< Números 3 >
1 Esta es la historia de las generaciones de Aarón y Moisés en el día en que Yahvé habló con Moisés en el monte Sinaí.
Sasa hii ndiyo historia ya uzao wa Haruni na Musa wakati BWANA aliposema na Musa kwenye mlima Sinai.
2 Estos son los nombres de los hijos de Aarón: Nadab, el primogénito, y Abiú, Eleazar e Itamar.
Majina ya watoto wa Haruni walikuwa Nadabu ambaye ndiyo mtoto wa kwanza, na Abihu, na Eliezeri, na Ithamari.
3 Estos son los nombres de los hijos de Aarón, los sacerdotes que fueron ungidos, a quienes consagró para que ejercieran el ministerio sacerdotal.
Haya ndiyo majina ya wana wa Haruni, makuhani waliokuwa wamepakwa mafuta na kuwekwa wakfu kutumika kama makuhani.
4 Nadab y Abiú murieron ante Yahvé cuando ofrecieron fuego extraño ante Yahvé en el desierto de Sinaí, y no tuvieron hijos. Eleazar e Itamar ejercieron el ministerio sacerdotal en presencia de Aarón, su padre.
Lakini Nadabu na Abihu walikufa mbele ya BWANA walipomtolea moto usiokubalika walipokuwa katika nyika ya Sinai. Nadabu na Abihu hawakuwa na watoto, kwa hiyo Eliazari na Ithamari walitumika kama makuhani pamoja na baba yao.
5 Yahvé habló a Moisés, diciendo:
BWANA alinena na Musa, akamwambia,
6 “Haz que se acerque la tribu de Leví, y ponlos delante del sacerdote Aarón, para que le sirvan.
“Walete kabila ya Lawi na uwaweke kwa Haruni kuhani ili wamsaidie
7 Ellos guardarán sus requerimientos, y los requerimientos de toda la congregación ante la Tienda de Reunión, para hacer el servicio del tabernáculo.
Nao lazima wafanye majukumu badala ya Haruni na jumuiya yote mbele ya hema ya kukutania. Lazima watumike hemani.
8 Guardarán todo el mobiliario de la Tienda de reunión y las obligaciones de los hijos de Israel, para hacer el servicio del tabernáculo.
Watayatunza mapambo ya hema ya kukutania, na watawatumikia makabila ya Israel kwa huduma ya hemani.
9 Darás los levitas a Aarón y a sus hijos. Le serán entregados íntegramente en nombre de los hijos de Israel.
Uwaweke Walawi kwa Haruni na watoto wake. Nimewatoa kikamilifu ili wamsaidie kuwatumikia watu wa Israel.
10 Designarás a Aarón y a sus hijos, y ellos conservarán su sacerdocio, pero el extranjero que se acerque será condenado a muerte.”
Umchague Haruni na watoto wake kuwa makuhani, lakini mgeni yeyote atakayekaribia lazima auawe.”
11 Yahvé habló a Moisés, diciendo:
BWANA alinena na Musa. akamwambia,
12 “He aquí que he tomado a los levitas de entre los hijos de Israel en lugar de todos los primogénitos que abren el vientre entre los hijos de Israel; y los levitas serán míos,
“Tazama, nimewachagua Walawi katika watu wa Israel. Nimefanya hivyo badala ya kuchukua mzaliwa wa kwanza wa kiume wa wana wa Israel. Hawa Walawi ni wangu.
13 porque todos los primogénitos son míos. El día en que derribé a todos los primogénitos en la tierra de Egipto, santifiqué para mí a todos los primogénitos de Israel, tanto hombres como animales. Serán míos. Yo soy Yahvé”.
Na hata wazaliwa wa kwanza ni mali yangu. Katika siku ambyo niliwavamia wazaliwa wote wa kwanza wa nchi ya Misri, Niliwatenga wazaliwa wa kwanza wa Israeli kwa ajili yangu, watu na wanyama pia. Ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.”
14 Yahvé habló a Moisés en el desierto del Sinaí, diciendo:
BWANA alinena na Musa katika nyika ya Sinai. Akasema,
15 “Cuenta a los hijos de Leví por las casas de sus padres, por sus familias. Contarás a todos los varones de un mes en adelante”.
“Wahesabu uzao wa Lawi katika kila familia, katika nyumba za koo zao. Hesabu kila mume kuanzia mwezi mmoja au zaidi.”
16 Moisés los contó según la palabra de Yahvé, como se le había ordenado.
Musa aliwahesabu, kufuata maelekezo ya BWANA, kama alivyoamriwa kufanya.
17 Estos fueron los hijos de Leví por sus nombres: Gersón, Coat y Merari.
Majina ya watoto waLawi yalikuwa Gerishoni, Kohathi, na Merari.
