< Josué 19 >

1 La segunda suerte salió para Simeón, para la tribu de los hijos de Simeón según sus familias. Su herencia estaba en medio de la herencia de los hijos de Judá.
Kura ya pili ikaangukia kabila la Simeoni, ukoo kwa ukoo. Urithi wao ulikuwa ndani ya eneo la Yuda.
2 Tuvieron por herencia Beerseba (o Seba), Molada,
Ulijumuisha: Beer-Sheba (au Sheba), Molada,
3 Hazar Sual, Balá, Ezem,
Hasar-Shuali, Bala, Esemu,
4 Eltolad, Betul, Horma,
Eltoladi, Bethuli, Horma,
5 Siclag, Bet Marcabot, Hazar Susa,
Siklagi, Beth-Markabothi, Hasar-Susa,
6 Bet Lebaot y Sharuhen; trece ciudades con sus aldeas;
Beth-Lebaothi na Sharuheni; hii ilikuwa miji kumi na mitatu pamoja na vijiji vyake.
7 Ain, Rimmón, Éter y Asán; cuatro ciudades con sus aldeas;
Pia Aini, Rimoni, Etheri, na Ashani; hii ilikuwa miji minne na vijiji vyake,
8 y todas las aldeas que estaban alrededor de estas ciudades hasta Baalat Beer, Ramá del Sur. Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Simeón según sus familias.
pamoja na vijiji vyote vinavyoizunguka miji hii mpaka Baalath-Beeri (ambayo ndiyo Rama iliyo katika Negebu). Huu ulikuwa ni urithi wa kabila la Simeoni ukoo kwa ukoo.
9 De la parte de los hijos de Judá fue la herencia de los hijos de Simeón; porque la parte de los hijos de Judá era demasiado para ellos. Por lo tanto, los hijos de Simeón tuvieron herencia en medio de su heredad.
Urithi wa Wasimeoni ulitolewa kutoka fungu la Yuda, kwa kuwa fungu la Yuda lilikuwa kubwa kuliko walivyohitaji. Hivyo kabila la Simeoni lilipewa urithi wao ndani ya eneo la Yuda.
10 La tercera suerte correspondió a los hijos de Zabulón según sus familias. El límite de su herencia fue hasta Sarid.
Kura ya tatu ikaangukia kabila la Zabuloni, ukoo kwa ukoo: Mpaka wa urithi wao uliendelea hadi Saridi.
11 Su límite subía hacia el oeste, hasta Maralá, y llegaba hasta Dabbeshet. Llegaba hasta el arroyo que está frente a Jocneam.
Kuelekea upande wa magharibi ukafika Marala, ukagusa Dabeshethi, na kuendelea mpaka kwenye bonde karibu na Yokneamu.
12 Desde Sarid giraba hacia el este, hacia la salida del sol, hasta el límite de Chisloth Tabor. Salió a Daberat, y subió a Jafa.
Ukageuka mashariki, kuanzia Saridi kuelekea mawio ya jua hadi kwenye nchi ya Kisiloth-Tabori, na kwenda hadi Daberathi, kupanda Yafia.
13 De allí pasaba hacia el oriente hasta Gat Hefer, hasta Etkazin; y salía en Rimón que se extiende hasta Neah.
Kisha ukaendelea mashariki hadi Gath-Heferi na kufika Eth-Kasini, ukatokea Rimoni na kugeuka kuelekea Nea.
14 La frontera la rodeaba por el norte hasta Hannatón; y terminaba en el valle de Iphtah El;
Huko mpaka ukazungukia upande wa kaskazini hadi Hanathoni na kuishia katika Bonde la Ifta-Eli.
15 Kattath, Nahalal, Shimron, Idalah y Belén: doce ciudades con sus aldeas.
Miji mingine iliyojumuishwa ni Katathi, Nahalali, Shimroni, Idala na Bethlehemu. Kulikuwa na miji kumi na miwili pamoja na vijiji vyake.
16 Esta es la herencia de los hijos de Zabulón según sus familias, estas ciudades con sus aldeas.
Miji hii na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa Zabuloni, ukoo kwa ukoo.
