< Números 33 >

1 Estos son los viajes de los hijos de Israel, cuando salieron de la tierra de Egipto con sus ejércitos bajo la mano de Moisés y Aarón.
Hizi ndizo safari za wana wa Israeli hapo walipotoka katika nchi ya Misri pamoja na makundi yao ya kijeshi chini ya uongozi wa Musa na Haruni.
2 Moisés escribió los puntos de partida de sus viajes por mandato de Yahvé. Estos son sus viajes según sus puntos de partida.
Musa aliandika maeneo yote tangu walipoondoka mpaka walipofika, kama alivyoamuriwa na BWANA. Hizi ndizo safari zao kama kutoka kwao kulivyokuwa kwa kila walipotoka.
3 Partieron de Ramsés en el primer mes, el día quince del primer mes; al día siguiente de la Pascua, los hijos de Israel salieron con la mano en alto a la vista de todos los egipcios,
Mwezi wa kwanza walisafiri kutoka Ramesi, waliondoka siku ya kumi na tano. Asubuhi siku iliyofuata baada ya Pasaka, Wana wa Israeli waliondoka wazi wazi, mbele ya machoya Wamisri wote.
4 mientras los egipcios enterraban a todos sus primogénitos, a los que Yahvé había herido entre ellos. Yahvé también ejecutó juicios sobre sus dioses.
Hii ilitokea wakati Wamisiri walipokuwa wakizika wazaliwa wao wa kwanza, ambao BWANA alikuwa amewaua miongoni mwao, kwa kuwa pia alikuwa ameiadhibu miungu yao.
5 Los hijos de Israel partieron de Ramsés y acamparon en Sucot.
Wana wa Israeli walisafiri kutoka Ramesi na kuweka kambi
6 Partieron de Sucot y acamparon en Etam, que está en el límite del desierto.
Sukothi. Walisafiri toka Sukothi na kuweka kambi Ethamu, mwisho wa nyika.
7 Partieron de Etam y volvieron a Pihahiroth, que está frente a Baal Zephon, y acamparon frente a Migdol.
Wakasafiri kutoka Ethamu wakarudi mpaka Pi-Hahirothi, ambayo inaikabili Baali Zephoni, ambapo waliweka kambi kuikabili Migidoli
8 Partieron de delante de Hahirot y cruzaron por el medio del mar hacia el desierto. Recorrieron tres días de camino en el desierto de Etam, y acamparon en Mara.
Kisha wakasafiri toka mkabala wa Pi-Hairothi na kupita katikati ya bahari kuelekea nyikani. Wakasafiri safari ya siku tatu katika nyika ya Ethamu na kuweka kambi Mara.
9 Partieron de Mara y llegaron a Elim. En Elim había doce fuentes de agua y setenta palmeras, y acamparon allí.
Wakasafiri kutoka Mara kufika Elimu. Pale Elimu kulikuwa na chemichemi kumi na mbili za maji na miti sabini ya mitende. hapo ndipo walipoweka kambi.
10 Partieron de Elim y acamparon junto al Mar Rojo.
Walisafiri kutoka Elimu na kuweka kambi karibu na Bahari ya Shamu.
11 Partieron del Mar Rojo y acamparon en el desierto de Sin.
Walisafiri kutoka Bahari ya Shamu na kuweka kambi katika nyika ya Sini.
12 Partieron del desierto de Sin y acamparon en Dolca.
Walisafiri kutoka nyika ya Sini na kuweka kambi Dofka.
13 Partieron de Dolca y acamparon en Alus.
Wakasafiri kutoka Dofka na kuweka kambi Alushi.
14 Partieron de Alus y acamparon en Refidim, donde no había agua para que el pueblo bebiera.
Wakasafiri kutoka Alushi na kuweka kambi Refidimu, ambapo watu walikosa maji ya kunywa.
15 Partieron de Refidim y acamparon en el desierto de Sinaí.
Walisafiri kutoka Refidimu na kuweka kambi kwenye nyika ya Sinai.
16 Partieron del desierto de Sinaí y acamparon en Kibroth Hattaava.
Walisafiri kutoka nyika ya Sinai na kuweka kambi Kibrothi Hataava.
