< Jeremías 15 >

1 Entonces el Señor me dijo: “Aunque Moisés y Samuel estuvieran delante de mí, mi mente no se volvería hacia este pueblo. Apártalos de mi vista y deja que salgan.
Kisha Bwana akaniambia: “Hata kama Mose na Samweli wangesimama mbele zangu, moyo wangu usingewaelekea watu hawa. Waondoe mbele za macho yangu! Waache waende!
2 Sucederá que cuando te pregunten: “¿Por dónde saldremos?”, les dirás: “Dice el Señor: “Los que son para la muerte, a la muerte; los que son para la espada, a la espada; los que son para el hambre, al hambre; y los que son para el cautiverio, al cautiverio”.
Nao kama wakikuuliza, ‘Twende wapi?’ Waambie, ‘Hili ndilo Bwana asemalo: “‘Wale waliowekwa kwa ajili ya kufa, wakafe; waliowekwa kwa ajili ya upanga, kwa upanga; waliowekwa kwa ajili ya njaa, kwa njaa: waliowekwa kwa ajili ya kutekwa, watekwe.’”
3 “Designaré sobre ellos cuatro clases”, dice Yahvé: “la espada para matar, los perros para desgarrar, las aves del cielo y los animales de la tierra para devorar y destruir.
Bwana asema, “Nitatuma aina nne za waharabu dhidi yao: nazo ni upanga ili kuua na mbwa ili wakokote mbali, ndege wa angani na wanyama wa nchi ili kula na kuangamiza.
4 Haré que sean arrojados de un lado a otro entre todos los reinos de la tierra, a causa de Manasés, hijo de Ezequías, rey de Judá, por lo que hizo en Jerusalén.
Nitawafanya wawe machukizo kwa falme zote za dunia kwa sababu ya kile alichofanya Manase mwana wa Hezekia mfalme wa Yuda huko Yerusalemu.
5 Porque ¿quién se apiadará de ti, Jerusalén? ¿Quién te llorará? ¿Quién vendrá a preguntar por su bienestar?
“Ni nani atakayekuhurumia, ee Yerusalemu? Ni nani atakayeomboleza kwa ajili yako? Ni nani atakayesimama ili kuuliza kuhusu hali yako?
6 Me has rechazado”, dice Yahvé. “Has ido hacia atrás. Por eso he extendido mi mano contra ti y te destruyó. Estoy cansado de mostrar compasión.
Umenikataa mimi,” asema Bwana. “Unazidi kukengeuka. Hivyo nitanyoosha mkono wangu juu yako na kukuangamiza, siwezi kuendelea kukuonea huruma.
7 Los he aventado con un abanico en las puertas de la tierra. Les he quitado hijos. He destruido a mi pueblo. No volvieron de sus caminos.
Nitawapepeta kwa uma wa kupepetea kwenye malango ya miji katika nchi. Nitaleta msiba na maangamizi juu ya watu wangu, kwa maana hawajabadili njia zao.
8 Sus viudas aumentan más que la arena de los mares. He traído sobre ellos contra la madre de los jóvenes un destructor al mediodía. He hecho que la angustia y los terrores caigan sobre ella de repente.
Nitawafanya wajane wao kuwa wengi kuliko mchanga wa bahari. Wakati wa adhuhuri nitamleta mharabu dhidi ya mama wa vijana wao waume; kwa ghafula nitaleta juu yao maumivu makuu na hofu kuu.
9 La que ha dado a luz a siete languidece. Ha renunciado al espíritu. Su sol se ha puesto cuando aún era de día. Se ha sentido decepcionada y confundida. Entregaré sus residuos a la espada ante sus enemigos”, dice Yahvé.
Mama mwenye watoto saba atazimia na kupumua pumzi yake ya mwisho. Jua lake litatua kungali bado mchana, atatahayarika na kufedheheka. Wale wote waliobaki nitawaua kwa upanga mbele ya adui zao,” asema Bwana.
10 ¡Ay de mí, madre mía, que me has dado a luz, un hombre conflictivo! ¡y un hombre de contención para toda la tierra! Yo no he prestado, ni los hombres me han prestado; pero cada uno de ellos me maldice.
