< Números 7 >
1 El día en que Moisés terminó de levantar el tabernáculo, lo ungió y lo santificó con todo su mobiliario, y el altar con todos sus utensilios, y los ungió y santificó;
Mose alipomaliza kuisimamisha Maskani, aliitia mafuta na kuiweka wakfu pamoja na samani zake zote. Pia alitia madhabahu mafuta na kuiweka wakfu, pamoja na vyombo vyake vyote.
2 los príncipes de Israel, los jefes de las casas de sus padres, dieron ofrendas. Estos eran los príncipes de las tribus. Estos son los que estaban sobre los contados;
Ndipo viongozi wa Israeli, wale wakuu wa jamaa waliokuwa viongozi wa kabila wasimamizi wa wale waliohesabiwa, wakatoa sadaka.
3 y trajeron su ofrenda ante Yahvé, seis carros cubiertos y doce bueyes; un carro por cada dos de los príncipes, y por cada uno un buey. Los presentaron ante el tabernáculo.
Walizileta kama matoleo yao mbele za Bwana: magari sita ya kukokotwa yaliyofunikwa, pamoja na maksai kumi na wawili; yaani maksai mmoja kutoka kwa kila kiongozi, na gari moja la kukokotwa kutoka kwa kila viongozi wawili. Haya waliyaleta mbele ya Maskani.
4 Yahvé habló a Moisés, diciendo:
Bwana akamwambia Mose,
5 “Acéptalos de ellos, para que sean utilizados en el servicio de la Tienda de Reunión; y los darás a los levitas, a cada uno según su servicio.”
“Vikubali vitu hivi kutoka kwao, ili viweze kutumika katika kazi kwenye Hema la Kukutania. Wapatie Walawi kama kazi ya kila mtu itakavyohitaji.”
6 Moisés tomó los carros y los bueyes y los entregó a los levitas.
Hivyo Mose akachukua yale magari ya kukokotwa pamoja na maksai, na kuwapa Walawi.
7 Dio dos carros y cuatro bueyes a los hijos de Gersón, según su servicio.
Aliwapa Wagershoni magari mawili ya kukokotwa na maksai wanne, kama walivyohitaji kwa kazi yao,
8 A los hijos de Merari les dio cuatro carros y ocho bueyes, según su servicio, bajo la dirección de Itamar, hijo del sacerdote Aarón.
na pia aliwapa Wamerari magari manne ya kukokotwa na maksai wanane, kama kazi yao ilivyohitaji. Wote walikuwa chini ya maelekezo ya Ithamari mwana wa kuhani, Aroni.
9 Pero a los hijos de Coat no les dio ninguno, porque el servicio del santuario les correspondía a ellos; lo llevaban sobre sus hombros.
Lakini Mose hakuwapa Wakohathi chochote kati ya hivyo, kwa sababu walitakiwa kubeba vitu vitakatifu mabegani mwao, vile walikuwa wanawajibika.
10 Los príncipes dieron ofrendas para la dedicación del altar el día en que fue ungido. Los príncipes dieron sus ofrendas ante el altar.
Wakati madhabahu yalitiwa mafuta, viongozi walileta sadaka zao kwa ajili ya kule kuwekwa wakfu kwake na kuziweka mbele ya madhabahu.
11 Yahvé dijo a Moisés: “Ofrecerán su ofrenda, cada príncipe en su día, para la dedicación del altar”.
Kwa maana Bwana alikuwa amemwambia Mose, “Kila siku kiongozi mmoja ataleta sadaka yake ili kuwekwa wakfu madhabahu.”
12 El que ofreció su ofrenda el primer día fue Naasón hijo de Aminadab, de la tribu de Judá,
Yule ambaye alileta sadaka yake siku ya kwanza alikuwa Nashoni, mwana wa Aminadabu, wa kabila la Yuda.
13 y su ofrenda fue: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka yake ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
14 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
15 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
16 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
17 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Naasón, hijo de Aminadab.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nashoni mwana wa Aminadabu.
18 El segundo día, Netanel hijo de Zuar, príncipe de Isacar, presentó su ofrenda.
Siku ya pili yake Nethaneli mwana wa Suari, kiongozi wa kabila la Isakari, alileta sadaka yake.
