< Éxodo 7 >
1 Yahvé dijo a Moisés: “He aquí que te he puesto como Dios ante el Faraón, y Aarón tu hermano será tu profeta.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Tazama, nimekufanya kuwa kama Mungu kwa Farao, naye Aroni, huyo ndugu yako, atakuwa nabii wako.
2 Tú hablarás todo lo que yo te mande; y Aarón tu hermano hablará al Faraón para que deje salir a los hijos de Israel de su tierra.
Utasema kila kitu nitakachokuagiza, naye Aroni ndugu yako atamwambia Farao awaachie Waisraeli watoke katika nchi yake.
3 Yo endureceré el corazón del Faraón, y multiplicaré mis señales y mis prodigios en la tierra de Egipto.
Lakini nitaufanya moyo wa Farao kuwa mgumu. Ingawa nitazidisha ishara na maajabu katika Misri,
4 Pero el Faraón no te escuchará, así que pondré mi mano sobre Egipto y sacaré a mis ejércitos, a mi pueblo los hijos de Israel, de la tierra de Egipto con grandes juicios.
hatawasikiliza. Kisha nitaupeleka mkono wangu juu ya Misri, na kwa matendo makuu ya hukumu nitavitoa vikundi vyangu, watu wangu Waisraeli.
5 Los egipcios sabrán que yo soy Yahvé cuando extienda mi mano sobre Egipto y saque a los hijos de Israel de entre ellos.”
Nao Wamisri watajua kuwa Mimi ndimi Bwana nitakapounyoosha mkono wangu dhidi ya Misri na kuwatoa Waisraeli watoke humo.”
6 Moisés y Aarón lo hicieron. Como el Señor les ordenó, así lo hicieron.
Mose na Aroni wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyowaagiza.
7 Moisés tenía ochenta años, y Aarón ochenta y tres, cuando hablaron con el faraón.
Mose alikuwa na umri wa miaka themanini na Aroni alikuwa na umri wa miaka themanini na mitatu walipozungumza na Farao.
8 Yahvé habló a Moisés y a Aarón, diciendo:
Bwana akamwambia Mose na Aroni,
9 “Cuando el Faraón les hable diciendo: ‘Hagan un milagro’, entonces le dirán a Aarón: ‘Toma tu vara y arrójala ante el Faraón, y se convertirá en una serpiente’”.
“Farao atakapowaambia, ‘Fanyeni muujiza,’ basi mwambie Aroni, ‘Chukua fimbo yako na uitupe chini mbele ya Farao,’ nayo fimbo itakuwa nyoka.”
10 Moisés y Aarón se presentaron ante el faraón, y así lo hicieron, tal como lo había ordenado el Señor. Aarón arrojó su vara ante el Faraón y ante sus servidores, y se convirtió en una serpiente.
Ndipo Mose na Aroni wakaenda kwa Farao wakafanya sawasawa kama vile Bwana alivyoagiza. Aroni akaitupa ile fimbo yake chini mbele ya Farao na maafisa wake, nayo ikawa nyoka.
11 Entonces el faraón llamó también a los sabios y a los hechiceros. Ellos también, los magos de Egipto, hicieron lo mismo con sus encantamientos.
Farao naye akawaita watu wenye maarifa na wachawi na waganga wa Kimisri, nao wakafanya vivyo hivyo kwa siri ya uganga wao.
12 Cada uno de ellos arrojó su vara y se convirtió en serpiente; pero la vara de Aarón se tragó sus varas.
Kila mmoja alitupa fimbo yake chini, nayo ikawa nyoka. Lakini fimbo ya Aroni ikazimeza zile fimbo zao.
13 El corazón del faraón se endureció y no los escuchó, como había dicho el Señor.
Hata hivyo moyo wa Farao ukawa mgumu, naye hakuwasikiliza Mose na Aroni, sawasawa kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
14 El Señor dijo a Moisés: “El corazón del faraón es obstinado. Se niega a dejar ir al pueblo.
Kisha Bwana akamwambia Mose, “Moyo wa Farao ni mgumu, anakataa kuwaachia watu kuondoka.