17 Partieron de Kibroth Hattaava y acamparon en Hazerot.
Walisafiri kutoka Kibrothi Hataava na kuweka kambi Hazerothi.
18 Partieron de Hazerot y acamparon en Ritma.
Walisafiri kutoka Hazerothi na kuweka kambi Rithima.
19 Partieron de Ritma y acamparon en Rimón Fares.
Walisafiri kutoka Rithima na kuweka kambi Rimoni Perezi.
20 Partieron de Rimón Fares y acamparon en Libná.
Walisafiri kutoka Rimoni Perezi na kuweka kambi Libna.
21 Partieron de Libná y acamparon en Rissá.
Walisafiri kutoka Libna na kuweka kambi Risa.
22 Partieron de Rissá y acamparon en Ceeletá.
Walisafiri kutoka Risa na kuweka kambi Kehelatha.
23 Partieron de Ceeletá y acamparon en el monte Sefer.
Walisafiri kutoka Kehelatha na kuweka kambi kwenye Mlima Sheferi.
24 Partieron del monte Sefer y acamparon en Harada.
Walisafiri kutoka Mlima Sheferi na kuweka kambi Harada.
25 Partieron de Harada y acamparon en Macelot.
Walisafiri kutoka Harada na kuweka kambi Makelothi.
26 Partieron de Macelot y acamparon en Tahat.
Walisafiri kutoka Makelothi na kuweka kambi Tahathi.
27 Partieron de Tahat y acamparon en Taré.
Walisafiri kutoka Ttahalathi na kuweka kambi Tera.
28 Partieron de Taré y acamparon en Mitcá.
Walisafiri kutokaTera na kuweka kambi Mithika.
29 Partieron de Mitca y acamparon en Hasmona.
Walisafiri kutoka Mithika na kuweka kambi Hashimona.
30 Partieron de Hasmona y acamparon en Moserot.
Walisafiri kutoka Hashimona na kuweka kambi Moserothi.
31 Partieron de Moserot y acamparon en Bene Jaacán.
Walisafiri kutoka Moserothi na kuweka kambi Bene Jaakani.
32 Partieron de Bene Jaacan y acamparon en Hor de Gidgad.
Walisafiri kutoka Bene Jaakani na kuweka kambi Hori Hagidigadi.
33 Partieron de Hor de Gidgad y acamparon en Jotbata.
Walisafiri kutoka Hori Hagidigadi na kuweka kambi Jotibatha.
34 Partieron de Jotbata y acamparon en Abrona.
Walisafiri kutoka Jotibatha na kuweka kambi Abrona.
35 Partieron de Abrona y acamparon en Ezión Geber.
Walisafiri kutoka Abrona na kuweka kambi Ezioni Geberi.
36 Partieron de Ezión Geber y acamparon en Cades, en el desierto de Zin.
Walisafiri toka Ezioini Geberi na kuweka kambi katika nyika ya Sini kule Kadeshi.
37 Partieron de Cades y acamparon en el monte Hor, en el límite de la tierra de Edom.
Walisafiri kutoka Kadeshi na kuweka kambi Mlima Hori, Pembezoni mwa nchi ya Edomu.
38 El sacerdote Aarón subió al monte Hor por orden de Yahvé y murió allí, en el cuadragésimo año después de que los hijos de Israel salieron de la tierra de Egipto, en el quinto mes, el primer día del mes.
Hapo ndipo Haruni kuhani alipoenda kwenye Mlima Hori kwa amri ya BWANA na kufa kule mwaka wa arobaini bada ya Wisraeli kutoka katika nchi ya Misri, katika siku ya kwanza ya mwezi wa tano.
39 Aarón tenía ciento veintitrés años cuando murió en el monte Hor.
Haruni alikuwa na umri wa mika 123 alipokufa pale juu ya Mlima Hori.
40 El rey cananeo de Arad, que vivía en el sur, en la tierra de Canaán, se enteró de la llegada de los hijos de Israel.
Wakanaani, mfalme wa Aradi, ambao waliishi kusini mwa nyika katika nchi ya Kanaani, walisikia juu ya ujio wa wana wa Israeli.
41 Partieron del monte Hor y acamparon en Zalmoná.
Walisafiri kutika Mlima Hori n a kuweka kambi Zalimona.
