< Nehemías 11 >

1 Los príncipes del pueblo vivían en Jerusalén. El resto del pueblo también echó suertes para que uno de los diez habitara en Jerusalén, la ciudad santa, y nueve partes en las demás ciudades.
Basi viongozi wa watu walikaa Yerusalemu, nao watu wale wengine walipiga kura ili kuleta mtu mmoja kati ya watu kumi aje kuishi Yerusalemu, mji mtakatifu, nao wengine tisa waliobaki wakae katika miji yao wenyewe.
2 El pueblo bendijo a todos los hombres que se ofrecieron voluntariamente para habitar en Jerusalén.
Watu waliwasifu wale wote waliojitolea kuishi Yerusalemu.
3 Estos son los jefes de la provincia que vivían en Jerusalén; pero en las ciudades de Judá, cada uno vivía en su posesión en sus ciudades: los sacerdotes, los levitas, los servidores del templo y los hijos de los servidores de Salomón.
Hawa ndio viongozi wa majimbo waliokuja kuishi Yerusalemu (baadhi ya Waisraeli, makuhani, Walawi, watumishi wa Hekalu, na wazao wa watumishi wa Solomoni waliendelea kuishi katika miji ya Yuda, kila mmoja katika milki yake mwenyewe katika miji mbalimbali,
4 Algunos de los hijos de Judá y de los hijos de Benjamín vivían en Jerusalén. De los hijos de Judá Ataías hijo de Uzías, hijo de Zacarías, hijo de Amarías, hijo de Sefatías, hijo de Mahalalel, de los hijos de Fares;
ambapo watu wengine kutoka Yuda na Benyamini waliishi Yerusalemu). Kutoka wazao wa Yuda: Athaya mwana wa Uzia, mwana wa Zekaria, mwana wa Amaria, mwana wa Shefatia, mwana wa Mahalaleli, mzao wa Peresi.
5 y Maasías hijo de Baruc, hijo de Colhoze, hijo de Hazaías, hijo de Adaías, hijo de Joiarib, hijo de Zacarías, hijo del silonita.
Naye Maaseya mwana wa Baruku, mwana wa Kolhoze, mwana wa Hazaya, mwana wa Adaya, mwana wa Yoyaribu, mwana wa Zekaria, mzao wa Mshiloni.
6 Todos los hijos de Fares que vivían en Jerusalén eran cuatrocientos sesenta y ocho hombres valientes.
Wazao wa Peresi walioishi Yerusalemu walikuwa 468, watu wenye uwezo.
7 Estos son los hijos de Benjamín: Salú, hijo de Mesulam, hijo de Joed, hijo de Pedaías, hijo de Colaías, hijo de Maasías, hijo de Itiel, hijo de Jesaías.
Kutoka wazao wa Benyamini: Salu mwana wa Meshulamu, mwana wa Yoedi, mwana wa Pedaya, mwana wa Kolaya, mwana wa Maaseya, mwana wa Ithieli, mwana wa Yeshaya
8 Después de él, Gabbai y Sallai, novecientos veintiocho.
na wafuasi wake, Gabai na Salai watu 928.
9 Joel hijo de Zicri era su supervisor; y Judá hijo de Hasenúa era el segundo sobre la ciudad.
Yoeli mwana wa Zikri alikuwa afisa wao mkuu, naye Yuda mwana wa Hasenua alikuwa msimamizi juu ya Mtaa wa Pili katika mji.
10 De los sacerdotes: Jedaías hijo de Joiarib, Jacín,
Kutoka makuhani: Yedaya, mwana wa Yoyaribu, Yakini,
11 Seraías hijo de Hilcías, hijo de Mesulam, hijo de Sadoc, hijo de Meraiot, hijo de Ahitub, jefe de la casa de Dios,
Seraya mwana wa Hilkia, mwana wa Meshulamu, mwana wa Sadoki, mwana wa Merayothi, mwana wa Ahitubu, msimamizi katika nyumba ya Mungu,
12 y sus hermanos que hacían la obra de la casa, ochocientos veintidós; y Adaías hijo de Jeroham, hijo de Pelalías, hijo de Amzi, hijo de Zacarías, hijo de Pashur, hijo de Malquías,
pamoja na wenzao waliofanya kazi hekaluni: watu 822. Adaya mwana wa Yerohamu, mwana wa Pelalia, mwana wa Amsi, mwana wa Zekaria, mwana wa Pashuri, mwana wa Malkiya,
13 y sus hermanos, jefes de las casas paternas, doscientos cuarenta y dos y Amashsai hijo de Azarel, hijo de Ahzai, hijo de Meshillemoth, hijo de Immer,
na wenzao, waliokuwa viongozi wa jamaa: watu 242. Amashisai mwana wa Azareli, mwana wa Azai, mwana wa Meshilemothi, mwana wa Imeri,
14 y sus hermanos, hombres valientes, ciento veintiocho; y su jefe era Zabdiel, hijo de Haggedolim.
na wenzao waliokuwa wenye uwezo: watu 128. Afisa wao mkuu alikuwa Zabdieli mwana wa Hagedolimu.