19 Ofreció por su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
20 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
21 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
22 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
23 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos, cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Natanel, hijo de Zuar.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Nethaneli mwana wa Suari.
24 Al tercer día Eliab hijo de Helón, príncipe de los hijos de Zabulón,
Siku ya tatu Eliabu mwana wa Heloni, kiongozi wa kabila la Zabuloni, alileta sadaka yake.
25 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
26 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
27 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
28 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
29 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Eliab, hijo de Helón.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliabu mwana wa Heloni.
30 El cuarto día Elizur, hijo de Sedeur, príncipe de los hijos de Rubén,
Siku ya nne Elisuri mwana wa Shedeuri, kiongozi wa kabila la Reubeni, alileta sadaka yake.
31 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
32 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
33 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
34 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
35 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Elizur, hijo de Sedeur.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elisuri mwana wa Shedeuri.
36 El quinto día, Selumiel, hijo de Zurishaddai, príncipe de los hijos de Simeón,
Siku ya tano Shelumieli mwana wa Surishadai, kiongozi wa watu wa Simeoni, alileta sadaka yake.
37 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
38 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
39 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
40 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
41 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año: esta fue la ofrenda de Selumiel, hijo de Zurishaddai.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Shelumieli mwana wa Surishadai.
42 Al sexto día, Eliasaf hijo de Deuel, príncipe de los hijos de Gad,
Siku ya sita Eliasafu mwana wa Deueli, kiongozi wa watu wa Gadi, alileta sadaka yake.
43 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
44 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
45 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
46 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
47 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Eliasaf, hijo de Deuel.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Eliasafu mwana wa Deueli.
48 El séptimo día Elishama, hijo de Ammihud, príncipe de los hijos de Efraín,
Siku ya saba Elishama mwana wa Amihudi, kiongozi wa watu wa Efraimu, alileta sadaka yake.
49 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
50 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
51 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
52 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
53 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Elisama, hijo de Amiud.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Elishama mwana wa Amihudi.
54 El octavo día Gamaliel, hijo de Pedasur, príncipe de los hijos de Manasés,
Siku ya nane Gamalieli mwana wa Pedasuri, kiongozi wa watu wa Manase, alileta sadaka yake.
55 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
56 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
57 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
58 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
59 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Gamaliel, hijo de Pedasur.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Gamalieli mwana wa Pedasuri.
60 El noveno día Abidán hijo de Gedeón, príncipe de los hijos de Benjamín,
Siku ya tisa Abidani mwana wa Gideoni, kiongozi wa watu wa Benyamini, alileta sadaka yake.
61 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
62 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
63 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
64 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
65 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Abidán, hijo de Gedeón.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Abidani mwana wa Gideoni.
66 El décimo día Ahiezer hijo de Amisadai, príncipe de los hijos de Dan,
Siku ya kumi Ahiezeri mwana wa Amishadai, kiongozi wa watu wa Dani, alileta sadaka yake.
67 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
68 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
69 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
70 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
71 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Ahiezer hijo de Amisadai.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahiezeri mwana wa Amishadai.
72 El undécimo día Pagiel, hijo de Ocrán, príncipe de los hijos de Aser,
Siku ya kumi na moja Pagieli mwana wa Okrani, kiongozi wa watu wa Asheri, alileta sadaka yake.
73 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
74 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
75 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
76 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
77 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Pagiel, hijo de Ocrán.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Pagieli mwana wa Okrani.
78 El duodécimo día Ahira, hijo de Enán, príncipe de los hijos de Neftalí,
Siku ya kumi na mbili Ahira mwana wa Enani, kiongozi wa watu wa Naftali, alileta sadaka yake.