15 Ve a ver al faraón por la mañana. He aquí que él va a salir al agua. Tú estarás a la orilla del río para recibirlo. Tomarás en tu mano la vara convertida en serpiente.
Nenda kwa Farao asubuhi wakati anapokwenda mtoni. Ngoja ukingoni mwa Naili ili uonane naye, na uchukue mkononi mwako fimbo ile iliyobadilishwa kuwa nyoka.
16 Le dirás: “Yahvé, el Dios de los hebreos, me ha enviado a ti, diciendo: “Deja ir a mi pueblo, para que me sirva en el desierto. He aquí que hasta ahora no has hecho caso”.
Kisha umwambie, ‘Bwana, Mungu wa Waebrania, amenituma nikuambie: Waachie watu wangu waende, ili wapate kuniabudu jangwani. Lakini hadi sasa hujasikiliza.
17 Yahvé dice: “En esto sabrán que yo soy Yahvé. Miren: Golpearé con la vara que tengo en mi mano las aguas que están en el río, y se convertirán en sangre.
Hili ndilo Bwana asemalo: Kwa hili utajua kuwa Mimi ndimi Bwana: Fimbo iliyo mkononi mwangu nitapiga nayo maji ya Naili nayo yatabadilika kuwa damu.
18 Los peces que están en el río morirán y el río se ensuciará. Los egipcios detestarán beber agua del río”.
Samaki waliomo katika Mto Naili watakufa, nao mto utanuka vibaya, Wamisri hawataweza kunywa hayo maji yake.’”
19 Yahvé dijo a Moisés: “Dile a Aarón: ‘Toma tu vara y extiende tu mano sobre las aguas de Egipto, sobre sus ríos, sobre sus arroyos y sobre sus estanques, y sobre todos sus estanques de agua, para que se conviertan en sangre. Habrá sangre en toda la tierra de Egipto, tanto en los recipientes de madera como en los de piedra’”.
Bwana akamwambia Mose, “Mwambie Aroni, ‘Chukua ile fimbo yako unyooshe mkono wako juu ya maji ya Misri, juu ya chemchemi na mifereji, juu ya madimbwi na mabwawa yote,’ navyo vitabadilika kuwa damu. Damu itakuwa kila mahali katika Misri, hata kwenye vyombo vya miti na vya mawe.”
20 Moisés y Aarón lo hicieron así, tal como lo había ordenado el Señor, y él levantó la vara y golpeó las aguas que estaban en el río, a la vista del Faraón y de sus servidores, y todas las aguas que estaban en el río se convirtieron en sangre.
Mose na Aroni wakafanya kama vile Bwana alivyokuwa amewaagiza. Akainua fimbo yake machoni pa Farao na maafisa wake na kuyapiga maji ya Mto Naili, na maji yote yakabadilika kuwa damu.
21 Los peces que había en el río murieron. El río se volvió fétido. Los egipcios no podían beber agua del río. La sangre se extendió por toda la tierra de Egipto.
Samaki katika Mto Naili wakafa, nao mto ukanuka vibaya sana kiasi kwamba Wamisri hawakuweza kunywa maji yake. Damu ilikuwa kila mahali katika nchi ya Misri.
22 Los magos de Egipto hicieron lo mismo con sus encantamientos. Así que el corazón del faraón se endureció y no les hizo caso, como había dicho el Señor.
Lakini waganga wa Misri kwa kutumia siri ya uganga wao wakafanya vivyo hivyo, nao moyo wa Farao ukawa mgumu, hakuwasikiliza Mose na Aroni, kama vile Bwana alivyokuwa amesema.
23 El faraón se volvió y entró en su casa, y ni siquiera lo tomó en cuenta.
Badala yake, Farao akageuka, akaenda kwenye jumba lake la kifalme, wala hakulitia hili moyoni.
24 Todos los egipcios cavaron alrededor del río en busca de agua para beber, porque no podían beber el agua del río.
Nao Wamisri wote wakachimba kandokando ya Mto Naili kupata maji ya kunywa, kwa sababu hawakuweza kunywa maji ya mto.
25 Se cumplieron siete días, después de que el Señor golpeó el río.
Zilipita siku saba baada ya Bwana kuyapiga maji ya Mto Naili.