17 La cuarta suerte salió para Isacar, para los hijos de Isacar según sus familias.
Kura ya nne ikamwangukia Isakari, ukoo kwa ukoo.
18 Su límite era Jezreel, Cesulot, Sunem,
Eneo lao lilijumuisha: Yezreeli, Kesulothi, Shunemu,
19 Hafaraim, Shion, Anaharat,
Hafaraimu, Shioni, Anaharathi,
20 Rabbith, Kishion, Ebez,
Rabithi, Kishioni, Ebesi,
21 Remeth, Engannim, En Haddah y Bet Pazzez.
Remethi, En-Ganimu, En-Hada na Beth-Pasesi.
22 La frontera llegaba hasta Tabor, Shahazumah y Beth Shemesh. Su frontera terminaba en el Jordán: dieciséis ciudades con sus aldeas.
Mpaka ule ukagusa Tabori, Shahasuma na Beth-Shemeshi, na ukaishia kwenye Yordani. Ilikuwa miji kumi na sita, pamoja na vijiji vyake.
23 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Isacar según sus familias, las ciudades con sus aldeas.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa urithi wa kabila la Isakari, ukoo kwa ukoo.
24 La quinta suerte salió para la tribu de los hijos de Aser según sus familias.
Kura ya tano ikaangukia kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
25 Su frontera era Helkath, Hali, Beten, Achshaph,
Eneo lao lilijumuisha: Helkathi, Hali, Beteni, Akishafu,
26 Allammelech, Amad, Mishal. Llegaba hasta el Carmelo, al oeste, y hasta Shihorlibnath.
Alameleki, Amadi na Mishali. Upande wa magharibi mpaka uligusa Karmeli na Shihor-Libnathi.
27 Se volvió hacia la salida del sol hasta Bet Dagón, y llegó hasta Zabulón, y hasta el valle de Iftá El hacia el norte, hasta Bet Emek y Neiel. Salía a Cabul por la izquierda,
Tena ukageuka mashariki kuelekea Beth-Dagoni, ukagusa Zabuloni na Bonde la Ifta-Eli, ukaenda upande wa kaskazini hadi Beth-Emeki na Neyeli, ukipitia Kabul upande wa kushoto.
28 y a Ebrón, Rehob, Hamón y Caná, hasta la gran Sidón.
Ukaendelea hadi Abdoni, Rehobu, Hamoni na Kana, na kufika Sidoni Kuu.
29 La frontera daba vuelta a Rama, a la ciudad fortificada de Tiro; y la frontera daba vuelta a Hosa. Termina en el mar, junto a la región de Aczib;
Mpaka huo ukageukia nyuma kuelekea Rama na kwenda hadi kwenye mji wenye ngome wa Tiro, ukageuka kuelekea Hosa na kutokeza baharini katika eneo la Akzibu,
30 También Umma, Afec y Rehob: veintidós ciudades con sus aldeas.
Uma, Afeki na Rehobu. Ilikuwepo miji ishirini na miwili, pamoja na vijiji vyake.
31 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Aser según sus familias, estas ciudades con sus aldeas.
Miji hii pamoja na vijiji vyake ilikuwa ndio urithi wa kabila la Asheri, ukoo kwa ukoo.
32 La sexta suerte salió para los hijos de Neftalí, para los hijos de Neftalí según sus familias.
Kura ya sita ikaangukia kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo:
33 Su frontera era desde Helef, desde la encina de Zaanannim, Adami-nekeb y Jabneel, hasta Lakkum. Terminaba en el Jordán.
Mpaka wao uliendelea kutoka Helefi na kwenye mti mkubwa ulio katika Saananimu, ukipitia Adami-Nekebu na Yabineeli hadi Lakumu, na kuishia katika Mto Yordani.
34 La frontera giraba hacia el oeste hasta Aznoth Tabor, y salía de allí hasta Hukkok. Llegaba hasta Zabulón por el sur, y llegaba hasta Aser por el oeste, y hasta Judá en el Jordán, hacia la salida del sol.
