< Isaías 5 >
1 Déjenme cantar para mi bien amado una canción de mi amado sobre su viña. Mi amado tenía un viñedo en una colina muy fructífera.
Acha niimbe kwa mpendwa wangu mzuri, wimbo wa mpendwa wangu kuhusu shamba la mzabibu. Mpendwa wangu ana shamba kwenye mlima wenye rutuba.
2 Lo desenterró, recogió sus piedras, la plantó con la vid más selecta, construyó una torre en el centro, y también recortó una prensa de vino en ella. Buscó que diera uvas, pero dio uvas silvestres.
Analilima, anaondoa mawe, na anaotesha aina ya mizabibu iliyo bora. Na hujenga mnara katikati ya shamba akichimba shinkizo ndani yake. Anasubiria mzabibu uzae matunda lakini unazaa zabibu mwitu.
3 “Ahora, habitantes de Jerusalén y hombres de Judá, por favor, juzga entre mi viña y yo.
Kwa hiyo sasa, wakazi wa Yerusalemu na watu wa Yuda, toa hukumu kati yangu na shamba la mzabibu.
4 ¿Qué más se puede hacer a mi viña que no haya hecho yo en ella? ¿Por qué, cuando busqué que diera uvas, dio uvas silvestres?
Je ni kitu gani cha ziada unaweza ukakifanya kwenye shamba langu la mizabibu, ambacho sijakifanya? ninapotamzamia izae matunda, kwa nini inazaa matunda mwitu?
5 Ahora te diré lo que haré con mi viña. Quitaré su seto y será devorado. Derribaré su muro, y será pisoteado.
Sasa nitawambia kitu nitakacho kifanya kwenye shamba langu la mzabibu: nitaondoa uzio, nitaligeuza kuwa malisho, Nitavunja ukuta wake chini. Na itakanyagwa chini.
6 La convertiré en un páramo. No se podará ni se azadonará, pero le crecerán zarzas y espinas. También ordenaré a las nubes que no llueva sobre él”.
Nami nitaliharibu wala halitapaliliwa wala kuilmwa, bali litatoa mbigiri na miba; nami nitayaamuru mawingu yasinyeshee mvua juu yake.
7 Porque la viña del Señor de los Ejércitos es la casa de Israel, y los hombres de Judá su planta agradable. Buscó la justicia, pero he aquí la opresión, por la justicia, pero he aquí un grito de angustia.
Maana shamba la mzabibu la Yahwe Bwana wa majeshi ni nyumba ya Israeli, na mtu wa Yuda ndio mazao yake ya kupendeza; anaisubiria haki lakini badala ya yaki kuna mauwaji; maana haki, lakini badala yake ni kelele zikihitaji msaada.
8 Ay de los que se unen de casa en casa, que se acuestan campo a campo, hasta que no hay espacio, ¡y se te hace habitar solo en medio de la tierra!
Ole wao wanaoungana nyumba kwa nyumba, shamba kwa shamba, mpaka wanamaliza, na umebaki mwenyewe kwenye shamba!
9 En mis oídos, el Señor de los Ejércitos dice: “Seguramente muchas casas quedarán desoladas, incluso grande y hermosa, desocupada.
Yahwe wa majeshi ameniambia mimi, nyumba nyingi zitakuwa wazi, hata kubwa na zinazovutia, hakuna mwenyeji yeyote.
10 Por diez acres de viñedo se producirá un baño, y un homer de semilla dará un efa”.
Maana mashamba ya mizabibu la nira kumi lilitoa bathi moja tu, na homeri ya mbegu itatoa efa tu.
11 Ay de los que se levantan de madrugada para seguir la bebida fuerte, que se quedan hasta altas horas de la noche, ¡hasta que el vino los enardece!
Ole wao wanaoamka asubuhi na mapema kutafuta pombe kali, wale wanaokaa usiku wa manane mpaka pombe inawaka moto.
12 El arpa, la lira, la pandereta y la flauta, con vino, están en sus fiestas; pero no respetan la obra de Yahvé, ni han considerado la operación de sus manos.
Wanasherekea kwa kinubi, kinanda, kigoma, filimbi, na mvinyo, lakini hawazitambui kazi za Yahwe, wala hawaziangalii kazi za mikono yake.
13 Por eso mi pueblo va al cautiverio por falta de conocimiento. Sus honorables hombres están hambrientos, y sus multitudes están muertas de sed.
Kwa hiyo watu wangu wameenda kifungoni kwa kukosa uelewa; viongozi wao wakuheshimiwa wanashinda na njaa, na watu wao hana kitu cha kunjwa.
14 Por lo tanto, el Seol ha ampliado su deseo, y abrió su boca sin medida; y su gloria, su multitud, su pompa, y el que se regocija entre ellos, descienden a ella. (Sheol )
Hivyo basi kuzimu kumeongeza ladha yake na imefungua kinywa chake kwa kiasi kikubwa; wasomi wao, viongozi wao, manabii na wenye furaha miongoni mwao, watashuka kuzimu. (Sheol )
15 Así el hombre se rebaja, la humanidad es humilde, y los ojos de los arrogantes se humillan;
Mtu atalazimishwa kuinama chini, na watu watakuwa wayenyekevu; na macho yao ya kujivuna yatatupwa chini,
16 pero Yahvé de los Ejércitos es exaltado en la justicia, y Dios el Santo es santificado en justicia.