42 Partieron de Zalmoná y acamparon en Punón.
Walisafiri kutoka Zalimona na kuweka kambi Punoni.
43 Partieron de Punón y acamparon en Obot.
Walisafiri kutoka Punoni na kuweka kambi Obothi.
44 Partieron de Oboth y acamparon en Ije Abarim, en la frontera de Moab.
Walisafiri kutoka Obothi na kuweka kambi Abarimu, katika mpaka wa Moabu.
45 Partieron de Ije Abarim y acamparon en Dibón Gad.
Walisafiri kutoka Abarimu na kuweka kambi Diboni Gadi.
46 Partieron de Dibón Gad y acamparon en Almon Diblataim.
Walisafiri kutoka Diboni Gadi na kuweka kambi Alimoni Diblathaimu.
47 Partieron de Almon Diblataim y acamparon en los montes de Abarim, frente a Nebo.
Walisafiri kutoka Alimoni Diblathaimu na kuweka kambi kwenye milima ya Abarimu mkabala na Nebo.
48 Partieron de los montes de Abarim y acamparon en las llanuras de Moab, junto al Jordán, en Jericó.
Walisafiri kutoka mlima wa Abarimuna kuweka kambi kwenye nyanda za Moabu karibu na Yorodani huko Yeriko.
49 Acamparon junto al Jordán, desde Bet Jesimot hasta Abel Sitim, en las llanuras de Moab.
Waliweka kambi karibu na Yorodani, kutoka Bethi Jeshimothi mpaka Abeli Shitimu katika nyanda za Moabu.
50 Yahvé habló a Moisés en las llanuras de Moab, junto al Jordán de Jericó, diciendo:
Hapo BWANA alinenana Musa katika nyanda za Moabu karibu na Yorodani kule Yeriko akasema,
51 Habla a los hijos de Israel y diles: “Cuando paséis el Jordán a la tierra de Canaán,
“Nena na wana wa Israeli uwaambie. 'Mtakapovuka mto Yorodani kuingia Kanaani,
52 entonces expulsaréis a todos los habitantes de la tierra de delante de vosotros, destruiréis todos sus ídolos de piedra, destruiréis todas sus imágenes fundidas y derribaréis todos sus lugares altos.
ndipo mtakapowafukuza wenyeji wote mbele yenu. Mtaziharibu sanamu zote za kuchongwa. Mtaziharibu sanamu zao za kusubu na kuharibu mahali pao pote palipoinuka.
53 Tomarás posesión de la tierra y habitarás en ella, porque yo te he dado la tierra para que la poseas.
Mtachukua hiyo ardhi iwe mali yenu na muishi ndani yake, kwa sababu nimewapeni hiyo nchi iwe mali yenu.
54 Heredaréis la tierra por sorteo según vuestras familias; a los grupos más numerosos les darás una herencia mayor, y a los más pequeños les darás una herencia menor. Dondequiera que le toque la suerte a un hombre, eso será suyo. Heredaréis según las tribus de vuestros padres.
Mtairithi hiyo nchi kwa kupiga kura, kwa kufuata kila ukoo. Kwa zile koo kubwa kubwa mtawapa sehemu kubwa ya ardhi, na kwa zile koo ndogo ndogo mtawapa sehemu ndogo ya ardhi. Kura itakapoanguka kwenye kila ukoo, hiyo ardhi itakuwa mali yake. Mtairithi ardhi kufuata ukoo wa kabilla la jamaa zenu.
55 “Pero si no expulsas a los habitantes de la tierra de delante de ti, los que dejes que queden de ellos serán como aguijones en tus ojos y espinas en tus costados. Te acosarán en la tierra en la que habitas.
Lakini kama hamtawafukuza wenyeji wa nchi hiyo watoke mbele yenu, ndipo wale watu mtakaowaruhusu wakae nanyi watakapokuwa kama sindano machoni mwenu na miiba katika mbavu zenu. Watayafanya maisha yenu yawe magumu katika nchi mnayoishi.
56 Sucederá que, como pensaba hacerles a ellos, así os haré a vosotros”.
Ndipo itakapotokea kuwa kile ambacho Mimi ninakusudia kufanya kwa wale watu, Nitawafanyia pia ninyi'”

< Números 33 >