< Job 38 >

1 Entonces Yahvé respondió a Job desde el torbellino,
Ndipo Yahweh alimwita Ayubu kutoka katika dhoruba kali na kumwambia,
2 “¿Quién es el que oscurece el consejo por palabras sin conocimiento?
“Huyu ni nani aletaye giza katika mipango kwa njia ya maneno bila maarifa?
3 Prepárate como un hombre, porque yo te interrogaré y tú me responderás.
Basi sasa jifunge kiunoni mwako kama mwanaume kwa kuwa nitakuuliza maswali, nawe lazima unijibu.
4 “¿Dónde estabas cuando puse los cimientos de la tierra? Declara, si tienes entendimiento.
Wewe ulikuwa wapi wakati nilipoitandaza misingi ya dunia? Niambie, kama unao ufahamu zaidi.
5 ¿Quién determinó sus medidas, si lo sabe? ¿O quién estiró la línea en él?
Je ni nani aliyeamuru vipimo vyake? Niambie, kama unajua, ni nani alivinyosha vipimo juu yake?
6 ¿Sobre qué estaban fijados sus cimientos? O quién puso su piedra angular,
Misingi yake ilitandazwa juu ya nini? Ni nani aliyeliweka jiwe lake la pembeni
7 cuando las estrellas de la mañana cantaban juntas, y todos los hijos de Dios gritaron de alegría?
wakati nyota za asubuhi zilipoimba pamoja na wana wote wa Mungu walipopiga kelele kwa furaha?
8 “O que cierra el mar con puertas, cuando salió del vientre materno,
Ni nani huifunga bahari kwa milango wakati inapofurika, kana kwamba inatoka katika tumbo,
9 cuando hice de las nubes su vestimenta, y lo envolvió en una espesa oscuridad,
wakati nilipoyafanya mawingu kuwa ni mavazi yake, na giza nene kuwa mkanda wake wa kujifungia?
10 marcadas para ello mi límite, poner barras y puertas,
Hapo ilikuwa wakati nilipoweka bahari mpaka wangu, na nilipoweka makomeo yake na milango,
11 y dijo: “Puedes venir aquí, pero no más allá. ¿Tus orgullosas olas serán detenidas aquí?
na wakati nilipoiambia, 'Unaweza kuja hapa kutoka mbali, lakini si zaidi; na hapa ndipo nitauweka mpaka kwa fahari ya mawimbi yako.'
12 “¿Has ordenado la mañana en tus días, y ha hecho que el amanecer conozca su lugar,
Je tangu mwanzo wa siku zako, ulishawahi kuigiza asubuhi ianze, na kuyafanya mapambazuko yajue sehemu yake katika mpangilio wa vitu,
13 para que se apodere de los confines de la tierra, y sacudir a los malvados fuera de ella?
ili kwamba ishikilie sehemu za dunia ili watu waovu watikiswe mbali nayo.
14 Se cambia como la arcilla bajo el sello, y presentado como una prenda de vestir.
Dunia imebadilishwa katika mwonekano kama udongo unavyobadilika chini ya muhuri; vitu vyote husimama juu yake dhahiri kama cha kibindo cha nguo.
15 A los malvados se les oculta la luz. El brazo alto está roto.
'Mwanga' wao umeondolewa kutoka kwa watu waovu; na mkono wao ulioinuliwa umevunjwa.
16 “¿Has entrado en los manantiales del mar? ¿O has caminado por los recovecos de las profundidades?
Je umeshaenda kwenye vyanzo vya maji ya bahari? Je umeshatembea sehemu za chini kabisa za kilindi?
17 ¿Se te han revelado las puertas de la muerte? ¿O has visto las puertas de la sombra de la muerte?
Je malango ya mauti yamefunuliwa kwako? Je umeshaona malango ya uvuli wa mauti?
18 ¿Has comprendido la tierra en su anchura? Declara, si lo sabes todo.
Je umeifahamu dunia katika upana wake? Niambie kama unayajua yote hayo.
19 “¿Cuál es el camino hacia la morada de la luz? En cuanto a la oscuridad, cuál es su lugar,
Je iko wapi njia ya sehemu ya kupumzikia kwa mwanga, na kama ilivyo kwa giza, iko wapi sehemu yake?
20 que lo lleves a su límite, para que discierna los caminos de su casa?
Je unaweza kuuongoza mwanga na giza katika sehemu zake za kazi? Waweza kuitambua njia ya kurudi katika nyumba zao?
21 Seguramente lo sabes, pues naciste entonces, ¡y el número de sus días es genial!
Bila shaka unajua, kwa kuwa ulizaliwa wakati huo; hesabu ya siku zako ni kubwa sana!
