< Proverbios 29 >

1 El que a menudo es reprendido y endurece su cuello será destruido de repente, sin remedio.
Mtu aliyepokea makaripio mengi lakini anashupaza shingo yake atavunjika ndani ya muda mfupi na hata pona.
2 Cuando los justos prosperan, el pueblo se alegra; pero cuando los malvados gobiernan, el pueblo gime.
Watenda mema wanapoongezeka, watu wanafurahi, bali wakati mtu mwovu anapotawala, watu huugua.
3 Quien ama la sabiduría alegra a su padre; pero un compañero de prostitutas despilfarra su riqueza.
Mwenye kupenda hekima baba yake anafurahi, bali anayeshikamana na makahaba huuharibu utajiri wake.
4 El rey, mediante la justicia, hace que la tierra sea estable, pero el que acepta sobornos lo derriba.
Mfalme huimarisha nchi kwa haki, bali mwenye kudai rushwa huirarua.
5 El hombre que adula a su prójimo extiende una red para sus pies.
Mtu anayejipendekeza kwa jirani yake anatandaza wavu kwenye miguu yake.
6 El hombre malvado está atrapado por su pecado, pero los justos pueden cantar y alegrarse.
Mtu mbaya hunaswa kwenye mtego wa dhambi yake mwenyewe, bali yeye atendaye haki huimba na kufurahi.
7 Los justos se preocupan por la justicia de los pobres. Los malvados no se preocupan por el conocimiento.
Atendaye haki hutetea madai ya masikini; mtu mwovu hafahamu maarifa kama hayo.
8 Los burlones agitan una ciudad, pero los hombres sabios apartan la ira.
Mwenye dhihaka huutia moto mji, bali wale wenye busara huigeuza ghadhabu.
9 Si un hombre sabio va a la corte con un hombre necio, el tonto se enfurece o se burla, y no hay paz.
Mtu mwenye busara anapojadiliana na mpumbavu, hughadhabika na kucheka, hakutakuwa na utulivu.
10 Los sanguinarios odian al hombre íntegro; y buscan la vida de los rectos.
Mkatili humchukia mwenye ukamilifu na hutafuta maisha ya mwenye haki.
11 Un tonto descarga toda su ira, pero un hombre sabio se controla a sí mismo.
Mpumabavu huonyesha hasira yake, bali mtu mwenye busara huishikilia na kujituliza mwenyewe.
12 Si un gobernante escucha las mentiras, todos sus funcionarios son malvados.
Kama matawala atazinagatia uongo, maafisa wake wote watakuwa waovu.
13 El pobre y el opresor tienen esto en común: Yahvé da la vista a los ojos de ambos.
Mtu masikini na mkandamizaji wanafanana, maana Yehova huyapa nuru macho yao wote.
14 El rey que juzga con justicia a los pobres, su trono se establecerá para siempre.
Kama mfalme atamhukumu masikini kwa uaminifu, kiti chake cha enzi kitaimarishwa milele.
15 La vara de la corrección da sabiduría, pero un niño abandonado a sí mismo causa vergüenza a su madre.
Fimbo na maonyo huleta hekima, bali mtoto huru mbali na makaripio humwaibisha mama yake.
16 Cuando los malvados aumentan, el pecado aumenta; pero los justos verán su caída.
Watu waovu wanapotawala, uovu huongezeka, bali wenye kutenda haki wataona anguko la watu waovu.
17 Corrige a tu hijo, y él te dará la paz; sí, traerá deleite a tu alma.
Mwadibishe mwanao naye atakupa pumziko; ataleta furaha katika maisha yako.
18 Donde no hay revelación, el pueblo abandona la contención; pero el que guarda la ley es bendecido.
Pasipo na maono ya kinabii watu huenda bila utaratibu, bali mwenye kuitunza sheria amebarikiwa.
19 Un siervo no puede ser corregido con palabras. Aunque lo entiende, no responde.
Mtumwa hawezi kurekebishwa kwa maneno, maana ingawa anaelewa, hakuna mwitikio.
20 ¿Ves a un hombre que se precipita en sus palabras? Hay más esperanza para un tonto que para él.
Je unamwona mtu mwenye haraka katika maneno yake? Kuna matumaini zaidi kwa mpumbavu kuliko kwake.
21 El que mima a su siervo desde la juventud hará que se convierta en un hijo al final.
Mwenye kumdekeza mtumwa wake tangu ujana, mwisho wake itakuwa taabu.
22 Un hombre enfadado suscita conflictos, y un hombre iracundo abunda en el pecado.
Mtu mwenye hasira huchochea ugomvi na bwana mwenye hasira sana hutenda dhambi nyingi.
23 La soberbia del hombre lo abate, pero uno de espíritu humilde gana honor.
Kiburi cha mtu humshusha chini, bali mwenye roho ya unyenyekevu atapewa heshima.
24 Quien es cómplice de un ladrón es enemigo de su propia alma. Presta juramento, pero no se atreve a declarar.
Anayeshirikiana na mwizi huyachukia maisha yake mwenyewe; husikia laana na wala hasemi chochote.
25 El miedo al hombre resulta ser una trampa, pero quien pone su confianza en Yahvé está a salvo.
Kumwogopa binadamu ni mtego, bali mwenye kumtumaini Yehova atalindwa.
26 Muchos buscan el favor del gobernante, pero la justicia del hombre viene de Yahvé.
Wengi huutafuta uso wa mtawala, bali kutoka kwa Yehova huja haki kwa ajili yake.
27 El hombre deshonesto detesta al justo, y los rectos en sus caminos detestan a los malvados.
Mtu dhalimu ni chukizo kwa wenye kutenda haki, bali mwenye njia ya haki ni chukizo kwa watu waovu.

< Proverbios 29 >