< Ezequiel 27 >

1 La palabra de Yahvé volvió a dirigirse a mí, diciendo:
Neno la Bwana likanijia kusema:
2 “Tú, hijo de hombre, levanta un lamento sobre Tiro;
“Mwanadamu, fanya maombolezo kwa ajili ya Tiro.
3 y dile a Tiro: ‘Tú que habitas a la entrada del mar, que eres el mercader de los pueblos a muchas islas, el Señor Yahvé dice: “Tú, Tiro, has dicho, ‘Soy perfecto en belleza’.
Umwambie Tiro, ulioko kwenye lango la bahari, ufanyao biashara na mataifa mengi ya pwani, ‘Hili ndilo Bwana Mwenyezi asemalo: “‘Ee Tiro, wewe umesema, “Mimi ni mkamilifu katika uzuri.”
4 Sus fronteras están en el corazón de los mares. Tus constructores han perfeccionado tu belleza.
Mipaka yako ilikuwa katika moyo wa bahari, wajenzi wako walikamilisha uzuri wako.
5 Han hecho todas tus tablas de ciprés de Senir. Han tomado un cedro del Líbano para hacer un mástil para ti.
Walizifanya mbao zako zote kwa misunobari itokayo Seniri; walichukua mierezi kutoka Lebanoni kukutengenezea mlingoti.
6 Han hecho tus remos de los robles de Basán. Han hecho tus bancos de marfil con incrustaciones de madera de ciprés de las islas de Kittim.
Walichukua mialoni toka Bashani wakakutengenezea makasia yako; kwa miti ya msanduku kutoka pwani ya Kitimu wakatengeneza sitaha yako na kuipamba kwa pembe za ndovu.
7 Tu vela era de lino fino con bordados de Egipto, que te sirva de estandarte. Azul y púrpura de las islas de Elishah era su toldo.
Kitani safi kilichotariziwa kutoka Misri kilikuwa tanga lako, nacho kilikuwa bendera yako; chandarua chako kilikuwa cha rangi ya buluu na ya zambarau kutoka visiwa vya Elisha.
8 Los habitantes de Sidón y de Arvad eran sus remeros. Tus sabios, Tiro, estaban en ti. Eran sus pilotos.
Watu kutoka Sidoni na Arvadi walikuwa wapiga makasia yako; watu wako wenye ustadi, ee Tiro, walikuwa ndio mabaharia wako.
9 Los ancianos de Gebal y sus sabios fueron sus reparadores de costuras de barcos en ti. Todas las naves del mar con sus marineros estaban en ti para comerciar con su mercancía.
Wazee wa Gebali pamoja na mafundi stadi walikuwa mafundi wako melini. Meli zote za baharini na mabaharia wao walikuja kwako ili kubadilishana bidhaa zako.
10 “‘“Persia, Lud y Put estaban en tu ejército, sus hombres de guerra. Colgaron el escudo y el casco en ti. Mostraron tu belleza.
“‘Watu wa Uajemi, Ludi na Putu walikuwa askari katika jeshi lako. Walitundika ngao zao na chapeo zao kwenye kuta zako, wakileta fahari yako.
11 Los hombres de Arvad con su ejército estaban en sus murallas por todas partes, y los hombres valientes estaban en sus torres. Colgaron sus escudos en sus paredes por todas partes. Han perfeccionado tu belleza.
Watu wa Arvadi na wa Heleki walikuwa juu ya kuta zako pande zote; watu wa Gamadi walikuwa kwenye minara yako. Walitundika ngao zao kuzizunguka kuta zako; wakaukamilisha uzuri wako.
12 “‘“Tarsis era tu mercader por la multitud de toda clase de riquezas. Comerciaban por tus mercancías con plata, hierro, estaño y plomo.
“‘Tarshishi walifanya biashara nawe kwa sababu ya utajiri wako mkubwa wa bidhaa, walibadilisha fedha, chuma, bati na risasi kwa mali zako.