22 ¿Has entrado en los almacenes de la nieve, o has visto los almacenes del granizo,
Je ulishaingia katika ghala ya barafu, au umeshaiona ghala ya mawe ya mvua,
23 que he reservado para el tiempo de la angustia, contra el día de la batalla y la guerra?
vitu hivi nimeviweka kwa ajili ya siku za mateso, kwa siku za mapigano na vita?
24 De qué manera se distribuye el rayo, o el viento del este disperso en la tierra?
Je iko wapi njia ya mshindo wa mwanga hutokea au je upepo husambazwa kutoka mashariki juu ya dunia?
25 Que ha cortado un canal para el agua de la inundación, o la trayectoria de la tormenta,
Ni nani aliyezitengeneza mifereji ya gharika ya mvua, au ni nani aliyezifanya njia za milipuko ya radi,
26 para hacer llover en una tierra donde no hay hombre, en el desierto, en el que no hay hombre,
na kuifanya mvua inyeshe juu ya nchi ambazo hakuna mtu aishiye ndani yake, na juu ya jangwa, ambayo ndani yake hakuna mtu yeyote,
27 para saciar el terreno baldío y desolado, para hacer crecer la hierba tierna?
kwa kusudi la kutimiza mahitaji ya mikoa iliyo kame na yenye ukiwa, na kuyastawisha majani mororo?
28 ¿La lluvia tiene padre? ¿O quién recoge las gotas de rocío?
Je kuna baba wa mvua? Ni nani aliyeyafanya matone ya umande?
29 ¿De qué vientre salió el hielo? ¿Quién ha dado a luz a la escarcha gris del cielo?
Je barafu ilitoka katika tumbo la nani? Na ni nani aliyeizaa theluji nyeupe katika anga?
30 Las aguas se vuelven duras como la piedra, cuando la superficie de las profundidades está congelada.
Maji hujificha menyewe na kuwa kama jiwe; sehemu za juu za vilindi huwa kama barafu.
31 “¿Puedes atar el cúmulo de las Pléyades, o aflojar las cuerdas de Orión?
Je unaweza kuzifunga minyororo ya Kilimia, au kuvifungua vifundo vya Orioni?
32 ¿Puedes guiar a las constelaciones en su estación? ¿O puedes guiar a la Osa con sus cachorros?
Je unaweza kuziongoza nyota kutokea katika nyakati zake? Je waweza kuongoza dubu pamoja na watoto wake?
33 ¿Conoces las leyes de los cielos? ¿Puede establecer su dominio sobre la tierra?
Je unazijua sheria za anga? Wewe uliweza kuanzisha sheria za anga juu ya dunia?
34 “¿Puedes elevar tu voz a las nubes, para que la abundancia de aguas te cubra?
Je waweza kupaza sauti yako hadi mawinguni, ili kwamba maji mengi ya mvua yakufunike?
35 ¿Puedes enviar relámpagos para que se vayan? ¿Te informan de que “aquí estamos”?
Je waweza kuagiza miali ya mwanga ili itokee, na kukwambia, 'Sisi tupo hapa'?
36 ¿Quién ha puesto la sabiduría en las partes interiores? ¿O quién ha dado entendimiento a la mente?
Ni nani ameweka hekima katika mawingu au ni nani ameweka ufahamu kwa ukungu?
37 ¿Quién puede contar las nubes con sabiduría? O que puede verter los contenedores del cielo,
Nani anaweza kuyahesabu mawingu kwa maarifa yake? Na ni nani awezaye kuvimwaga viriba vya anga
38 cuando el polvo se convierte en una masa, y los terrones se pegan?
wakati mavumbi yanapoungana kuwa kitu kigumu na mabonge ya dunia yanaposhikama kwa pamoja?
39 “¿Puedes cazar la presa para la leona, o satisfacer el apetito de los jóvenes leones,
Je waweza kuwinda mawindo kwa ajili ya simba jike au kutosheleza hamu ya watoto wadogo wa simba
40 cuando se agazapan en sus guaridas, y acechar en la espesura?
wakati wanapokwaruza kwaruza katika pango lao na kukaa katika kificho ili kulala katika hali ya kuvizia?
41 Que proporciona al cuervo su presa, cuando sus jóvenes claman a Dios, y vagan por falta de comida?
Ni nani aletaye mawindo kwa ajili ya kunguru wakati ambapo watoto wao wanapomlilia Mungu na kutangatanga kwa kukosa chakula?

< Job 38 >