Ole wangu, mama yangu, kwamba ulinizaa, mtu ambaye ulimwengu wote unashindana na kugombana naye! Sikukopa wala sikukopesha, lakini kila mmoja ananilaani.
11 Yahvé dijo, “Ciertamente te fortaleceré para siempre. Ciertamente haré que el enemigo te suplique en el tiempo del mal y en el tiempo de aflicción.
Bwana akasema, “Hakika nitakuokoa kwa kusudi jema, hakika nitawafanya adui zako wakuombe msaada nyakati za maafa na nyakati za dhiki.
12 Se puede romper el hierro, incluso el hierro del norte, y el bronce?
“Je, mtu aweza kuvunja chuma, chuma kitokacho kaskazini, au shaba?
13 Daré tus bienes y tus tesoros por un botín sin precio, y eso por todos sus pecados, incluso en todas sus fronteras.
Utajiri wako na hazina zako nitavitoa kuwa nyara, bila gharama, kwa sababu ya dhambi zako zote katika nchi yako yote.
14 Los haré pasar con tus enemigos a una tierra que no conoces; porque un fuego se enciende en mi ira, que arderá en ti”.
Nitakufanya uwe mtumwa wa adui zako katika nchi usiyoijua, kwa kuwa katika hasira yangu moto umewashwa utakaowaka juu yako daima.”
15 Yahvé, ya sabes. Recuérdame, visítame, y véngame de mis perseguidores. Eres paciente, así que no me lleves. Sabed que por vosotros he sufrido reproches.
Wewe unafahamu, Ee Bwana, unikumbuke na unitunze mimi. Lipiza kisasi juu ya watesi wangu. Kwa uvumilivu wako usiniondolee mbali; kumbuka jinsi ninavyoshutumiwa.
16 Sus palabras fueron encontradas, y me los comí. Tus palabras fueron para mí una alegría y el regocijo de mi corazón, porque me llaman por tu nombre, Yahvé, Dios de los Ejércitos.
Maneno yako yalipokuja, niliyala; yakawa shangwe yangu na furaha ya moyo wangu, kwa kuwa nimeitwa kwa jina lako, Ee Bwana Mungu Mwenye Nguvu Zote.
17 No me senté en la asamblea de los que se alegran y se regocijan. Me senté solo por tu mano, porque me has llenado de indignación.
Kamwe sikuketi katika kundi la wafanyao sherehe, wala kamwe sikujifurahisha pamoja nao; niliketi peke yangu kwa sababu mkono wako ulikuwa juu yangu, na wewe ulikuwa umenijaza hasira.
18 Por qué mi dolor es perpetuo, y mi herida incurable, que se niega a ser curado? ¿Serás para mí como un arroyo engañoso, ¿como las aguas que fallan?
Kwa nini maumivu yangu hayakomi, na jeraha langu ni la kuhuzunisha, wala haliponyeki? Je, utakuwa kwangu kama kijito cha udanganyifu, kama chemchemi iliyokauka?
19 Por eso dice Yahvé, “Si vuelves, entonces te traeré de nuevo, para que te presentes ante mí; y si sacas lo precioso de lo vil, serás como mi boca. Volverán a ti, pero no volverás a ellos.
Kwa hiyo hili ndilo asemalo Bwana: “Kama ukitubu, nitakurejeza ili uweze kunitumikia; kama ukinena maneno yenye maana, wala si ya upuzi, utakuwa mnenaji wangu. Watu hawa ndio watakaokugeukia, wala si wewe utakayewageukia wao.
20 Haré de ti para este pueblo un muro de bronce fortificado. Lucharán contra ti, pero no prevalecerán contra ti; porque yo estoy con vosotros para salvaros y para liberarte”, dice Yahvé.
Nitakufanya wewe uwe ukuta kwa watu hawa, ngome ya ukuta wa shaba; watapigana nawe lakini hawatakushinda, kwa maana mimi niko pamoja nawe kukuponya na kukuokoa,” asema Bwana.
21 “Te libraré de la mano de los malvados, y te redimiré de la mano de los terribles”.
“Nitakuokoa kutoka mikono ya waovu, na kukukomboa kutoka makucha ya watu wakatili.”

< Jeremías 15 >