18 Estos son los nombres de los hijos de Gersón por sus familias Libni y Simei.
Ukoo uliotokana na watoto wa Gerishoni walikuwa ni Libni na Shimei.
19 Los hijos de Coat por sus familias: Amram, Izhar, Hebrón y Uziel.
Ukoo uliotokana na watoto Kohathi walikuwa ni Amramu na, Izihari, Hebroni, na Uzieli.
20 Los hijos de Merari por sus familias: Mahli y Mushi. Estas son las familias de los levitas según las casas de sus padres.
Ukoo uliotokana na watoto wa Merari walikuwa ni Mahili na Mushi. Hizi ndizo koo za Walawi, zilizoorodheshwa ukoo kwa ukoo.
21 De Gersón era la familia de los libnitas, y la familia de los simeítas. Estas son las familias de los gersonitas.
Koo za Walibini na Washimei zilitokana na Wagerishoni. Hizi ndizo koo za Wagerishoni.
22 Los que fueron contados de ellos, según el número de todos los varones de un mes para arriba, fueron siete mil quinientos.
Wanaume wote wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa na kufikia idadi ya 7, 500.
23 Las familias de los gersonitas acamparán detrás del tabernáculo hacia el oeste.
Koo za Wagerishoni watapanga upande wa magharibi wa hema.
24 Eliasaf, hijo de Lael, será el príncipe de la casa paterna de los gersonitas.
Eliasafu mwana wa Laeli ataongoza koo za uzao wa Wagerishoni.
25 La tarea de los hijos de Gersón en la Tienda de reunión será el tabernáculo, la tienda, su cubierta, la cortina de la puerta de la Tienda de reunión,
Familia ya Gerishoni watalilinda hema la kukutania pamoja na hiyo masikani. Watalilinda hema, kifuniko chake, na lile pazia la lango la hema ya kukutania.
26 las cortinas del atrio, la cortina de la puerta del atrio que está junto al tabernáculo y alrededor del altar, y sus cuerdas para todo su servicio.
Wataulinda ua, lile pazia la kwenye lango—ua unaozunguka mahali patakatifu na madhabahu. Watazilinda kamba za hema ya kukutania na vyote vilivyomo.
27 De Coat era la familia de los amramitas, la familia de los izharitas, la familia de los hebronitas y la familia de los uzielitas. Estas son las familias de los coatitas.
Koo zifuatazo zinatokana na Kohathi: ukoo wa Waamrami, ukoo wa Waizihari ukoo wa Wahebroni, na ukoo wa Wauzieli. Koo hizi zinatokana na Wakohathi.
28 Según el número de todos los varones de un mes en adelante, había ocho mil seiscientos que cumplían con los requisitos del santuario.
Wanaume 8, 600 wenye umri wa mwezi mmoja au zaidi walihesabiwa ili kulinda vitu vya BWANA.
29 Las familias de los hijos de Coat acamparán al sur de la tienda.
Familia ya uzao wa Kohathi watapanga upande wa kusini wa Hema.
30 El príncipe de la casa paterna de las familias de Coat será Elizafán hijo de Uziel.
Elizafani mwana wa Uzieli ndiye atakayeongoza ukoo wa Wakohathi.
31 Su tarea será el arca, la mesa, el candelabro, los altares, los utensilios del santuario con los que se ministra, la cortina y todo su servicio.
Watalilinda sanduku, meza, vikalishio vya taa, madhabahu, vitu vitakatifu ambvyo hutumika katika huduma yao, pazia, na kazi zote zinazoambatana na hema.
32 Eleazar, hijo del sacerdote Aarón, será el príncipe de los príncipes de los levitas, con la supervisión de los que cumplen los requisitos del santuario.
Eliazari mwana wa Haruni kuhani atawaongoza wanaume wanaowaongoza Walawi. Atawasimamia wanaume wanaongoza eneo takatifu.
33 De Merari era la familia de los Musitas y la familia de los Mushitas. Estas son las familias de Merari.
Koo mbili zimetoka kwa Merari: Ukoo wa Mahili na ukoo wa Mushi. Koo hizi zimetokana na Merari,
34 Los contados de ellos, según el número de todos los varones de un mes para arriba, fueron seis mil doscientos.
Wanaume 6, 200 wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi walihesabiwa.
35 El príncipe de la casa paterna de las familias de Merari era Zuriel hijo de Abihail. Acamparán en el lado norte del tabernáculo.
Zurieli mwana wa Abihaili ataongoza ukoo wa Merari. Hawa watapanga upande wa kaskazini mwa hema.
36 La tarea asignada a los hijos de Merari será las tablas del tabernáculo, sus barras, sus pilares, sus bases, todos sus instrumentos, todo su servicio,
Uzao wa Merari utatunza mbao za hema, mataruma, nguzo, makalishio, viifaa vya ujenzi na vitu vyote vinavyohusika,
37 los pilares del atrio que lo rodea, sus bases, sus clavijas y sus cuerdas.
na nguzo za ua zinazozunguka hema, makalishio, vigingi na kamba zake.