13 “‘“Javan, Tubal y Meshech eran tus comerciantes. Ellos cambiaron las personas de los hombres y los recipientes de bronce por tus mercancías.
“‘Uyunani, Tubali na Mesheki, walifanya biashara nawe, walibadilisha watumwa na vyombo vya shaba kwa bidhaa zako.
14 “‘“Los de la casa de Togarmah comerciaban con tus mercancías con caballos, caballos de guerra y mulas.
“‘Watu wa Beth-Togarma walibadilisha farasi wa mizigo, farasi wa vita na nyumbu kwa mali zako.
15 “‘“Los hombres de Dedán comerciaban contigo. Muchas islas fueron el mercado de tu mano. Te trajeron a cambio cuernos de marfil y ébano.
“‘Watu wa Dedani walifanya biashara nawe, watu wengi wa nchi za pwani walikuwa wachuuzi wako, walikulipa kwa pembe za ndovu na mpingo.
16 “‘“Siria fue tu mercader por la multitud de tus trabajos manuales. Ellos comerciaban por tus mercancías con esmeraldas, púrpura, bordados, lino fino, coral y rubíes.
“‘Watu wa Aramu walifanya biashara nawe kwa ajili ya wingi wa kazi za mikono yako, wakibadilishana kwa almasi, vitambaa vya rangi ya zambarau, vitambaa vilivyotariziwa, kitani safi, matumbawe na akiki nyekundu.
17 “‘“Judá y la tierra de Israel fueron tus comerciantes. Comerciaban con el trigo de Minnith, los dulces, la miel, el aceite y el bálsamo por tus mercancías.
“‘Yuda na Israeli walifanya biashara nawe, walibadilishana kwa ngano kutoka Minithi, mtama, asali, mafuta na zeri ya kuponyeshea.
18 “‘“Damasco fue tu mercader por la multitud de tus obras, por la multitud de toda clase de riquezas, con el vino de Helbón y la lana blanca.
“‘Dameski, kwa sababu ya wingi wa kazi za mikono yako na ukuu wa utajiri wa mali, walifanya biashara nawe wakibadilishana mvinyo kutoka Helboni na sufu kutoka Zahari.
19 “‘“Vedan y Javan comerciaron con hilo para sus mercancías; el hierro forjado, la casia y el cálamo estaban entre sus mercancías.
“‘Wadani na Wayunani kutoka Uzali, walikuletea mali za biashara, nao wakabadilishana nawe chuma kilichofuliwa, mdalasini na mchaichai.
20 “‘“Dedán era tu mercader en preciosas mantas para montar a caballo.
“‘Dedani alifanya biashara nawe kwa matandiko ya farasi.
21 “‘“Arabia y todos los príncipes de Cedar eran tus comerciantes favoritos de corderos, carneros y cabras. En estos, eran tus comerciantes.
“‘Arabuni na wakuu wote wa Kedari walikuwa wanunuzi wako waliobadilishana bidhaa zako na wana-kondoo, kondoo dume na mbuzi.
22 “‘“Los comerciantes de Saba y Raamah eran tus comerciantes. Comerciaban por tus mercancías con lo mejor de todas las especias, todas las piedras preciosas y el oro.
“‘Wafanyabiashara wa Sheba na wa Raama walifanya biashara nawe, wakabadilishana bidhaa zako na aina zote za vikolezi, vito vya thamani na dhahabu.
23 “‘“Harán, Canneh, Edén, los comerciantes de Sabá, Asur y Chilmad, eran tus comerciantes.
“‘Harani, Kane na Edeni na wafanyabiashara wa Sheba, Ashuru na Kilmadi walifanya biashara nawe.
24 Estos eran tus comerciantes en mercancías selectas, en envoltorios de azul y bordados, y en cofres de cedro de ricas ropas atadas con cuerdas, entre tus mercancías.
Kwenye soko lako, walifanya biashara nawe kwa mavazi mazuri, vitambaa vya buluu, nguo za kutariziwa na mazulia ya rangi mbalimbali yenye kamba zilizosokotwa na kuwekwa mafundo imara.