15 De los levitas Semaías hijo de Hasub, hijo de Azricam, hijo de Hasabías, hijo de Bunni;
Kutoka Walawi: Shemaya mwana wa Hashubu, mwana wa Azrikamu, mwana wa Hashabia, mwana wa Buni;
16 y Sabetai y Jozabad, de los jefes de los levitas, que tenían a su cargo los asuntos externos de la casa de Dios;
Shabethai na Yozabadi, viongozi wawili wa Walawi, ambao walisimamia kazi za nje za nyumba ya Mungu;
17 y Matanías hijo de Mica, hijo de Zabdi, hijo de Asaf, que era el jefe que iniciaba la acción de gracias en la oración, y Bacbuquías, el segundo entre sus hermanos; y Abda hijo de Sammúa, hijo de Galal, hijo de Jedutún.
Matania mwana wa Mika, mwana wa Zabdi, mwana wa Asafu, kiongozi aliyeongoza kutoa shukrani na maombi; Bakbukia aliyekuwa msaidizi wake kati ya wenzake; na Abda mwana wa Shamua, mwana wa Galali, mwana wa Yeduthuni.
18 Todos los levitas de la ciudad santa eran doscientos ochenta y cuatro.
Jumla ya Walawi waliokaa katika mji mtakatifu walikuwa watu 284.
19 Además, los guardianes de las puertas, Acub, Talmón y sus hermanos, que vigilaban las puertas, eran ciento setenta y dos.
Mabawabu: Akubu, Talmoni na wenzao, waliolinda malango: watu 172.
20 El resto de Israel, de los sacerdotes y de los levitas, estaban en todas las ciudades de Judá, cada uno en su heredad.
Waisraeli waliosalia, pamoja na makuhani na Walawi, walikuwa katika miji yote ya Yuda, kila mmoja katika urithi wa baba yake.
21 Pero los servidores del templo vivían en Ofel, y Ziha y Gishpa estaban al frente de los servidores del templo.
Watumishi wa Hekalu waliishi katika kilima cha Ofeli. Siha na Gishpa walikuwa wasimamizi wao.
22 El supervisor de los levitas en Jerusalén era Uzi hijo de Bani, hijo de Hasabías, hijo de Matanías, hijo de Mica, de los hijos de Asaf, los cantores, estaba a cargo de los asuntos de la casa de Dios.
Afisa mkuu wa Walawi huko Yerusalemu alikuwa Uzi mwana wa Bani, mwana wa Hashabia, mwana wa Matania, mwana wa Mika. Uzi alikuwa mmoja wa wazao wa Asafu, waliokuwa waimbaji wenye kuwajibika kwa ajili ya huduma ya nyumba ya Mungu.
23 Porque había un mandamiento del rey acerca de ellos, y una provisión establecida para los cantores, como cada día lo requería.
Waimbaji walikuwa chini ya amri za mfalme, ambazo pia ziliratibu shughuli zao za kila siku.
24 Petaías, hijo de Meshezabel, de los hijos de Zera, hijo de Judá, estaba al lado del rey en todos los asuntos del pueblo.
Pethahia mwana wa Meshezabeli, mmoja wa wazao wa Zera mwana wa Yuda, alikuwa mwakilishi wa mfalme katika mambo yote kuhusu mahusiano na watu.
25 En cuanto a las aldeas con sus campos, algunos de los hijos de Judá vivían en Quiriat Arba y sus pueblos, en Dibón y sus pueblos, en Jekabzeel y sus aldeas,
Kuhusu vijiji na mashamba yake, baadhi ya watu wa Yuda waliishi Kiriath-Arba na makazi yaliyokizunguka, katika Diboni na makazi yake, katika Yekabzeeli na vijiji vyake,
26 en Jesúa, en Moladah, Bet Pelet,
katika Yeshua, katika Molada, katika Beth-Peleti,
27 en Hazar Shual en Beersheba y sus aldeas,
katika Hasar-Shuali, katika Beer-Sheba na makazi yake,
28 en Ziklag, en Meconah y sus aldeas,
katika Siklagi, katika Mekona na makazi yake,
29 en En Rimmon, en Zorah, en Jarmuth,
katika En-Rimoni, katika Sora, katika Yarmuthi,
30 Zanoah, Adullam y sus aldeas, Lachish y sus campos, y Azekah y sus aldeas. Y acamparon desde Beerseba hasta el valle de Hinom.
Zanoa, Adulamu na vijiji vyake, katika Lakishi na mashamba yake, na katika Azeka na makazi yake. Hivyo walikuwa wakiishi kuanzia Beer-Sheba mpaka Bonde la Hinomu.
31 Los hijos de Benjamín también vivían desde Geba, en Micmas y Aija, y en Betel y sus pueblos,
Wazao wa Wabenyamini kutoka Geba waliishi Mikmashi, Aiya, Betheli na makazi yake,
32 en Anatot, Nob, Ananías,
katika Anathothi, Nobu na Anania,
33 Hazor, Ramá, Gittaim,
katika Hazori, Rama na Gitaimu,
34 Hadid, Zeboim, Neballat,
katika Hadidi, Seboimu na Nebalati,
35 Lod y Ono, el valle de los artesanos.
katika Lodi na Ono, na katika Bonde la Mafundi.
36 De los levitas, ciertas divisiones de Judá se establecieron en el territorio de Benjamín.
Baadhi ya makundi ya Walawi wa Yuda waliishi huko Benyamini.

< Nehemías 11 >