< Isaías 30 >
1 “¡Ay de los hijos rebeldes — dice el Señor — que toman consejo, pero no de mí; y que se alían, pero no con mi Espíritu, para añadir pecado al pecado;
Bwana asema, “Ole kwa watoto wakaidi, kwa wale wanaotimiza mipango ambayo si yangu, wakifanya makubaliano, lakini si kwa Roho wangu, wakilundika dhambi juu ya dhambi,
2 que se proponen bajar a Egipto sin pedir mi consejo, para fortalecerse en la fuerza del Faraón, y para refugiarse en la sombra de Egipto!
wale washukao kwenda Misri bila kutaka shauri langu, wanaotafuta msaada wa ulinzi wa Farao, watafutao kivuli cha Misri kwa ajili ya kimbilio.
3 Por eso la fuerza del Faraón será su vergüenza, y el refugio en la sombra de Egipto su confusión.
Lakini ulinzi wa Farao utakuwa kwa aibu yenu, kivuli cha Misri kitawaletea fedheha.
4 Porque sus príncipes están en Zoán, y sus embajadores han llegado a Hanes.
Ingawa wana maafisa katika Soani na wajumbe wamewasili katika Hanesi,
5 Todos ellos se avergonzarán a causa de un pueblo que no puede aprovecharles, que no es una ayuda ni un beneficio, sino una vergüenza, y también un oprobio.”
kila mmoja ataaibishwa kwa sababu ya taifa lisilowafaa kitu, ambalo haliwaletei msaada wala faida, bali aibu tu na fedheha.”
6 La carga de los animales del Sur. A través de la tierra de la angustia y del sufrimiento, de la leona y del león, de la víbora y de la serpiente voladora, llevan sus riquezas sobre los hombros de los burros jóvenes, y sus tesoros sobre las jorobas de los camellos, a un pueblo inútil.
Neno kuhusu wanyama wa Negebu: Katika nchi ya taabu na shida, ya simba za dume na jike, ya nyoka mwenye sumu kali na nyoka warukao, wajumbe huchukua utajiri wao juu ya migongo ya punda, hazina zao juu ya nundu za ngamia, kwa lile taifa lisilokuwa na faida,
7 Porque Egipto ayuda en vano y en vano; por eso la he llamado Rahab, la que se queda quieta.
kuvipeleka Misri, ambaye msaada wake haufai kabisa. Kwa hiyo nimemwita “Rahabu Asiyefanya Chochote.”
8 Ahora ve, escríbelo delante de ellos en una tabla, e inscríbelo en un libro, para que quede para los tiempos venideros por siempre y para siempre.
Nenda sasa, liandike neno hili juu ya kibao kwa ajili yao, liandike kwenye kitabu, ili liweze kuwa shahidi milele kwa ajili ya siku zijazo.
9 Porque es un pueblo rebelde, hijos mentirosos, hijos que no quieren escuchar la ley de Yahvé;
Hawa ni watu waasi, watoto wadanganyifu, watoto ambao hawataki kusikiliza mafundisho ya Bwana.
10 que dicen a los videntes: “¡No veas!” y a los profetas: “No nos profeticen cosas buenas. Dígannos cosas agradables. Profetizad engaños.
Wanawaambia waonaji, “Msione maono tena!” Nako kwa manabii wanasema, “Msiendelee kutupatia maono ambayo ni ya kweli! Tuambieni mambo ya kupendeza, tabirini mambo ya uongo.
11 Quítate del camino. Apartaos del camino. Haced que el Santo de Israel deje de estar delante de nosotros”.
Acheni njia hii, ondokeni katika mapito haya, nanyi acheni kutukabili pamoja na yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli!”
12 Por lo tanto, el Santo de Israel dice: “Por cuanto desprecias esta palabra y confías en la opresión y la perversidad, y te apoyas en ella,
Kwa hiyo, hili ndilo asemalo yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli: “Kwa sababu mmekataa ujumbe huu, mkategemea uonevu na kutumainia udanganyifu,
13 por lo tanto, esta iniquidad será para ti como una brecha a punto de caer, que se hincha en un muro alto, cuya ruptura llega de repente en un instante.
dhambi hii itakuwa kwenu kama ukuta mrefu, wenye ufa na wenye kubetuka, ambao unaanguka ghafula, mara moja.