25 “‘“Los barcos de Tarsis eran tus caravanas para tus mercancías. Te reabasteciste y hecho muy glorioso en el corazón de los mares.
“‘Merikebu za Tarshishi ndizo zinazokusafirishia bidhaa zako. Umejazwa shehena kubwa katika moyo wa bahari.
26 Tus remeros te han llevado a grandes aguas. El viento del este te ha roto en el corazón de los mares.
Wapiga makasia wako wanakupeleka mpaka kwenye maji makavu. Lakini upepo wa mashariki umekuvunja vipande vipande katika moyo wa bahari.
27 Tus riquezas, tus mercancías, tu mercadería, sus marineros, sus pilotos, sus reparadores de costuras de barcos, los distribuidores de su mercancía, y todos tus hombres de guerra que están en ti, con toda la compañía que hay entre vosotros, caerá en el corazón de los mares en el día de tu ruina.
Utajiri wako, bidhaa zako na mali zako, mabaharia wako, manahodha wako, mafundi wako wa meli, wafanyabiashara wako na askari wako wote, na kila mmoja aliyeko melini atazama kwenye moyo wa bahari siku ile ya kuvunjika kwa meli yako.
28 Al sonido del grito de tus pilotos, las tierras de pastoreo temblarán.
Nchi za pwani zitatetemeka wakati mabaharia wako watakapopiga kelele.
29 Todos los que manejan los remos, los marineros y todos los pilotos del mar, bajarán de sus barcos. Se pararán en la tierra,
Wote wapigao makasia wataacha meli zao, mabaharia wote na wanamaji wote watasimama pwani.
30 y hará que su voz se escuche sobre ti, y llorará amargamente. Levantarán polvo sobre sus cabezas. Se revolcarán en las cenizas.
Watapaza sauti zao na kulia sana kwa ajili yako; watajitupia mavumbi juu ya vichwa vyao na kujivingirisha kwenye majivu.
31 Se quedarán calvos por ti, y se visten de saco. Llorarán por ti con amargura de alma, con amargo luto.
Watanyoa nywele zao kwa ajili yako, nao watavaa nguo za magunia. Watakulilia kwa uchungu wa moyo na kwa maombolezo makuu.
32 En sus lamentos se lamentarán por ti, y se lamentan por ti, diciendo, ‘¿Quién hay como Tiro, como la que es llevada al silencio en medio del mar”.
Watakapokuwa wanalia na kuomboleza juu yako, watafanya maombolezo kukuhusu wakisema: “Ni nani aliyepata kuangamizwa kama Tiro, katika moyo wa bahari?”
33 Cuando sus mercancías vinieron de los mares, llenasteis muchos pueblos. Has enriquecido a los reyes de la tierra con la multitud de tus riquezas y de tus mercancías.
Wakati bidhaa zako zilipotoka baharini, ulitosheleza mataifa mengi; kwa wingi wa utajiri wako na bidhaa zako ulitajirisha wafalme wa dunia.
34 En el tiempo en que fuiste quebrado por los mares, en las profundidades de las aguas, su mercancía y toda su empresa cayó dentro de usted.
Sasa umevunjavunjwa na bahari, katika vilindi vya maji, bidhaa zako na kundi lako lote vimezama pamoja nawe.
35 Todos los habitantes de las islas se asombran de ti, y sus reyes están terriblemente asustados. Tienen problemas en la cara.
Wote waishio katika nchi za pwani wanakustaajabia; wafalme wao wanatetemeka kwa hofu kuu, nazo nyuso zao zimekunjamana kwa woga.
36 Los mercaderes de los pueblos te silban. Has llegado a un final terrible, y ya no serás más””.
Wafanyabiashara miongoni mwa mataifa wanakucheka; umefikia mwisho wa kutisha nawe hutakuwepo tena.’”

< Ezequiel 27 >