< Job 37 >

1 “Sí, ante esto mi corazón tiembla, y es desplazado de su lugar.
“Kwa hili moyo wangu unatetemeka, nao unaruka kutoka mahali pake.
2 Escucha, oh, escucha el ruido de su voz, el sonido que sale de su boca.
Sikiliza! Sikiliza ngurumo ya sauti yake, sauti ya ngurumo itokayo kinywani mwake.
3 Lo envía bajo todo el cielo, y sus rayos hasta los confines de la tierra.
Huuachilia umeme wake wa radi chini ya mbingu yote na kuupeleka hata miisho ya dunia.
4 Tras ella ruge una voz. Truena con la voz de su majestad. No se guarda nada cuando se escucha su voz.
Baada ya hayo huja sauti ya ngurumo yake; Mungu hunguruma kwa sauti yake ya fahari. Wakati sauti yake ingurumapo tena, huuachilia umeme wake wa radi.
5 Dios truena maravillosamente con su voz. Él hace grandes cosas, que no podemos comprender.
Sauti ya Mungu hunguruma kwa namna za ajabu; yeye hutenda mambo makuu kupita ufahamu wetu.
6 Porque dice a la nieve: “Cae sobre la tierra”. también a la lluvia, y a los chubascos de su poderosa lluvia.
Huiambia theluji, ‘Anguka juu ya dunia,’ nayo manyunyu ya mvua, ‘Uwe mvua ya nguvu.’
7 Él sella la mano de cada hombre, para que todos los hombres a los que ha hecho lo conozcan.
Ili wanadamu wote aliowaumba wapate kujua kazi zake, yeye humzuilia kila mtu shughuli zake.
8 Entonces los animales se ponen a cubierto, y permanecen en sus guaridas.
Wanyama hujificha; hubakia kwenye mapango yao.
9 De su habitación sale la tormenta, y el frío del norte.
Dhoruba hutoka katika chumba chake, baridi hutoka katika upepo uendao kasi.
10 Por el soplo de Dios se da el hielo, y la anchura de las aguas está congelada.
Pumzi ya Mungu hutoa barafu, eneo kubwa la maji huganda.
11 Sí, carga la espesa nube con humedad. Extiende la nube de su rayo.
Huyasheheneza mawingu kwa maji, naye husambaza umeme wake wa radi kupitia hayo.
12 Se ha dado la vuelta gracias a su guía, para que hagan todo lo que él les mande en la superficie del mundo habitable,
Nayo mawingu huzungukazunguka pande zote kwa amri yake, juu ya uso wa dunia yote, kufanya lolote ayaamuruyo.
13 ya sea por la corrección, o por su tierra, o por la bondad amorosa, que la hace venir.
Huleta mawingu ili kuadhibu wanadamu, au kuinyeshea dunia yake na kuonyesha upendo wake.
14 “Escucha esto, Job. Quédate quieto y considera las obras maravillosas de Dios.
“Ayubu, sikiliza hili; nyamaza na uyafikiri maajabu ya Mungu.
15 ¿Sabes cómo los controla Dios? y hace brillar el rayo de su nube?
Je, unajua jinsi Mungu anavyoyaongoza mawingu, na kufanya umeme wake wa radi utoe mwanga?
16 ¿Conoces el funcionamiento de las nubes, las obras maravillosas de aquel que es perfecto en el conocimiento?
Je, wajua jinsi mawingu yanavyokaa yakiwa yametulia, hayo maajabu yake yeye aliye mkamilifu katika maarifa?
17 Tú, cuya ropa es cálida cuando la tierra está quieta a causa del viento del sur?
Wewe unayeshindwa na joto katika nguo zako wakati nchi imenyamazishwa kimya bila upepo wa kusini,
18 ¿Puedes, con él, extender el cielo, que es fuerte como un espejo de metal fundido?
je, waweza kuungana naye katika kuzitandaza anga, zilizo ngumu kama kioo cha shaba ya kuyeyushwa?
19 Enséñanos lo que le vamos a decir, porque no podemos hacer nuestro caso a causa de la oscuridad.
“Tuambieni yatupasayo kumwambia; hatuwezi kutayarisha shauri letu kwa sababu ya ujinga wetu.
20 ¿Se le dirá que voy a hablar? ¿O debería un hombre desear ser tragado?
Je, aambiwe kwamba nataka kuongea? Je, yuko mtu ambaye angeomba kumezwa?
21 Los hombres no ven la luz que brilla en los cielos, pero el viento pasa y los despeja.
Basi hakuna awezaye kulitazama jua, jinsi linavyongʼaa angani, upepo ukishafagia mawingu.
22 Del norte viene el esplendor dorado. Con Dios hay una majestuosidad impresionante.
Kutoka kaskazini yeye huja na fahari kuu; Mungu huja katika utukufu wa kutisha.
23 No podemos llegar al Todopoderoso. Está exaltado en el poder. Con justicia y gran rectitud, no oprimirá.
Yeye Mwenyezi hatuwezi kumfikia, naye ametukuzwa katika uweza; katika hukumu zake na haki yake kuu, hataonea.
24 Por eso los hombres lo veneran. No tiene en cuenta a los sabios de corazón”.
Kwa hiyo, wanadamu mheshimuni, kwa kuwa yeye hamstahi yeyote anayejidhania kuwa ana hekima.”

< Job 37 >