14 La romperá como se rompe una vasija de alfarero, partiéndola en pedazos sin escatimar, de modo que no se encontrará entre los pedazos rotos una pieza lo suficientemente buena para tomar fuego del hogar, o para sacar agua de la cisterna.”
Utavunjika vipande vipande kama chombo cha udongo ukipasuka pasipo huruma ambapo katika vipande vyake hakuna kipande kitakachopatikana kwa kuukulia makaa kutoka jikoni au kuchotea maji kisimani.”
15 Porque así ha dicho el Señor Yahvé, el Santo de Israel: “Te salvarás en el retorno y el descanso. Vuestra fuerza estará en la tranquilidad y en la confianza”. Vosotros os negasteis,
Hili ndilo Bwana Mwenyezi, yeye Aliye Mtakatifu wa Israeli, asemalo: “Katika kutubu na kupumzika ndio wokovu wenu, katika kutulia na kutumaini ndizo nguvu zenu, lakini hamkutaka.
16 pero dijisteis: “No, porque huiremos a caballo”; por tanto, huiréis; y “montaremos en los veloces”; por tanto, los que os persigan serán veloces.
Mlisema, ‘Hapana, tutakimbia kwa farasi.’ Kwa hiyo mtakimbia! Mlisema, ‘Tutakimbia kwa farasi waendao kasi.’ Kwa hiyo wanaowafukuza watakwenda kasi!
17 Mil huirán ante la amenaza de uno. Ante la amenaza de cinco, huiréis hasta quedar como un faro en la cima de una montaña, y como un estandarte en una colina.
Watu 1,000 watakimbia kwa ajili ya kitisho cha mtu mmoja, kwa vitishio vya watu watano wote mtakimbia, hadi mtakapoachwa kama mlingoti wa bendera juu ya kilele cha mlima, kama bendera juu ya kilima.”
18 Por eso Yahvé esperará, para que tenga piedad de ustedes; y por eso será exaltado, para que tenga piedad de ustedes, porque Yahvé es un Dios de justicia. Bienaventurados todos los que lo esperan.
Hata hivyo Bwana anatamani kutupatia neema, anainuka ili kuwaonyesha huruma. Kwa kuwa Bwana ni Mungu wa haki. Wamebarikiwa wote wanaomngojea yeye!
19 Porque el pueblo habitará en Sión, en Jerusalén. No llorará más. Ciertamente, él se apiadará de ti a la voz de tu clamor. Cuando te escuche, te responderá.
Enyi watu wa Sayuni, mnaoishi Yerusalemu, hamtalia tena. Tazameni jinsi atakavyokuwa na huruma mtakapolia kwa kumwomba msaada! Mara asikiapo, atawajibu.
20 Aunque el Señor te dé el pan de la adversidad y el agua de la aflicción, tus maestros ya no estarán ocultos, sino que tus ojos verán a tus maestros;
Ingawa Bwana huwapa chakula cha shida na maji ya taabu, walimu wenu hawatafichwa tena, kwa macho yenu wenyewe mtawaona.
21 y cuando te gires a la derecha, y cuando te gires a la izquierda, tus oídos oirán una voz detrás de ti, que dirá: “Este es el camino. Camina por él”.
Mkigeuka kuume au kushoto, masikio yenu yatasikia sauti nyuma yenu ikisema, “Hii ndiyo njia, ifuateni.”
22 Profanarás el revestimiento de tus imágenes grabadas de plata y el revestimiento de tus imágenes fundidas de oro. Las desecharás como cosa inmunda. Le dirás: “¡Vete!”
Kisha mtanajisi sanamu zenu zilizofunikwa kwa fedha, na vinyago vyenu vilivyofunikwa kwa dhahabu. Mtazitupilia mbali kama vitambaa vya wakati wa hedhi na kuziambia, “Haya, tokeni hapa!”
23 Él dará la lluvia para tu semilla, con la que sembrarás la tierra; y el pan del crecimiento de la tierra será rico y abundante. En ese día, tu ganado se alimentará en grandes pastos.
