< Job 33 >
1 “Sin embargo, Job, escucha mi discurso, y escucha todas mis palabras.
Kwahiyo sasa, nakuomba wewe, Ayubu, usikilize hotuba yangu; sikiliza maneno yangu yote.
2 Mira ahora, he abierto mi boca. Mi lengua ha hablado en mi boca.
Tazama sasa, nimeufumbua mdomo wangu; ulimi wangu umesema maneno ndani ya mdomo wangu.
3 Mis palabras expresarán la rectitud de mi corazón. Lo que mis labios saben que hablarán con sinceridad.
Maneno yangu yatasema uadilifu wa moyo wangu; yatasema kwa unyofu yale ambayo mdomo wangu unayajua.
4 El Espíritu de Dios me ha hecho, y el aliento del Todopoderoso me da la vida.
Roho ya Mungu imeniumba; pumzi ya Mwenye nguvu imenipatia uhai.
5 Si puedes, respóndeme. Pon en orden tus palabras ante mí, y levántate.
Kama unaweza, nijibu; weka maneno yako katika mpangilio mbele yangu na kisha usimame.
6 He aquí que yo soy para con Dios lo mismo que vosotros. Yo también estoy formado de la arcilla.
Tazama, niko kama wewe ulivyo mbele za Mungu; nimeumbwa pia kutoka katika udongo.
7 He aquí que mi terror no te hará temer, ni mi presión será pesada para ti.
Ona, tishio langu halitakufanya wewe uogope; wala mzigo wangu hautakuwa mzito kwako.
8 “Ciertamente, has hablado a mi oído, He escuchado la voz de tus palabras, diciendo,
Umesema kwa hakika katika masikio yangu; nimeisikia sauti ya maneno yakeo yakisema,
9 ‘Estoy limpio, sin desobediencia. Soy inocente y no hay iniquidad en mí.
'Mimi ni safi na bila hila; sina hatia, na hakuna dhambi ndani yangu.
10 He aquí que encuentra ocasiones contra mí. Me cuenta como su enemigo.
Tazama, Mungu huona nafasi za kunishambulia mimi; huniangalia mimi kama adui yake.
11 Pone mis pies en el cepo. Él marca todos mis caminos”.
Huweka miguu yangu akiba; naye huangalia njia zangu zote.'
12 “He aquí que yo te responderé. En esto no eres justo, porque Dios es más grande que el hombre.
Tazama, katika hili hauko sawa, nitakujibu, kwa kuwa Mungu ni mkuu kuliko mtu.
13 ¿Por qué os esforzáis contra él? porque no da cuenta de ninguno de sus asuntos?
Kwanini unashindana naye? Huwa hahesabu matendo yake yoyote.
14 Porque Dios habla una vez, sí dos veces, aunque el hombre no presta atención.
Kwa kuwa Mungu huzungumza mara moja, naam, mara mbili, ingawa mwanadamu hawezi kutambua.
15 En un sueño, en una visión nocturna, cuando el sueño profundo cae sobre los hombres, en el sueño en la cama,
Katika ndoto, katika maono ya usiku, wakati usingizi mzito unapowapata watu, katika usingizi kitandani -
16 entonces abre los oídos de los hombres, y sella su instrucción,
basi Mungu hufungua masikio ya watu, na kuwatisha kwa vitisho,
17 para que retire al hombre de su propósito, y ocultar el orgullo del hombre.
kwa kusudi la kumvuta mtu atoke katika makusudio yake maovu, na kuyaweka majivuno mbali naye.
18 Aleja su alma de la fosa, y su vida de perecer por la espada.
Mungu huyaokoa maisha ya mwanadamu kutoka katika shimo, na uhai wake dhidi ya kifo.
19 “También es castigado con dolor en su cama, con una lucha continua en sus huesos,
Mtu huadhidibiwa pia na maumivu kitandani mwake, na maumivu makali yanayodumu katika mifupa yake,
20 para que su vida aborrezca el pan, y su alma un alimento delicado.
ili kwamba maisha yake yachukie chakula, na roho yake ichukie vyakula vizuri.
21 Su carne está tan consumida que no se puede ver. Sus huesos que no se vieron sobresalen.
Nyama yake imeharibiwa ili kwamba usionekane; mifupa yake, mara moja isionekane, sasa basi ng'ang'ania.
22 Sí, su alma se acerca a la fosa, y su vida a los destructores.
Hakika, roho yake inasogea shimoni, na uhai wake unasogea kwa wale wanaotaka kuuharibu.
23 “Si hay junto a él un ángel, un intérprete, uno entre mil, para mostrar al hombre lo que es correcto para él,
Lakini kama kuna malaika anayeweza kuwa mpatanishi kwa ajili yake, mpatanishi mmoja miongoni mwa maelfu ya malaika, kumwonesha kile kilicho cha haki ili atende haki,
24 entonces Dios se apiada de él y le dice, Líbralo de bajar a la fosa, He encontrado un rescate”.
na kama malaika ni mpole kwake na kumwambia Mungu, 'Mwokoe mtu huyu ili asishuke chini shimoni; nimepata fidia kwa ajili yake,'
25 Su carne será más fresca que la de un niño. Vuelve a los días de su juventud.
kisha mwili wake utakuwa mororo kuliko mwili wa mtoto, atazirudia siku za nguvu za ujana wake.
26 Reza a Dios, y éste le es favorable, para que vea su rostro con alegría. Él devuelve al hombre su justicia.
Atamwomba Mungu, na Mungu atakuwa mwema kwake, ili kwamba auone uso wa Mungu akiwa mwenye furaha. Mungu atampa mtu ushindi wake.
27 Canta ante los hombres y dice, He pecado y he pervertido lo que era justo, y no me benefició.
Ndipo mtu huyo ataimba mbele ya watu wengine na kusema, 'Nilitenda dhambi na kuasi kile kilichokuwa cha haki, lakini dhambi yangu haikuadhibiwa.
28 Él ha redimido mi alma de ir a la fosa. Mi vida verá la luz”.
Mungu ameiokoa roho yangu isiende chini shimoni; maisha yangu yataendelea kuuona mwanga.'
29 “He aquí que Dios hace todas estas cosas, dos veces, sí tres veces, con un hombre,
Tazama, Mungu hufanya mambo haya yote pamoja na mwanadamu, mara mbili, naam, hata mara tatu,
30 para sacar su alma de la fosa, para que sea iluminado con la luz de los vivos.
kuirudisha roho yake kutoka shimoni, ili kwamba aweze kumlikwa na mwanga wa maisha.
31 Fíjate bien, Job, y escúchame. Guarda silencio, y yo hablaré.
Ayubu, zingatia na unisikilize mimi; nyamaza nami nitasema.
32 Si tienes algo que decir, respóndeme. Habla, pues deseo justificarte.
Ikiwa una kitu cha kusema, na unijibu; sema, maana nataka kuhakikisha kwamba wewe uko katika haki.
33 Si no, escúchame. Guarda la paz, y yo te enseñaré la sabiduría”.
Kama sivyo, basi nisikilize, ubaki kimya, nami nitakufundisha wewe hekima.”