< Proverbios 26 >

1 Como la nieve en verano, y como la lluvia en la cosecha, por lo que el honor no es propio de un tonto.
Kama theluji wakati wa joto au mvua kwenye mavuno, ndivyo mpumbavu asivyostahili heshima.
2 Como un gorrión que revolotea, como una golondrina, para que la maldición inmerecida no llegue a su fin.
Kama shorowanda hurukaruka na kumeza wadudu wakati wa kuruka, ndivyo ilivyo laana isiyostahili haishuki.
3 El látigo es para el caballo, una brida para el burro, ¡y una vara para la espalda de los tontos!
Mjeledi ni kwa ajili ya farasi, hatamu kwa ajili ya punda na fimbo ni kwa ajili mgongo wa wapumbavu.
4 No respondas al necio según su necedad, para que no seáis también como él.
Usimjibu mpumbavu na kujiunga katika upumbavu wake, au utakuwa kama yeye.
5 Responde al necio según su necedad, para no ser sabio en sus propios ojos.
Mjibu mpumbavu na jiunge katika upumbavu wake, ili asiweze kuwa na busara katika macho yake mwenyewe.
6 El que envía un mensaje de la mano de un tonto es cortar los pies y beber con violencia.
Anayetuma ujumbe kwa mkono wa mpumbavu huikata miguu yake mwenyewe na kunywa vurugu.
7 Como las piernas de los cojos que cuelgan sueltas, así es una parábola en boca de los tontos.
Miguu ya kiwete inayoning'ia chini ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
8 Como quien ata una piedra en una honda, así es el que da honor a un tonto.
Kujaribisha jiwe kwenye kombeo ni sawa na kumpa heshima mpumbavu.
9 Como un arbusto de espinas que va a la mano de un borracho, así es una parábola en boca de los tontos.
Mwiba unaochoma kwenye mkono wa mlevi ni kama mithali kwenye kinywa cha wapumbavu.
10 Como un arquero que hiere a todos, así es el que contrata a un tonto o el que contrata a los que pasan.
Mpiga mishale anayejeruhi kila mtu ni kama mtu anayemwajiri mpumbavu au kila mtu anayepita karibu yake.
11 Como un perro que vuelve a su vómito, así es un tonto que repite su locura.
Kama mbwa anavyorudia matapishi yake, ndivyo alivyo mpumbavu anayerudia upuuzi wake.
12 ¿Ves a un hombre sabio en sus propios ojos? Hay más esperanza para un tonto que para él.
Je unamwona mtu mwenye busara katika macho yake mwenyewe? Mpumbavu anamatumaini zaidi kuliko yeye.
13 El perezoso dice: “¡Hay un león en el camino! Un león feroz recorre las calles”.
Mtu mvivu husema “Kuna simba kwenye barabara! Kuna simba katikati ya njia kuu!”
14 Mientras la puerta gira sobre sus goznes, también lo hace el perezoso en su cama.
Kama mlango unavyogeuka kwenye bawaba zake, ndivyo alivyo mtu mvivu kwenye kitanda chake.
15 El perezoso entierra su mano en el plato. Es demasiado perezoso para llevárselo a la boca.
Mtu mvivu hutia mkono wake kwenye sufuria na bado hana nguvu kuunyanyua kwenda kwenye kinywa chake.
16 El perezoso es más sabio a sus propios ojos que siete hombres que responden con discreción.
Mtu mvivu ni mwenye hekima kwenye macho yake mwenyewe kuliko watu saba wenye ufahamu.
17 Como quien agarra las orejas de un perro es el que pasa y se entromete en una disputa que no es la suya.
Kama mtu anayeshikilia masikio ya mbwa, ndivyo alivyo mpitajia anayepata hasira kwenye ugomvi ambao si wake.
18 Como un loco que dispara antorchas, flechas y muerte,
Kama mtu mwendawazimu anayetupa mishale,
19 es el hombre que engaña a su prójimo y dice: “¿No estoy bromeando?”
ndivyo alivyo ambaye humdanganya jirani yake na kusema, “Je sikuwa naongea utani?”
20 Por falta de leña se apaga el fuego. Sin chismes, una pelea se apaga.
Kwa kukosa kuni, moto huzimika; na pale pasipo na mmbea ugomvi hukoma.
21 Como los carbones a las brasas, y leña al fuego, así que es un hombre contencioso para encender el conflicto.
Mkaa ni kwa kuwasha makaa na kuni kwa ajili ya moto, ndivyo alivyo mtu mgomvi kwa kuwasha ugomvi.
22 Las palabras de un susurrador son como bocados delicados, bajan a las partes más internas.
Maneno ya mmbea ni kama chembe tamu; nazo zinashuka chini kwenye sehemu za ndani ya mwili.
23 Como escoria de plata en una vasija de barro son los labios de un ferviente con un corazón malvado.
Kioo kinachofunika chombo cha udongo ni kama midomo inayoungua na moyo mbaya.
24 El hombre malicioso se disfraza con sus labios, pero alberga el mal en su corazón.
Yule ambaye huwachukia wengine huficha hisia zake kwa midomo na hufunika uongo ndani yake mwenyewe.
25 Cuando su discurso es encantador, no le creas, porque hay siete abominaciones en su corazón.
Ataongea kwa huruma, lakini usimwamini, maana kuna machukizo saba kwenye moyo wake.
26 Su malicia puede ser ocultada por el engaño, pero su maldad será expuesta en la asamblea.
Ingawa chuki zake zimefunikwa kwa udanganyifu, uovu wake utakuwa wazi katika kusanyiko.
27 El que cava una fosa caerá en ella. Quien hace rodar una piedra, se vuelve contra él.
Anayechimba shimo atatumbukia ndani yake na jiwe litamsaga yule anayelisukuma.
28 La lengua mentirosa odia a los que hiere; y una boca halagadora trabaja la ruina.
Ulimi wa uongo huchukia watu unaowajeruhi na kinywa cha uongo husogeza karibu uharibifu.

< Proverbios 26 >