79 dio su ofrenda: una bandeja de plata, cuyo peso era de ciento treinta siclos, un cuenco de plata de setenta siclos, según el siclo del santuario, ambos llenos de harina fina mezclada con aceite para una ofrenda de harina;
Sadaka aliyoleta ilikuwa sahani moja ya fedha yenye uzito wa shekeli 130, na bakuli moja la fedha la kunyunyizia lenye uzito wa shekeli sabini, vyote kulingana na shekeli ya mahali patakatifu, vikiwa vimejazwa unga laini uliochanganywa na mafuta kama sadaka ya nafaka;
80 un cazo de oro de diez siclos, lleno de incienso;
sinia moja la dhahabu lenye uzito wa shekeli kumi, likiwa limejazwa uvumba;
81 un becerro joven, un carnero, un cordero macho de un año, para el holocausto;
fahali mmoja mchanga, kondoo dume mmoja na mwana-kondoo dume mmoja wa mwaka mmoja, kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa;
82 un macho cabrío como ofrenda por el pecado;
mbuzi dume mmoja kwa ajili ya sadaka ya dhambi;
83 y para el sacrificio de las ofrendas de paz, dos cabezas de ganado, cinco carneros, cinco machos cabríos y cinco corderos de un año. Esta fue la ofrenda de Ahira, hijo de Enán.
maksai wawili, kondoo dume watano, mbuzi dume watano na wana-kondoo dume watano wa mwaka mmoja, ili vitolewe dhabihu kama sadaka ya amani. Hii ndiyo ilikuwa sadaka ya Ahira mwana wa Enani.
84 Esta fue la ofrenda de dedicación del altar, el día en que fue ungido, por los príncipes de Israel: doce fuentes de plata, doce tazones de plata, doce cucharones de oro;
Hizi ndizo zilikuwa sadaka za viongozi wa Israeli madhabahu yalipowekwa wakfu, wakati yalitiwa mafuta: sahani kumi na mbili za fedha, bakuli kumi na mbili za fedha za kunyunyizia, na masinia kumi na mawili ya dhahabu.
85 cada fuente de plata pesaba ciento treinta siclos, y cada tazón setenta; toda la plata de los utensilios dos mil cuatrocientos siclos, según el siclo del santuario;
Kila sahani ya fedha ilikuwa na uzito wa shekeli 130, na kila bakuli la fedha la kunyunyizia lilikuwa na uzito wa shekeli sabini. Masinia yote kumi na mawili yalikuwa na uzito wa shekeli 2,400kulingana na shekeli ya mahali patakatifu.
86 los doce cucharones de oro, llenos de incienso, pesaban diez siclos cada uno, según el siclo del santuario; todo el oro de los cucharones pesaba ciento veinte siclos;
Sahani kumi na mbili za dhahabu zilizojazwa uvumba zilikuwa na uzito wa shekeli kumi kila moja, kulingana na shekeli ya mahali patakatifu. Kwa jumla, sahani za dhahabu zilikuwa na uzito wa shekeli 120.
87 todo el ganado para el holocausto, doce becerros, los carneros doce, los corderos machos de un año doce, y su ofrenda de comida; y doce machos cabríos para la ofrenda por el pecado;
Jumla ya wanyama waliotolewa kwa ajili ya sadaka ya kuteketezwa walikuwa fahali kumi na wawili wachanga, kondoo dume kumi na wawili na wana-kondoo dume kumi na wawili wa mwaka mmoja, pamoja na sadaka zao za nafaka. Mbuzi waume kumi na wawili walitolewa kwa ajili ya sadaka za dhambi.
88 y todo el ganado para el sacrificio de las ofrendas de paz: veinticuatro becerros, sesenta carneros, sesenta machos cabríos y sesenta corderos de un año. Esta fue la ofrenda de dedicación del altar, después de ser ungido.
Jumla ya wanyama kwa ajili ya dhabihu ya sadaka ya amani walikuwa maksai ishirini na wanne, kondoo dume sitini, mbuzi dume wa mwaka mmoja sitini na wana-kondoo dume wa mwaka mmoja sitini. Hizi ndizo zilikuwa sadaka zilizoletwa kwa ajili ya kuwekwa wakfu kwa madhabahu baada ya kutiwa mafuta.
89 Cuando Moisés entró en la Tienda del Encuentro para hablar con Yahvé, oyó su voz que le hablaba desde lo alto del propiciatorio que estaba sobre el arca del Testimonio, desde entre los dos querubines; y le habló.
Mose alipoingia kwenye Hema la Kukutania kuzungumza na Bwana, alisikia sauti ikisema naye kutoka kati ya wale makerubi wawili waliokuwa juu ya kile kiti cha rehema, juu ya Sanduku la Ushuhuda. Mose akazungumza naye.