Mpaka ukaendelea magharibi kupitia Aznoth-Tabori na kutokea Hukoki. Ukagusa Zabuloni upande wa kusini, Asheri upande wa magharibi, na Yordani upande wa mashariki.
35 Las ciudades fortificadas eran Ziddim, Zer, Hamat, Rakkat, Chinnereth,
Miji yenye ngome ilikuwa Sidimu, Seri, Hamathi, Rakathi, Kinerethi,
36 Adamah, Ramah, Hazor,
Adama, Rama, Hazori,
37 Kedesh, Edrei, En Hazor,
Kedeshi, Edrei, na En-Hasori,
38 Hierro, Migdal El, Horem, Beth Anath y Beth Shemesh; diecinueve ciudades con sus aldeas.
Ironi, Migdal-Eli, Horemu, Beth-Anathi na Beth-Shemeshi. Kulikuwa na miji kumi na tisa na vijiji vyake.
39 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Neftalí según sus familias, las ciudades con sus aldeas.
Miji hiyo pamoja na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Naftali, ukoo kwa ukoo.
40 La séptima suerte correspondió a la tribu de los hijos de Dan según sus familias.
Kura ya saba ikaangukia kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
41 El límite de su heredad fue Zora, Eshtaol, Irshemesh,
Eneo la urithi wao lilijumuisha: Sora, Eshtaoli, Iri-Shemeshi,
42 Shaalabbin, Aijalon, Ithlah,
Shaalabini, Aiyaloni, Ithla,
43 Elon, Timnah, Ecron,
Eloni, Timna, Ekroni,
44 Eltekeh, Gibbethon, Baalath,
Elteke, Gibethoni, Baalathi,
45 Jehud, Bene Berak, Gath Rimmon,
Yehudi, Bene-Beraki, Gath-Rimoni,
46 Me Jarkon, y Rakkon, con el límite frente a Joppa.
Me-Yarkoni na Rakoni, pamoja na eneo linalotazamana na Yafa.
47 El límite de los hijos de Dan iba más allá de ellos, pues los hijos de Dan subieron y combatieron contra Leshem, la tomaron y la hirieron a filo de espada, la poseyeron y vivieron en ella, y llamaron a Leshem, Dan, por el nombre de Dan, su antepasado.
(Lakini Wadani walipata shida kulimiliki eneo lao; kwa hiyo walipanda kuishambulia Leshemu, wakaitwaa, wakawaua watu wake kwa upanga na kuukalia. Walikaa Leshemu na kuuita Dani kufuatana na jina la baba yao.)
48 Esta es la herencia de la tribu de los hijos de Dan según sus familias, estas ciudades con sus aldeas.
Miji hii na vijiji vyake ndio iliyokuwa urithi wa kabila la Dani, ukoo kwa ukoo.
49 Así terminaron de distribuir la tierra en herencia por sus fronteras. Los hijos de Israel dieron en herencia a Josué, hijo de Nun, entre ellos.
Walipomaliza kugawanya nchi katika migawo kulingana na sehemu zao zilizowaangukia, Waisraeli wakampa Yoshua mwana wa Nuni urithi katikati yao,
50 De acuerdo con el mandato de Yahvé, le dieron la ciudad que pidió, es decir, Timnathserah, en la región montañosa de Efraín; y él edificó la ciudad y vivió allí.
kama vile Bwana alivyokuwa ameamuru. Walimpa mji alioutaka, ambao ni Timnath-Sera ulio katika nchi ya vilima ya Efraimu. Naye akajenga mji, akakaa huko.
51 Estas son las herencias que el sacerdote Eleazar, Josué hijo de Nun y los jefes de las casas paternas de las tribus de los hijos de Israel, repartieron por sorteo en Silo, delante de Yahvé, a la puerta de la Tienda del Encuentro. Así terminaron de repartir la tierra.
Haya ndiyo maeneo ambayo kuhani Eleazari, Yoshua mwana wa Nuni, na viongozi wa koo za kabila za Israeli waliyoyagawanya kwa kura huko Shilo mbele za Bwana penye ingilio la Hema la Kukutania. Hivyo wakamaliza kuigawanya nchi.

< Josué 19 >