38 Los que acampen delante del tabernáculo hacia el oriente, frente a la Tienda de Reunión hacia la salida del sol, serán Moisés, con Aarón y sus hijos, guardando los requisitos del santuario para el deber de los hijos de Israel. El forastero que se acerque será condenado a muerte.
Musa na Haruni na watoto wake watapanga upande wa mashariki wa masikani, mbele ya hema ya kukutania kuelekea mawio ya jua. Wao wataajibika na majukumu ya mahali patakatifu na majukumu ya wana wa Israeli. Mgeni atakayekaribia mahali patakatifu auawe.
39 Todos los contados de los levitas, que Moisés y Aarón contaron por orden de Yahvé, por sus familias, todos los varones de un mes en adelante, fueron veintidós mil.
Musa na Haruni wakawahesabu wanaume wote wa ukoo wa Walawi walikuwa na umri wa mwezi mmoja na zaidi, kama vile BWANA alivyokuwa ameagiza. Walihesabu wanaume ishirini na mbili elfu.
40 Yahvé dijo a Moisés: “Cuenta todos los primogénitos varones de los hijos de Israel de un mes en adelante, y toma la cuenta de sus nombres.
BWANA alisema na Musa, “Wahesabu wanaume wote ambo ni wazaliwa wa kwanza wa Israeli ambao wana umri wa mwezi mmoja na zaidi. Orodhesha majina yao.
41 Tomarás a los levitas para mí — yo soy Yahvé — en lugar de todos los primogénitos entre los hijos de Israel; y el ganado de los levitas en lugar de todos los primogénitos entre el ganado de los hijos de Israel.”
Unitwalie walawi kwa ajili yangu badala ya wazaliwa wa kwanza wa Israeli, Mimi ndimi BWANA. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wazaliwa wa kwanza wa wanyama wa uzao wa Israeli,”
42 Moisés contó, como le había ordenado Yahvé, todos los primogénitos de los hijos de Israel.
Musa akawahesabu wazaliwa wa kwanza wote wa Israeli kama BWANA alivyomwagiza kufanya.
43 Todos los primogénitos varones, según el número de nombres, de un mes para arriba, de los que fueron contados, fueron veintidós mil doscientos setenta y tres.
Aliwahesabu wazaliwa wote wa kwanza kwa mjina, wenye umri wa mwezi mmoja na zaidi. Alihesabu wanaume 22, 273.
44 Yahvé habló a Moisés diciendo:
Tena BWANA alinena na Musa. Akasema,
45 “Toma a los levitas en lugar de todos los primogénitos de los hijos de Israel, y el ganado de los levitas en lugar de su ganado; y los levitas serán míos. Yo soy Yahvé.
“Watwae Walawi badala ya wazaliwa wote wa kwanza wa wana wa Israeli. Na utwae wanyama wa Walawi badala ya wanyama wa Waisreli wengine. Walawi ni mali yangu. Mimi ndimi BWANA.
46 Para la redención de los doscientos setenta y tres primogénitos de los hijos de Israel que excedan el número de los levitas,
Unikusanyie shekeli tano za wokovu kwa kila hao 273 za hao wazaliwa wa kwanza wa Israeli za hao wanaozidi idadi ya Walawi.
47 tomarás cinco siclos por cada uno; según el siclo del santuario los tomarás (el siclo es de veinte gerahs);
Utazitumia hizo shekeli tano kwa kipimo cha mahali patakatifu. Shekeli moja ni sawa na gera ishirini.
48 y darás el dinero, con el que se redime su resto, a Aarón y a sus hijos.”
Utawalipa hizo shekeli za wokovu kwa Haruni na wanawe.”
49 Moisés tomó el dinero de la redención de los que excedían el número de los redimidos por los levitas;
Kwa hiyo Musa akakusanya shakeli za wokovu kutoka kwa wale waliozidi idadi ya wale waliookolewa na Walawi.
50 de los primogénitos de los hijos de Israel tomó el dinero, mil trescientos sesenta y cinco siclos, según el siclo del santuario;
Musa akakusanya zile fedha kutoka kwa hao wazaliwa wa kwanza wa wana wa Israeli. Alikusanya jumla ya shekeli 1, 365, zenye kipimo sawa na mahali patakatifu. Musa akamlipa Haruni na wanawe hizo shekeli za wokovu.
51 y Moisés dio el dinero de la redención a Aarón y a sus hijos, según la palabra de Yahvé, como Yahvé le ordenó a Moisés.
Musa akafanya kila kitu alichoagizwa na neno la BWANA kama BWANA alivyomwagiza.