< Proverbios 31 >
1 Las palabras del rey Lemuel: la revelación que le enseñó su madre:
Misemo ya Mfalme Lemueli, usia wa mama yake aliyomfundisha:
2 “¡Oh, hijo mío! ¡Oh, hijo de mi vientre! ¡Oh, hijo de mis votos!
“Ee mwanangu, ee mwana wa tumbo langu, ee mwana wa nadhiri zangu,
3 No des tu fuerza a las mujeres, ni tus caminos a lo que destruye a los reyes.
Usitumie nguvu zako kwa wanawake, uhodari wako kwa wale wanaowaharibu wafalme.
4 No es para reyes, Lemuel, no es para los reyes beber vino, ni que los príncipes digan: “¿Dónde está la bebida fuerte?
“Ee Lemueli, haifai wafalme, haifai wafalme kunywa mvinyo, haifai watawala kutamani sana kileo,
5 para que no beban y se olviden de la ley, y pervierten la justicia debida a quien está afligido.
wasije wakanywa na kusahau vile sheria inavyoamuru na kuwanyima haki zao wote walioonewa.
6 Da de beber fuerte al que está a punto de perecer, y el vino a los amargados de alma.
Wape kileo wale wanaoangamia, mvinyo wale walio na uchungu,
7 Que beba y se olvide de su pobreza, y no recordar más su miseria.
Wanywe na kusahau umaskini wao na wasikumbuke taabu yao tena.
8 Abre la boca para el mudo, en la causa de todos los que quedan desolados.
“Sema kwa ajili ya wale wasioweza kujisemea, kwa ajili ya haki za wote walioachwa ukiwa.
9 Abre tu boca, juzga con justicia, y servir de justicia a los pobres y necesitados”.
Sema na uamue kwa haki, tetea haki za maskini na wahitaji.”
10 ¿Quién puede encontrar una mujer digna? Porque su valor está muy por encima de los rubíes.
Mke mwenye sifa nzuri, ni nani awezaye kumpata? Yeye ni wa thamani sana kuliko marijani.
11 El corazón de su marido confía en ella. No le faltará ganancia.
Mume wake anamwamini kikamilifu wala hakosi kitu chochote cha thamani.
12 Ella le hace el bien y no el mal, todos los días de su vida.
Humtendea mumewe mema, wala si mabaya, siku zote za maisha yake.
13 Busca lana y lino, y trabaja con entusiasmo con sus manos.
Huchagua sufu na kitani naye hufanya kazi kwa mikono yenye bidii.
14 Es como los barcos mercantes. Ella trae su pan desde lejos.
Yeye ni kama meli za biashara akileta chakula chake kutoka mbali.
15 También se levanta cuando todavía es de noche, da comida a su casa, y porciones para sus sirvientas.
Yeye huamka kungali bado giza huwapa jamaa yake chakula na mafungu kwa watumishi wake wa kike.
16 Considera un campo y lo compra. Con el fruto de sus manos, planta un viñedo.
Huangalia shamba na kulinunua, kutokana na mapato yake hupanda shamba la mizabibu.
17 Ella arma su cintura con fuerza, y hace que sus brazos sean fuertes.
Hufanya kazi zake kwa nguvu, mikono yake ina nguvu kwa ajili ya kazi zake.
18 Ella percibe que su mercancía es rentable. Su lámpara no se apaga por la noche.
Huona kwamba biashara yake ina faida, wala taa yake haizimiki usiku.
19 Pone las manos en la rueca, y sus manos sostienen el huso.
Huweka mikono yake kwenye pia, navyo vidole vyake hushikilia kijiti chenye uzi.
20 Ella abre sus brazos a los pobres; sí, extiende sus manos a los necesitados.
Huwanyooshea maskini mikono yake na kuwakunjulia wahitaji vitanga vyake.
21 No teme a la nieve por su casa, porque toda su casa está vestida de escarlata.
Theluji ishukapo, hana hofu kwa ajili ya watu wa nyumbani mwake, kwa maana wote wamevikwa nguo za kutia joto.
22 Hace para sí misma alfombras de tapiz. Su ropa es de lino fino y de color púrpura.
Hutengeneza mazulia ya urembo ya kufunika kitanda chake, yeye huvaa kitani safi na urujuani.
23 Su marido es respetado en las puertas, cuando se siente entre los ancianos de la tierra.
Mume wake anaheshimiwa kwenye lango la mji, aketipo miongoni mwa wazee wa nchi.
24 Ella hace prendas de lino y las vende, y entrega las fajas al comerciante.
Hutengeneza mavazi ya kitani na kuyauza, naye huwauzia wafanyabiashara mishipi.
25 La fuerza y la dignidad son su vestimenta. Se ríe de la hora que viene.
Amevikwa nguvu na heshima, anaweza kucheka bila kuwa na hofu kwa siku zijazo.
26 Ella abre su boca con sabiduría. La instrucción amable está en su lengua.
Huzungumza kwa hekima na mafundisho ya kuaminika yapo ulimini mwake.
27 Ella mira bien los caminos de su casa, y no come el pan de la ociosidad.
Huangalia mambo ya nyumbani mwake wala hali chakula cha uvivu.
28 Sus hijos se levantan y la llaman bendita. Su marido también la elogia:
Watoto wake huamka na kumwita aliyebarikiwa, mumewe pia humsifu, akisema:
29 “Muchas mujeres hacen cosas nobles, pero tú los superas a todos”.
“Wanawake wengi hufanya vitu vyenye sifa nzuri, lakini wewe umewapita wote.”
30 El encanto es engañoso, y la belleza es vana; pero la mujer que teme a Yahvé, será alabada.
Kujipamba ili kuvutia ni udanganyifu na uzuri unapita upesi, bali mwanamke anayemcha Bwana atasifiwa.
31 ¡Dale del fruto de sus manos! ¡Que sus obras la alaben en las puertas!
Mpe thawabu anayostahili, nazo kazi zake na zimletee sifa kwenye lango la mji.