? Porque su valor está muy por encima de los rubíes.
Mke hodari ni nani anaweza kumpata? Thamani yake ni zaidi kuliko vito.
11 El corazón de su marido confía en ella. No le faltará ganancia.
Moyo wa mume wake humwamini, na hatakuwa masikini.
12 Ella le hace el bien y no el mal, todos los días de su vida.
Humtendea mambo mema na wala si mabaya siku zote za maisha yake.
13 Busca lana y lino, y trabaja con entusiasmo con sus manos.
Huchagua sufu na kitani, na hufanya kazi yake ya mikono kwa furaha.
14 Es como los barcos mercantes. Ella trae su pan desde lejos.
Yupo kama meli za wafanyabiashara; huleta chakula chake kutoka mbali.
15 También se levanta cuando todavía es de noche, da comida a su casa, y porciones para sus sirvientas.
Huamka wakati wa usiku na kuwapa chakula watu wa kaya yake, na kugawa kazi kwa watumishi wake wa kike.
16 Considera un campo y lo compra. Con el fruto de sus manos, planta un viñedo.
Hulifikiria shamba na kulinunua, kwa tunda la mikono yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Ella arma su cintura con fuerza, y hace que sus brazos sean fuertes.
Yeye mwenyewe hujivika nguvu na kuimarisha mikono yake.
18 Ella percibe que su mercancía es rentable. Su lámpara no se apaga por la noche.
Huangalia ni kipi kitaleta faida nzuri kwake; usiku wote taa yake haizimishwi.
19 Pone las manos en la rueca, y sus manos sostienen el huso.
Mikono yake huiweka kwenye mpini wa kisokotea nyuzi na hushikilia kisokotea nyuzi.
20 Ella abre sus brazos a los pobres; sí, extiende sus manos a los necesitados.
Mkono wake huwafikia watu masikini; mikono yake huwafikia watu wahitaji.
21 No teme a la nieve por su casa, porque toda su casa está vestida de escarlata.
Haogopi theluji kwa ajili ya kaya yake, kwa maana nyumba yake yote imevika kwa nguo nyekundu.
22 Hace para sí misma alfombras de tapiz. Su ropa es de lino fino y de color púrpura.
Hutengeneza matandiko ya kitanda chake, na huvaa nguo za kitani ya dhambarau safi.
23 Su marido es respetado en las puertas, cuando se siente entre los ancianos de la tierra.
Mume wake anajulikana malangoni, anapoketi na wazee wa nchi.
24 Ella hace prendas de lino y las vende, y entrega las fajas al comerciante.
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, na naleta mishipi kwa wafanyabiashara.
25 La fuerza y la dignidad son su vestimenta. Se ríe de la hora que viene.
Amevaa nguvu na heshima, na wakati ujao huucheka.
26 Ella abre su boca con sabiduría. La instrucción amable está en su lengua.
Anafumbua kinywa chake kwa hekima na sheria ya ukarimu ipo kwenye ulimi wake.
27 Ella mira bien los caminos de su casa, y no come el pan de la ociosidad.
Huangalia njia za nyumba yake na hawezi kula mkate wa uvivu.
28 Sus hijos se levantan y la llaman bendita. Su marido también la elogia:
Watoto wake huinuka na kumwita heri na mume wake humsifia, akisema,
29 “Muchas mujeres hacen cosas nobles, pero tú los superas a todos”.
“Wanawake wengi wamefanya vizuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 El encanto es engañoso, y la belleza es vana; pero la mujer que teme a Yahvé, será alabada.
Madaha ni udanganyifu, uzuri ni ubatili; bali mwanamke amchaye Yehova, atasifiwa.
31 ¡Dale del fruto de sus manos! ¡Que sus obras la alaben en las puertas!
Mpeni tunda la mikono yake na kazi zake zimsifu katika malango.

< Proverbios 31 >