Yahwe wa majeshi atainuliwa katika haki yake, na Mungu mtakatifu atajidhirisha kuwa mtakatifu kwa haki yake.
17 Entonces los corderos pastarán como en su pasto, y los extraños comerán las ruinas de los ricos.
Ndipo kondoo watalishwa kama wako kwenye malisho yao wenyewe, na katika uharibifu, kondoo watachungwa kama wageni.
18 Ay de los que atraen la iniquidad con cuerdas de mentira, y la maldad como con cuerda de carreta,
Ole wao wanaovuta pamoja na waovu kwa kamba isiyo na maana na wanaovuta pamoja na dhambi kwa kamba za gari.
19 que dicen: “Que se apresure, que acelere su obra, para que la veamos; que el consejo del Santo de Israel se acerque y venga, para que lo conozcamos”.
Ole kwa wale wasemao, '' Basi na Mungu afanye haraka, basi afanya upesi, ili tuweze kuona kinachotokea; na tuache mipango ya Mtakatifu wa Israeli ije, ili tuifahamu.''
20 Ay de los que llaman bueno al mal y malo al bien; que puso la oscuridad por la luz, y la luz para la oscuridad; que puso lo amargo por lo dulce, ¡y dulce por amargo!
Ole wao waitao uovu wema, na wema ni uovu; inayowakilisha giza kama mwanga, na mwanga kama giza; inayowakilisha kitu kichungu kama kitamu, na kitamu kama kichungu!
21 Ay de los que son sabios a sus propios ojos, ¡y prudente ante sus propios ojos!
Ole kwa wale wenye busara machoni mwao, na buasra kwa uelewa wao!
22 Ay de los que son poderosos para beber vino, y campeones en la mezcla de bebidas fuertes;
Ole wao ambao ni washindi kwa kunjwa mvinyo, na wazoefu wa kuchanganya pombe kali;
23 que absuelven a los culpables a cambio de un soborno, ¡pero negar la justicia a los inocentes!
ambao wako huru kumpa haki mtenda maovu, na kuwanyima haki wenye haki!
24 Por eso, como la lengua de fuego devora el rastrojo, y como la hierba seca se hunde en la llama, por lo que su raíz será como la podredumbre, y su flor se convertirá en polvo, porque han rechazado la ley de Yahvé de los Ejércitos, y despreciaron la palabra del Santo de Israel.
Hivyo basi kama ndimi za moto zinazokula mabua, kama majani makavu yanavyochomwa na moto, hivyo basi mizizi yake itaoza na maua yake yataperuka kama mavumbi. Hii itatokea kwa sababu wameikataa sheria ya Yahwe wa majeshi, na kwa sababu wamedharau neno la Mtakatifu wa Israeli.
25 Por eso la ira de Yahvé arde contra su pueblo, y ha extendido su mano contra ellos y los ha golpeado. Las montañas tiemblan, y sus cadáveres son como basura en medio de las calles. Por todo esto, su ira no se desvía, pero su mano sigue extendida.
Hivyo basi hasira ya Yahwe imewaka juu ya watu wake. Ameunyoosh mkono wake juu yao na kuwaadhibu wao. Milima inatikisika, na maiti ni kama takata mitaani. Katika mambo yote haya, hasira yake haijapungua; badala yake, ameonyoosha mkono wake nje.
26 Él levantará un estandarte a las naciones desde muy lejos, y les silbará desde el fin de la tierra. He aquí que vendrán rápida y velozmente.
Atapandisha bendera ya ishara mabali na mataifa na atapuliza filimbi kwa wale walio mwisho wa nchi. Tazama watakuja wakikimbia mara moja.
27 Nadie se cansará ni tropezará entre ellos; nadie se adormecerá ni dormirá, ni se desatará el cinturón de su cintura, ni se rompa la correa de sus sandalias,
Hakuna tairi wala mashaka miongoni mwao; hakuna asinzae wala kulala usingizi. Au kama mkanda uliolegea, wala kamba za viatu kukatika.
28 cuyas flechas son afiladas, y todos sus arcos doblados. Los cascos de sus caballos serán como el pedernal, y sus ruedas como un torbellino.
Mishale yao ni mikali na upinde wao umejikunja; kwato za farasi wao' ni kama jiwe, na gari lao magurudumu yake ni kama miba.
29 Su rugido será como el de una leona. Rugirán como jóvenes leones. Sí, rugirán, y agarrar su presa y llevársela, y no habrá nadie que lo entregue.
Mngurumo wao utakuwa kama wa simba, wataunguruma kama mtoto wa simba. Watanguruma na kukamata mawindo na kuvuta mbali, na hakuna hatakayeokolewa.
30 En aquel día rugirán contra ellos como el rugido del mar. Si uno mira a la tierra, he aquí la oscuridad y la angustia. La luz se oscurece en sus nubes.
Siku hiyo ataunguruma juu ya mawindo kama vile bahari kwa kishindo. Yeyote atakayeangalia nchi, ataona giza na mateso; hata mwanga hutafanjwa kuwa mweusi kwa mawingu.