Pia atawapa mvua kwa ajili ya mbegu mnazootesha ardhini, chakula kinachotoka ardhini kitakuwa kizuri sana, tena tele. Katika siku ile, ngʼombe wenu watalisha katika shamba pana la majani.
24 También los bueyes y los asnos jóvenes que cultivan la tierra comerán un alimento sabroso, que ha sido aventado con la pala y con el tenedor.
Maksai na punda walimao watakula majani makavu na vyakula vilivyotengenezwa, vinavyotandazwa kwa uma na sepeto.
25 Habrá arroyos y corrientes de agua en toda montaña elevada y en todo cerro alto en el día de la gran matanza, cuando caigan las torres.
Katika siku ile ya mauaji makuu, wakati minara itakapoanguka, vijito vya maji vitatiririka juu ya kila mlima mrefu na kila kilima kilichoinuka sana.
26 Además, la luz de la luna será como la luz del sol, y la luz del sol será siete veces más brillante, como la luz de siete días, el día en que Yahvé cure la fractura de su pueblo y sane la herida con que fue herido.
Mwezi utaangaza kama jua, nao mwanga wa jua utangʼaa mara saba zaidi, kama nuru ya siku saba, wakati Bwana atakapoyafunga majeraha ya watu wake na kuwaponya vidonda alivyowatia.
27 He aquí que el nombre de Yahvé viene de lejos, ardiendo con su cólera y en espeso humo creciente. Sus labios están llenos de indignación. Su lengua es como un fuego devorador.
Tazama, Jina la Bwana linakuja kutoka mbali, likiwa na hasira kali inayowaka pamoja na wingu zito la moshi, midomo yake imejaa ghadhabu na ulimi wake ni moto ulao.
28 Su aliento es como un torrente desbordante que llega hasta el cuello, para tamizar a las naciones con el cedazo de la destrucción. Un freno que lleva a la ruina estará en las fauces de los pueblos.
Pumzi yake ni kama mkondo wa maji yaendayo kasi, yakipanda hadi shingoni. Hutikisa mataifa katika chekecheke ya uharibifu, huweka lijamu katika mataya ya mataifa ambayo huwaongoza upotevuni.
29 Tendrás un canto, como en la noche en que se celebra una fiesta sagrada, y alegría de corazón, como cuando se va con una flauta a venir al monte de Yahvé, a la Roca de Israel.
Nanyi mtaimba kama usiku ule mnaadhimisha sikukuu takatifu. Mioyo yenu itashangilia kama vile watu wanapokwea na filimbi kwenye mlima wa Bwana, kwa Mwamba wa Israeli.
30 Yahvé hará oír su voz gloriosa y mostrará el descenso de su brazo, con la indignación de su cólera y la llama de un fuego devorador, con ráfaga, tormenta y granizo.
Bwana atawasababisha watu waisikie sauti yake ya utukufu, naye atawafanya wauone mkono wake ukishuka pamoja na hasira yake kali na moto ulao, kukiwa na tufani ya mvua, ngurumo za radi na mvua ya mawe.
31 Porque por la voz de Yahvé el asirio será desalentado. Lo golpeará con su vara.
Sauti ya Bwana itaivunjavunja Ashuru, kwa fimbo yake ya utawala atawapiga.
32 Cada golpe de la vara de castigo que Yahvé impondrá sobre él, será con el sonido de panderetas y arpas. Luchará con ellos en las batallas, blandiendo armas.
Kila pigo Bwana atakaloliweka juu yao kwa fimbo yake ya kuadhibu, litakuwa kwa wimbo wa matari na vinubi, anapopigana nao katika vita kwa mapigo ya mkono wake.
33 Porque su lugar de ardor está preparado desde hace tiempo. Sí, está preparado para el rey. Ha hecho su pira profunda y grande con fuego y mucha leña. El aliento de Yahvé, como una corriente de azufre, lo enciende.
Tofethi imeandaliwa toka zamani, imewekwa tayari kwa ajili ya mfalme. Shimo lake la moto limetengenezwa kwa kina kirefu na kwa upana mkubwa, likiwa na moto na kuni tele; pumzi ya Bwana, kama kijito cha kiberiti, huuwasha moto.